Amshitaki mkewe kwa kumzalia watoto wenye sura mbaya

blackwise

Member
Joined
Aug 4, 2013
Posts
39
Reaction score
62
MWANASHERIA AMSHITAKI MKEWE KWA KUMZALIA WATOTO WENYE SURA MBAYA, NA HAKIMU AMWAGIZA MKE KULIPA FIDIA.

Gazeti la mtandaoni la KINEDA limeripoti habari yenye msisimko wa kipekee, ambapo mwanasheria mmoja aitwaye Jian Feng, amemshitaki mkewe kwa kumzaliwa watoto wenye sura mbaya. Bwana Feng anasema alimuoa mkewe kwa furaha na upendo, lakini furaha hiyo imetoweka na kuwasababishia mfarakano wa kindoa baada ya mkewe huyo kumzalia watoto wenye sura mbaya kiasi hata cha kuwaogopa.

Kwa kujitazama utanashati wake, pamoja na urembo wa mkewe, bwana Feng hakuamini kama watoto wale wangekuwa ni wa kwake, hivyo alimshutumu mkewe kwa kukosa uaminifu katika ndoa. Lakini hata hivyo, vipimo vya DNA vilithibitisha kuwa watoto wale ni wa kwake.

Kwa bahati, baadaye mke wa Feng, alikuja kukikiri wazi na kuthibitisha kwamba, huko nyuma kabla hawajafunga ndoa, alipata kutumia kiasi cha dola 100,000 kufanyiwa upasuaji nchini Korea Kusini wa kujibadili mwonekano wake (Cosmetic surgery).

Kufuatia kukiri huko, Feng alimshitaki mkewe kwa kosa la kugushi mwonekano, na kutosema kweli juu ya upasuaji aliofanya kiasi cha kupelekea aonekane mrembo kinyume na uhalisia. Jaji alikubaliana na malalamiko ya Feng, na kumtakama mke alipe fidia ya dola 120,000.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hata kama ni ya zamani lakini kuna funzo ndani yake (KUGHUSHI)

Cairo's
 
AMSHITAKI MKEWE KWA KUMZALIA WATOTO WENYE SURA MBAYA, NA HAKIMU AMWAGIZA MKE KULIPA FIDIA.

Gazeti la mtandaoni la KINEDA limeripoti habari yenye msisimko wa kipekee, ambapo mwanaume mmoja aitwaye Jian Feng, amemshitaki mkewe kwa kumzaliwa watoto wenye sura mbaya. Bwana Feng anasema alimuoa mkewe kwa furaha na upendo, lakini furaha hiyo imetoweka na kuwasababishia mfarakano wa kindoa baada ya mkewe huyo kumzalia watoto wenye sura mbaya kiasi hata cha kuwaogopa.

Kwa kujitazama utanashati wake, pamoja na urembo wa mkewe, bwana Feng hakuamini kama watoto wale wangekuwa ni wa kwake, hivyo alimshutumu mkewe kwa kukosa uaminifu katika ndoa. Lakini hata hivyo, vipimo vya DNA vilithibitisha kuwa watoto wale ni wa kwake.

Kwa bahati, baadaye mke wa Feng, alikuja kukikiri wazi na kuthibitisha kwamba, huko nyuma kabla hawajafunga ndoa, alipata kutumia kiasi cha dola 100,000 kufanyiwa upasuaji nchini Korea Kusini wa kujibadili mwonekano wake (Cosmetic surgery).

Kufuatia kukiri huko, Feng alimshitaki mkewe kwa kosa la kugushi mwonekano, na kutosema kweli juu ya upasuaji aliofanya kiasi cha kupelekea aonekane mrembo kinyume na uhalisia. Jaji alikubaliana na malalamiko ya Feng, na kumtakama mke alipe fidia ya dola 120,000.
 
Huko ndipo kuna Uhuru wa Mahakama na siyo hapa kwetu,kila kukicha kukimbizana na Wapinzani kama ndiyo maendeleo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Tatizo ni aliye mfahamisha kuwa kuna sura mbaya na nzuri akasahau kuuliza ikiwa yake ni mbaya au nzuri

2 Timotheo:4.2
lihubiri neno, uwe tayari, wakati ukufaao na wakati usiokufaa, karipia, kemea, na kuonya kwa uvumilivu wote na mafundisho.
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
ila huyo dogo mkubwa wao kapungua kidogo

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…