Amka kijana, jitegemee

JF FARMS

Member
Joined
Jul 23, 2021
Posts
13
Reaction score
17
Naamka asubui naangalia wallet yangu kitandani " dah! amna kitu, Mungu wangu nimekosa nini mimi?". Hii ilikuwa sentensi yangu kila siku nilipokuwa nikiamka na nililaani sana mfumo wa nchi hii kama kijana niliyesoma na mwenye Stahasha ya Biashara ya Uhasibu( B.A. BBA-Acoounting). Nililaumu viongozi wetu ,wazazi wangu na ndugu kwa kukosa ajira ya maana. Siku moja nikajiuliza hivi ningekuwa yatima au ningekuwa mzazi wa watoto watatu ningefanyaje mbona vijana wengi wanamaduka yao, biasharaa zao kama Fredy Vunjabei na kwanini mimi siwezi. Majibu yalikuja baada ya kuamka na kutambua vijana wengi tunaangamia kwa;
  1. Kukaa mitaani na kusikiliza maneno ya watu ambayo ayajengi wala hayaleti chakula kichwani mwetu.
  2. Kubeti kila siku, Kubeti sio kosa ila je unapata fedha ya kujikimu na mahitaji yako unayapata kwenye kubeti.
  3. Ideology mbaya ya kuajiliwa kwa waliosoma .
  4. Maneno ya kukatishana tamaa ya mbona huyu kashindwa, je wewe utaweza?
  5. Kukalia mambo ya simba na yanga, Diamond na Alikiba au ManU na ManCity. aya yote hayawezi kuleta chakula kichwani mwako.
Yafuatayo yanaweza kukupa mwanga katika maisha yako;
  1. Jifunze kuweka budget yako vizuri na punguza matumizi ambayo hayana umuhimu.
  2. Jifunze kutunza kila kiasi kidogo ata 500/= kwenye kibubu au M-pesa, Tigopesa maana kutunza kwako leo kunaweza kukuinua miaka ijayo.
  3. Kuna baishara nyingi za kufanya zinazohitaji mtaji mdogo mfano ufugaji wa kuku, nguruwe au kilimo.
  4. Andaa proposal yako au mwone mtaalamu yeyote wa biashara akusaidie na unaweza kwenda Benki au mashirika yanayojishugulisha na biashara na wanaweza kukukopa mtaji kwa muda mrefu na ukasimama.
  5. Hii ni kubwa kuliko vyote, mkumbuke muumba wako kila saa na kila muda.
 
Watakuelewa kwani wao wanawaza serikali itoe maburungutu iwape wanasahau kuwa mkono mtupu haurambwi
 
Tuambie ulifanyaje kuondoa majuto uliokuwa unapata kila unapo ona wallet empty
Nilienda kwa mama mmoja nikakuta anafuga kuku nikamwomba anipe kuku watano, jogoo mmoja na mitende minne na nikaanza kufuga kuku kea matarajio ya kuzalisha vifaranga 100 na niliweza 2020 na saivi nafuga nguruwe na kuku
 
Hata hili andiko vijana tutajifanya hatulioni,kwa sababu ya negativity zilizojaa vichwani mwetu.Tupunguze kulaumu kila kitu..mwanga utaonekana tuu.
Tuzidi kupambana na Tumuweke Mungu katika maisha yetu.
 
Nanukuu
Kuna baishara nyingi za kufanya zinazohitaji mtaji mdogo mfano ufugaji wa kuku, nguruwe au kilimo

Kaka hizi biashara za kilimo na ufugaji kweli zinahitaji mtaji mdogoo?
 
ndyo
Nanukuu
Kuna baishara nyingi za kufanya zinazohitaji mtaji mdogo mfano ufugaji wa kuku, nguruwe au kilimo

Kaka hizi biashara za kilimo na ufugaji kweli zinahitaji mtaji mdogoo?

Nanukuu
Kuna baishara nyingi za kufanya zinazohitaji mtaji mdogo mfano ufugaji wa kuku, nguruwe au kilimo

Kaka hizi biashara za kilimo na ufugaji kweli zinahitaji mtaji mdogoo?
Yah kilimo ni kikubwa ila ukianza ufugaji mdogo mdogo miezi mitatu unakua kutoka sehmu uliyokuwa hadi nyingine..usiogope kufanya kitu ww anza kukifanya utafika sehmu unayohitaji
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…