Ameandika Edo Kumwembe

Hivi Edo Kumwembe naye ni mchambuzi wa soka? Ni lini amelijua soka hata kuwa mchambuzi wa soka? Ni lini amecheza soka kwa kiwango cha juu kisha kujiweka kwenye uchambuzi wake? Anawalaumu bure wenzake maana wote wao na yeye soka hawalijui. Afadhali wenzake wameona wajazie upungufu wao kwa kuchambua yasiyohusiana na soka lakini angalau yako jirani na soka na wanaweza kuzoza hapo!!

Uchambuzi wa soka hapa bongo waachiwe kina Ally Mayai Tembele na wenzake waliowahi kuujua na kuucheza mpira!! Nyie akina Kumwembe mnakera sana wala huna tofauti yoyote na wenzako!!
 
Mmmmh
 
Ukipunguza chuki na hasira unaweza kujua tofauti ya Eddo na hao wenzake uliowaandika..... halafu wapi wamesema ili uwe mchambuzi lzm uwe umecheza soka kwa kiwango cha juu!!
 
Atleast jamaa sio mfia tumbo kama hao wachambuzi waliotangulia ufukara mbele kuliko weledi.
 
in general hii industry ina tatizo kubwa sana. kuanzia watangazaji, wamiliki nk. yan station za siku hizi ni ujinga mtupu kusikiliza. mmiliki anaajiri mashoga, wambea, chawa, watu hawajui ueledi yan ukiweza kuropoka maneno ovyo tu unaajiriwa. hivi mwajiri unawezaje kuajiri mtu kama juma lokole ktk radio yako? ili uionyeshe au uiambie nn jamii? Huku kwenye uchambuzi wa soka ndo balaa wameona chaka la kujificha mtu hajui lolote kuhusu soka analisemea soka. yan shida tupu. radio hakizingatii ratiba. kipindi kinaisha saa 1 kamili wao wanabwabwaja hadi saa 1 na robo. mara wanamualika mgeni wanamuuliza swali kabla hajajibu wanamkatisha sijui tangazo. mara mchongo pesa vurugu tupu
 
Huyo Edo ni mpiga domo tu kwa kuwa mpira unapendwa na watu wengi basi nao wanaojiita wachambuzi wanapata kula yao hapo maana kuna wengi wanaopenda kusikiliza domo lolote linalopigwa kuhusu mpira.

Unachambua nini kuhusu mechi wakati kila mtu anaona mechi inavyochezwa?

Ni mara kumi hao wanaoongelea mikataba maana vilabu vyetu kwenye uwazi bado sana. Mikataba haiwekwi hadharani, tunaambiwa tu kuna hiki na hiki basi.

Kwa hiyo mwandishi au mtangazaji ambaye angalau naweza kumpa pointi ni yule atakayepeleleza na kuupata mkataba na akauweka hadharani. Ila sijamuona bado mwandishi wa hivyo.

Lakini sio eti unatuchambulia mechi. Sasa unachambua nini wakati mechi na sisi tumeiona. Yaani ukae eti unatuambia fulani fulani walicheza vizuri au timu fulani ilipwaya eneo fulani? Si wote tumeiona mechi!
 
Ukipunguza chuki na hasira unaweza kujua tofauti ya Eddo na hao wenzake uliowaandika..... halafu wapi wamesema ili uwe mchambuzi lzm uwe umecheza soka kwa kiwango cha juu!!
Si lazima uwe umecheza mpira ili uwe mchambuzi mzuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…