Amri Kiemba: Simba Imepata Tuzo ya Kujaza Watu Uwanjani Sio Mashabiki Bora

Mbona haijaandikwa Simba Fans?

Kifupi hiyo siyo tuzo ya Simba bali wapenzi wote wa soka waliohudhuria mechi ile ya Al Ahly na Simba wakiwemo mashabiki wa Yanga, Simba, Al Ahly na wapenzi wengine wote wa mpira!

Pelekeni TFF hiyo tuzo ni mali ya Taifa!
 
Mliambiwa haiwahusuuu leo mnaidai hiyo tuzo
 
Sasa wewe aliyesababisha hiyo game ichezwe hapa Tanzania ni timu gani kama sio SIMBA? Kama kuna mashabiki wengine waliokuja uwanjani siku hiyo tofauti na wale wa Simba ni viherehere vyao tu vya kutaka kuona kila tendon linalotendeka kwa jirani nyumba ya pili.
 
Huo ndio ushirikina wenyewe! Tangu lini wapenzi wa soka wakazuiwa kuangalia mechi za timu ambazo hawazishabikii?
 
Aaahaaa
 
Chura bhana, mnaacha kujadili tuzo za supu pale kibanda cha jangwani mnadandia tuzo zisizo wahusu 😂😂
 

Attachments

  • Screenshot_20231113-144418.png
    370 KB · Views: 4
Kuna tabia naiona kama inazidi kukua nchini, ya mashabiki wa soka kuona wachambuzi wa soka kama mbadala wa kufikiria kwao, yaani wao hawawezi kuwaza au kuelewa jambo bila wachambuzi.

Lakini, kuna baadhi ya vitu havihitaji wachambuzi ili kuelewa, huwa viko wazi. Mfano ni hiki alichosema Kiemba hapa, Hadi anashindwa kueleweka, anatenganisha kujaa uwanjani na kutoa sapoti.

Vipo vipengele kadhaa vya mashabiki bora, kimojawapo ni kujaa uwanjani. Ubora wa shabiki hauwezi kuonekana kwenye mchezo bila ya kuingia uwanjani. Kushangalia hadi kuvua nguo hilo ni jambo jingine.

Pia, sifa kuu ya mashabiki ni kujaa uwanjani kila timu yake inapocheza. Sasa unapokataa ubora wa mashabiki wa Simba, hata huko kwa kujaa uwanjani, inashangaza sana.

Ova
 
Sasa kwanini kapewa mwenyekiti wa bodi ya Simba na sio karia?
 
Unajua nn wengi hizi kanuni au vipengele vya mashindano hatuvijui ama kwa kutofatilia au kwa wahusika kutozitoa watu wazijue kabla
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…