Uchaguzi 2020 Amini nawaambia, ni heri Lissu na Mnyika wawe Bungeni. Wakibaki nje ya Bunge wataisambaratisha CCM!

Uchaguzi 2020 Amini nawaambia, ni heri Lissu na Mnyika wawe Bungeni. Wakibaki nje ya Bunge wataisambaratisha CCM!

VUTA-NKUVUTE

JF-Expert Member
Joined
Nov 25, 2010
Posts
6,137
Reaction score
17,908
Scenario 1: Lissu ameshinda Urais wa Tanzania. Anaunda Serikali. CCM ina wingi wa Wabunge. Inatoa Waziri Mkuu na Mawaziri wengi. Serikali ya Lissu itapelekeshwa na chama chetu tutakavyo na kukistawisha chama kuelekea 2025. CCM itashinda kwa kishindo mwaka 2025.

Scenario 2: Lissu hashindi Urais. Hawi Mbunge. Anabaki kama Makamu Mwenyekiti wa CHADEMA. Anabaki kuwa mwanasiasa wa CHADEMA kukitangaza, kukistawisha na kukipigania chama chake akiutumia Uanasheria wake.

Ataungana na John Mnyika ambaye naye pia hatakuwa Mbunge. CHADEMA itastawi, CCM itasinyaa. Hakika, Lissu na Mnyika wataisambaratisha CCM. Mwaka 2025, CHADEMA haitazuilika katika kuchukua Serikali.

Ni heri Lissu na Mnyika watingwe na Urais na Ubunge. Wakiwa wanasiasa wa kichama zaidi, CCM itapotea kwenye ramani za siasa Tanzania mwaka 2025.

Mzee Tupatupa wa Lumumba (kwasasa Kigoma).
 
Kama ilivyo jina lako hiyo inaitwa .@vuta nkuvute
 
Tutajitahidi wabaki nje ili wasambaratishe mambo 😝😝
 
Wabaki tuu nje wasubirie ubunge wa kuteuliwa na mheshimiwa Rais John Pombe Magufuli. Maendeleo hayana vyama
 
Scenario 1: Lissu ameshinda Urais wa Tanzania. Anaunda Serikali. CCM ina wingi wa Wabunge. Inatoa Waziri Mkuu na Mawaziri wengi. Serikali ya Lissu itapelekeshwa na chama chetu tutakavyo na kukistawisha chama kuelekea 2025. CCM itashinda kwa kishindo mwaka 2025...
Scenario 1: Ikitokea hivyo atawanunua Wabunge wa CCM kama CCM ilivyonunua wa CHADEMA na mambo yataendelea
 
Umetumwa wewe wameshaona ngoma ni nzito sasa wamekutuma uwatengenezee mazingira. Waambie yako maisha nje ya bunge na walisha ya ishi hapo awali kabla ya kuwa wabunge, hofu ya nini sasa?
 
Lissu akishinda Urais na kutangazwa halafu akose wabunge wa kutosha anaweza kulivunja bunge na akaitisha uchaguzi mpya, kumbuka kabla ya kulivunja Bunge anaweza kuwa-impress wananchi kwa mambo baadhi atakayoyafanya akiwa ikulu ambayo ni ya wananchi moja kwa moja hivyo akivunja bunge wananchi wengi watakuwa na imani nayena kumpa wabunge
 
Scenario 1: Lissu ameshinda Urais wa Tanzania. Anaunda Serikali. CCM ina wingi wa Wabunge. Inatoa Waziri Mkuu na Mawaziri wengi. Serikali ya Lissu itapelekeshwa na chama chetu tutakavyo na kukistawisha chama kuelekea 2025. CCM itashinda kwa kishindo mwaka 2025...
Mmehamia huko tena!!?

MAGUFULI4LIFE.
 
Scenario 1: Ikitokea hivyo atawanunua Wabunge wa CCM kama CCM ilivyonunua wa CHADEMA na mambo yataendelea
Atawanunua kwa pesa hiyohiyo ya tuma kwa mpesa au kwa msaada wa watu wa ubelgiji?
 
Post zote za huyu mzee hapa jf hakuna iliyowahi kuwa kweli
 
Lissu akishinda Urais na kutangazwa halafu akose wabunge wa kutosha anaweza kulivunja bunge na akaitisha uchaguzi mpya, kumbuka kabla ya kulivunja Bunge anaweza kuwa-impress wananchi kwa mambo baadhi atakayoyafanya akiwa ikulu ambayo ni ya wananchi moja kwa moja hivyo akivunja bunge wananchi wengi watakuwa na imani nayena kumpa wabunge

Uzuri ni kwamba hawezi kushinda urais

Wapiga kura 29M
Wanachama wa CCM 15M+
Wanachama wa chadema 2M

Na hapo bado wana wajumbe wa serikali za mtaa kwa zaidi ya 97% wanaoishi na wapiga kura usiku na mchana wakihamasishana na kusaidiana, kushinda ni kujiandaa sio kuongea tuu
 
Post zote za huyu mzee hapa jf hakuna iliyowahi kuwa kweli
Zamani enzi za JK alikuwa anajifanya mwanachama wa CCM kindakindaki akawa analipoti "Classified info" kutoka kwenye vikao vikubwa vya chama na serikali na alikuwa anapatia kweli hadi akawa maarufu hapa JF! Sasa kazi yake ni kupiga ramli chonganishi kwa habari za kuokota okota!
 
Chadema namba haziko upande wao, kosa lao hadi leo bado wanaamini siasa za mabarabarani kuliko mikakati ya ushindi.Chadema wafarijika na nyomi, siasa za kizamani.
Baada ya wajumbe kumaliza kazi yao sasa ccm wanaongelea mabalozi.Kama ulifuatilia mkutano wa ufunguzi pale Dodoma, mabalozi wa nyumba kumi mkoa wa Dodoma walialikwa na waliandaliwa jukwaa lao.Wale ndiyo wasaka kura za nyumba kwa nyumba, kitanda kwa kitanda na shuka kwa shuka.Tundu Lissu ajiandae na kipigo cha karne.Jamaa atatia aibu chadema
 
Back
Top Bottom