Amebadilika siku chache kabla ya mahari


Kuna kitu nimegundua kwenye familia hasa wakati wa ndoa. Kuna wanafiki watajitokeza na kusema maneno watakayo yasema, ili ndoa isifanyike halafu wapate wacheke pembeni. Lakini wakija kwenye kikao cha posa(ndoa) hujifanya kondoo ila nafsi zao za chui. Ushauri wangu kwako mpigie mwenza wako simu mwambie hivi:- KAMA UNANIPENDA NA UNATAKA UWE NA MIMI MILELE MWENYEZI MUNGU ATAKULETA NA NDOA YA KHERI ITAFANYIKA. KAMA SIO RISKI YANGU INSHALLAH MWENYEZI MUNGU AKUPE MWENYE KHERI NAWE PAMOJA NA MIMI.
Mwanaume wa kweli atayatafakari sana hayo maneno, baada ya hapo omba kwa Mola wako akufanyie wepesi pia toa sadaka kwa mnyama au wadudu(sukari kwa sisimizi au dagaa kwa paka) hakika sadaka huleta Amani ya Moyo na furaha ya nafsi.



Kwioooo [emoji239][emoji239][emoji239]
 
Kwani wewe unataka shoo au unataka atoe mahali? Miaka minne unakazwa bureee, wewe ndo umebadilika sio yeye wewe si unataka mahali?
Kama mnapendana wapige chini wazazi wako na hizo mahali zao au msubili mwingine.
 
Nimependa hicho kipande cha kutoa sadaka kwa wanyama [emoji3][emoji3][emoji116][emoji116][emoji116]

"toa sadaka kwa mnyama au wadudu(sukari kwa sisimizi au dagaa kwa paka) hakika sadaka huleta Amani ya Moyo na furaha ya nafsi"
 
Mahari alipangiwa alipe kiasi gani?tuanzie hapo
 
nafdat dada yangu mpendwa;
Pole kwa changamoto hii.
Najua unapitia kipindi kigumu sana.
Huenda mwenzio aliiuwa hajamaanisha zaidi aliona amepata mteremko wa kupata free p.

Wanawake mnapitia magumu sana.
Nikushauri kuwa uwe jasiri, idharau aibu.
Mimi ni Mkristo kuna mstari huwa unanitia nguvu naomba kushea;

(5 Iweni na nia iyo hiyo ndani yenu ambayo ilikuwamo pia ndani ya Kristo Yesu;
Wafilipi 2:5

6 ambaye yeye mwanzo alikuwa yuna namna ya Mungu, naye hakuona kule kuwa sawa na Mungu kuwa ni kitu cha kushikamana nacho;
Wafilipi 2:6

7 bali alijifanya kuwa hana utukufu, akatwaa namna ya mtumwa, akawa ana mfano wa wanadamu;
Wafilipi 2:7

8 tena, alipoonekana ana umbo kama mwanadamu, alijinyenyekeza akawa mtii hata mauti, naam, mauti ya msalaba.
Wafilipi 2:8

9 Kwa hiyo tena Mungu alimwadhimisha mno, akamkirimia Jina lile lipitalo kila jina;
Wafilipi 2:9

10 ili kwa jina la Yesu kila goti lipigwe, la vitu vya mbinguni, na vya duniani, na vya chini ya nchi;
Wafilipi 2:10

11 na kila ulimi ukiri ya kuwa YESU KRISTO NI Bwana, kwa utukufu wa Mungu Baba.
Wafilipi 2:11)
Maneno hayo maana yake ni kuwa Yesu ambaye alikuwa na utukufu, kuna wakati alikubali kuaibika na hakuona kuwa ni tatizo bali aliutazama utukufu mpya ujao.
Hakukwepa aibu bali aliikabili ndipo alipoishinda aibu Mungu alimuadhimisha mno au alimpa utukufu mpya.

Dada iiabili aibu huku ukimsubiri mume wako bora kabisa.
Mungu atakupa kitu bora kabisa..tulia.

Yatunze haya maneno.
 
me kuna kaka mmoja alikuwaga ananificha kweli mambo yake, nikawa najiuliza huyu mtu mbona ana fichaficha vitu shida ni nini? kuja kutahamaki, kijana ana mtoto mchanga wa kike. aiseee nilikonda ndani ya siku moja. na ukiangalia mahusiano wameanza tokea muda ila kaka anaficha tu. ikabidi nijiondoe tu kwenye hayo mahusiano for the sake ya huyo kichanga.... duniani watu wana siri. yaani unaweza kubaki mdomo wazi
 
kumbe ndoa ni riziki
anyway hiyo ni njia ya kuachwa pia
 
Itakuumiza sana kwa ssbabu ana alama moyoni mwako.Ila ukiiruhusu akuli yako ifanye kazi bila kuathiriea na kemikali za homoni ya mapenzi.Ni kwamba hakutaki.
Dawa ni moja,kubali kuwa utaumia sana,lakini with time uta heal.
Alafu maisha yataendelea.Usilazimishe mahusiano
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…