Amkeni mdai nyumba yenu. Mkija shtuka mtakuwa mmechelewa, pengine mnadhani kwa sasa mpo salama

Amkeni mdai nyumba yenu. Mkija shtuka mtakuwa mmechelewa, pengine mnadhani kwa sasa mpo salama

Komeo Lachuma

JF-Expert Member
Joined
Oct 31, 2014
Posts
7,926
Reaction score
17,030
Nikikuuzia au kukupangishia haka kakiwanja utanipa sh. ngapi? watoto watalalamika lakini mwishowe yataisha we kama unapapenda hapa sema tuongee bizinez. na wao nitawaambia hii pesa tunafanyia ukarabati wa nyumba au kulimia.nitawapa kiasi kidogo lakini mambo mengine tunamalizana"

Mama wa kambo anauza na kutaka gawa maeneo ambayo mzee ameacha. haya mambo yapo katika maisha. mitoto mipuuzi inashabikia tu kila kitu.. mama anaonekana hizi pesa anatumia kula na michepuko na watu alio date miaka ya nyuma. mitoto ikipewa pesa za kuvutia bhangi na kunywa viroba inafurahi na kusema mama yupo poa sana.

Kuna shida sehemu watu badala waamke na kudai mali zao ambazo wamehangaikia pia kupatikana wakilima na kufuga wakiuza mifugo na mazao .. na wakanunua maeneo hayo. ameolewa mama huyu baada ya mama wa kwanza kufariki na mzee kufariki mambo yamebadilika.

Nyumbani hapakaliki mama ana safiri tu ngomani kila wakati na miardi bubu ya vicoba. pesa za michango ya msiba anatumia kujineemesha yeye na ndugu zake. watu wanaofaidi ni wale ambao wana ukaribu naye ndugu na jamaa zake.

Watoto wa marehemu hawa wanapewa pesa zakavute bangi na kunywa pombe wanasherehekea mambo ya kipuuzi tu huku maeneo yao yakiuzwa na kukodishwa kwa bei cheeee.. yenye mafanikio kwa mama na ndugu zake. hii nyumba imekosa wenye mapenzi mema nayo kabia kila mtu anaishi humu kama mpitaji tu hakuna anayejali.
 
Back
Top Bottom