Amenogewa na penzi lake (ana wivu mbaya)

Amenogewa na penzi lake (ana wivu mbaya)

Pape

JF-Expert Member
Joined
Dec 11, 2008
Posts
5,487
Reaction score
83
kuna mshikaji wangu fulani ana mpenzi wake. Huyu jamaa alisota sana mpaka kumpata huyo mpenzi ikiwa ni pamoja na kupewa majibu ya kukatisha tamaa hapo mwanzoni. Siku ya siku ilipofika alikabidhiwa ufunguo! Kwasasa ni wapenzi kama wiki 3 hivi! mpenzi wake anasema anampenda sana jamaa ndio maana alikuwa anamchunguza kabla ya kumpa jibu la ndio!

Baada ya wiki moja huyu jamaa amegundua kwamba mpenzi wake ana wivu sana kwani hata jamaa akiwa anachati katika facebook, yahoo anahisi anachati na 'wanawake wengine'. jamaa amemweleza sana na kumtajia hata marafiki zake lakini bibie huyo anaona kama anaibiwa vile! Huyu jamaa ananyumba yake na mpenzie pia ananyumba yake! sasa mamaa anataka kila siku jamaa awe analala kwake (nyumbani kwa bibie) hata kama hawali tunda! Lengo sijui ni kutaka kuwa na uhakika kwamba anapata uhakika kwamba 'haibiwi'...

Jamaa yangu kwakweli anaona kama vile hii ni kero kwani hana nafasi hata ya kuongea na simu kwa uhuru, kuchati na washikaji na hata kutumia muda hapa JF...

Je, atumie mbinu gani kumwelewesha bibie kwani hata yeye anampenda sana na hataki kumpoteza!
 
kuna mshikaji wangu fulani ana mpenzi wake. Huyu jamaa alisota sana mpaka kumpata huyo mpenzi ikiwa ni pamoja na kupewa majibu ya kukatisha tamaa hapo mwanzoni. Siku ya siku ilipofika alikabidhiwa ufunguo! Kwasasa ni wapenzi kama wiki 3 hivi! mpenzi wake anasema anampenda sana jamaa ndio maana alikuwa anamchunguza kabla ya kumpa jibu la ndio!

Baada ya wiki moja huyu jamaa amegundua kwamba mpenzi wake ana wivu sana kwani hata jamaa akiwa anachati katika facebook, yahoo anahisi anachati na 'wanawake wengine'. jamaa amemweleza sana na kumtajia hata marafiki zake lakini bibie huyo anaona kama anaibiwa vile! Huyu jamaa ananyumba yake na mpenzie pia ananyumba yake! sasa mamaa anataka kila siku jamaa awe analala kwake (nyumbani kwa bibie) hata kama hawali tunda! Lengo sijui ni kutaka kuwa na uhakika kwamba anapata uhakika kwamba 'haibiwi'...

Jamaa yangu kwakweli anaona kama vile hii ni kero kwani hana nafasi hata ya kuongea na simu kwa uhuru, kuchati na washikaji na hata kutumia muda hapa JF...

Je, atumie mbinu gani kumwelewesha bibie kwani hata yeye anampenda sana na hataki kumpoteza!
upuuzi mtupu!
 
what did he expected. thumb up kwa huyo mwanamke, mkome kuruka ruka hovyo.
 
mnadanganyana/ibiana tu....wiki 3?....hakuna kitu hapo.
 
Si ndoo hapo!UPUUZI MTUPU!
pole na msiba

nshapoa ndugu na jana tulikuwa na frnd tunamliwaza kidogo......Bora ujiolee baby boy mana naona mapenzi ya uzushi yanachipuka kila kukicha.....
 
Ukipenda BOGA penda na ua lake, so jamaa inabidi apige kimya tuu
 
Mi nadhani kwa wiki tatu, kisha huyo bwana 'ameshachoka' tayari na vituko vya bibie, hapo kuna walakini.

Scenario mojawapo ni kuwa huyo bibie alikuwa na mtu mwingine na sasa amemmwaga ndo akaona arudie kwa jamaa kumdanganya kuwa 'alikuwa anamchunguza'...na kwa vile anajua kuwa ukishapoteza kupata tena sio rahisi ndo anajifanya kuwa na wivu wa kupindukia!

Ninachomshauri huyo bwana ni kuwa akae naye amweleze wazi wazi nini matarajio yake/yao kwenye hiyo meli mpya MV mapenzi, ili baadaye kusije kukatokea kutokuelewana kama hivi!
 
Christmas-Minnie-Mickey-Claus.jpg


A Holy Child born unto us
to redeem a lost world of sin
Filling hearts with love and joy
weary souls He came to win
 
Shida ilikuwa kula tunda kesha kula sasa anaanza visababu
 
Sidhani kama kuna love ambayo inakolea kwa week 3...ni siku ndogo sana yaani na hapo kuna walakini sio bure...ila mwambie jamaa awe makini sana!!
 
Back
Top Bottom