Amechaguliwa na Mungu': Wakristo wanaomwona Trump kama mwokozi wao
Akiwa amesimama kwenye jukwaa katika kituo cha mikutano cha Florida usiku wa uchaguzi, safu ya bendera za Marekani nyuma yake na umati wa watu wenye furaha wakitazama, Donald Trump alisema: "Watu wengi wameniambia kwamba Mungu aliokoa maisha yangu kwa sababu fulani, na sababu hiyo ilikuwa ni kuokoa nchi yetu na kuirejesha Marekani katika ukuu.”
Hii ilikuwa moja ya mada ya kuvutia zaidi ya kampeni yake ya uchaguzi - kwamba alikuwa amechaguliwa na Mungu. Hata kabla ya jaribio la kumuua mnamo Julai 13 huko Butler, Pennsylvania, mamilioni ya Wamarekani tayari walihisi kuongozwa na imani yao kumuunga mkono rais wa zamani, na sasa ajaye.
Wengine walifanya uchaguzi kwa njia isiyo ya kawaida na kumfananisha Trump na mtu anayetajwa katika Biblia.
Mwaka jana, kwenye kipindi cha Kikristo cha FlashPoint, mwinjilisti wa TV Hank Kunneman alielezea "vita kati ya wema na uovu", na kuongeza: "Kuna kitu juu ya Rais Trump ambacho adui anaogopa: kinaitwa upako."
Source: BBC swahili
Ndio Yessu wao?
Akiwa amesimama kwenye jukwaa katika kituo cha mikutano cha Florida usiku wa uchaguzi, safu ya bendera za Marekani nyuma yake na umati wa watu wenye furaha wakitazama, Donald Trump alisema: "Watu wengi wameniambia kwamba Mungu aliokoa maisha yangu kwa sababu fulani, na sababu hiyo ilikuwa ni kuokoa nchi yetu na kuirejesha Marekani katika ukuu.”
Hii ilikuwa moja ya mada ya kuvutia zaidi ya kampeni yake ya uchaguzi - kwamba alikuwa amechaguliwa na Mungu. Hata kabla ya jaribio la kumuua mnamo Julai 13 huko Butler, Pennsylvania, mamilioni ya Wamarekani tayari walihisi kuongozwa na imani yao kumuunga mkono rais wa zamani, na sasa ajaye.
Wengine walifanya uchaguzi kwa njia isiyo ya kawaida na kumfananisha Trump na mtu anayetajwa katika Biblia.
Mwaka jana, kwenye kipindi cha Kikristo cha FlashPoint, mwinjilisti wa TV Hank Kunneman alielezea "vita kati ya wema na uovu", na kuongeza: "Kuna kitu juu ya Rais Trump ambacho adui anaogopa: kinaitwa upako."
Source: BBC swahili
Ndio Yessu wao?