Amekamilisha taarifa zake zote muhimu kwa ajili ya kubadili jina na amehakikiwa kwa finger print ila kaambiwa asubiri miezi 3 jina ndiyo

nuporo

JF-Expert Member
Joined
Oct 18, 2018
Posts
1,534
Reaction score
3,387
USUMBUFU NIDA:Amekamilisha taarifa zake zote muhimu kwa ajili ya kubadili jina na amehakikiwa kwa finger print ila kaambiwa asubiri miezi 3 jina ndiyo libadilike Kwenye system

Mbona Kwenye usajili wa laini mambo haya hayapo?

Pesa kalipa, uhamiaji kapita na kahakikiwa kila kitu na mhusika ni yeye hata fingerprint zimedhirisha kwanini asubiri miezi 3 ndio jina libadilike?

Mbona jamii forum na WhatsApp unaweza post na kuedit post yako Wala haitaji kusubiri Miezi 3 kwanini iwe NIDA ? na mhusika ni yeye na hatua zote kafuata?
 
Amekamilisha ule usemi wa mkono tupu haulambwi au anakodoa macho tu...??
Hajatoa chochote: kwakuwa hatua zote kafata na kukamilisha kwanini asubiri miezi 3 ndio jina libadilike?
 
Uko mkoa gani?
Kama jirani na Burundi,Rwanda,Congo
Sio raia🤣😂
😁😁 mkoa x mfano wewe unaitwa Ironbutterfly lakini jina lako liandikwe irenbutterfly umefata mchakato wote kuonesha jina lako limekosewa herufi na umelipia na wameconfirm kwa vidole vyako kabisa kuwa ni wewe sasa kubadili irenbutterfly kuwa ironbutterfly ndio ichukue miezi 3. ?
 
Kuna watu wa pembezoni siyo raia.

So wanatumia siku 90 kujidhihirisha Kama ni raia au damu ya kagame🤣

Jiongeze👌

Hatutaki interahamwe tized👌
 
Kuna watu wa pembezoni siyo raia
So wanatumia siku 90 kujidhihirisha Kama ni raia au damu ya kagame[emoji1787]
Jiongeze[emoji108]
Hatutaki interahamwe tized[emoji108]
Kama uhamiaji wamejiridhisha

Hakuna mamlaka nyingine kisheria yenye jukumi hilo.

Hakuna Cha siku 90 kisheria, au utuambie hayo mamlaka NIDA wanayatoa wapi?
 
Kwanini anataka kubadili jina tuanzie hapo! Je! Alikuwa muhalifu anataka kujificha?
 
Kubadilisha jina ni tofauti na mtu anaeomba kitambulisho kwa mara ya kwanza kwa majina yake halisi. Unapibadili jina lazima tufanye thorough investigation kujiridhisha je hujafanya uhalifu wowote kwa jina unalolikana? Kwa nini ulikane? Unataka kuficha nini? Process ni ndefu sana kiufupi.
 
case kama yangu, tangu july NIDA hawajashughulikia tatizo langu...mimi nimelipia elfu 20 kwa mtandao lakini bado hakuna majina...nimeapa majina yote yangu ila kitambulisho nataka kitoke kwa jina ninalopendekeza mimi...mpaka leo wapo kimyaa. NIDA hovyo sana
 
Kuwa mpole na mvumilivu hatua iliyofanya ni kubwa.... maombi yako huenda yanafanyiwa uhakiki... subiri muda ufike majina kwenye data base ya Taifa hawafuti tuu na kurekebisha kama post au notes... wakimaliza kufanya uhakiki utapata stahili yako....
 
Lkn ni too primitive miezi 3.🤒
 
Hii ilinikumba mimi pia.Afadhali wewe wamekwambia uje baada ya miezi mitatu

Process nilikamilisha mwaka jana mwezi wa kumi,Nimeenda Nida mara nyingi tu mara leo hivi kesho hivi jina limekuja kubadilishwa mwezi wa tisa mwaka huu, ila kitambulisho nimeambiwa nisitarajie leo wala kesho
 
Ingekuwa ni majina yote hapo sawa lakini herufi moja.. yaani Kama imeandikwa beba unataka iwe baba na vitambulisho vyake vyote anavyo vya kutoka anasoma Hadi kuzaliwa kimendikwa baba, ila NIDA tu wamekosea wameandika beba , ndio ichukue miezi 3? As if bado tunatumia mfumo wa kizamani wa analogia wakati tupo digital.
 
Mkono mtupu haulambwi sheikh wangu
Hata mimi nilifikiri miezi 3 mingi Sana au Kuna namna ya kuzipunguza miezi kutoka miezi 3 badi 24 hours.




Hapo Kama ni kijana kapata nafasi sehemu sehemu itabidi asubiri miezi 3 ndiyo akubaliwe maana NIDA yake ikiingizwa kwenye mfumo majina yake yote yanaonekana pamoja na jina lake lilokosewa herufi mfumo lazima umteme.
 
Kwani wwe una haraka gani,umeambiwa na mamlaka subiri miezi mitatu subiri, kama kuna sehemu taarifa zako zinatakiwa waombe barua endelea na mambo yako hadi hiyo miezi mitatu au watakapokwita ghafla kwa ajili ya mahojiano zaidi kuhusu taarifa zako!!
 
Kama uhamiaji wamejiridhisha

Hakuna mamlaka nyingine kisheria yenye jukumi hilo.

Hakuna Cha siku 90 kisheria, au utuambie hayo mamlaka NIDA wanayatoa wapi?
Hili swali lako umewauuliza NIDA!!? Na wao wanasemaje!!??
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…