Amunike ni dhaifu kusoma mchezo na kubadilika

Amunike ni dhaifu kusoma mchezo na kubadilika

Hata angecheza nani jana tatizo la Tz sio nani anacheza ila stamina na fitness level yetu sio nzuri kila dakika ndio ilikuwa kama tumeisha na Kenya wanaanza ni wazi kabisa level ya fitness haikuwa sawa. Unaweza kuwa na wachezaji wa kawaida ila wakiwa fit na kufanya majukumu yao inatosha tumeona leo Algeria wachezaji wao sio kama Senegal ila wako fit kila mpira wapo na nidhamu. Fey alicheza mechi ya kwanza na alishindwa vibaya tuseme Senegal level nyingine lakini kama wewe mzuri huwezi kutolewa dakika ya 43 na angecheza leo halafu angeshindwa ndio angepoteza imani na ndoto zake.
 
Wakuu,

Kocha wetu ni dhaifu mno kusoma mchezo na kubadili mbinu. Timu inacheza vile vile hata wapinzani wanapobadili mbinu. Mbaya zaidi kilema kikuu ni kocha kutojua namna ya kutumia viungo wetu. Hivi unamtumia kiungo kama Himid asaidie nini? Yule ni mkabaji tu na hawezi kuchezesha timu.

Badala ya kuingiza mtu wa kutuliza timu au kuongeza kasi ya mashambulizi unaingiza mkabaji tu na kufanya timu ielemewe. Nyoni aliomba sub mapema lakini haikufanyika hadi akalala chini na bado hawakufikiri haraka namna ya kujaza lile gap muhimu.

Amunike anafaa kuwa mkufunzi wa TFF kuendeleza program za soka lakini si mwalimu mzuri kabisa. Hakuna mechi aliyofanya sub za maana na akifanya ni too late damage inakuwa imeshakuwa kubwa na habadiliki haraka kwa kuwasoma wapinzani.

Wachezaji wanapambana wenyewe bila mbinu za ziada. Kwa timu hii hii angepatikana kocha anayewajua vizuri wachezaji wetu na anayeweza kubadilika kutokana na mchezo miujiza ingetokea.

Zambia walichukua hili kombe wakiwa hawana mastaa wa kutisha kulinganisha na wapinzani wao wengi. Technical bench ni msingi muhimu sana kabla hata ya timu yenyewe.

Wachezaji wetu wamepambana kwa uwezo wao wote lakini benchi la ufundi limewaangusha sana. Wasisingizie uzoefu mdogo, akina Okwi wana uzoefu gani? Jana tulihitaji uzoefu gani? Tatizo ni mbinu za kimichezo hatuna.
Wacha kumzingizia Amunike nuksi ni kwa ccm kutaka kutekeleza ilani ya chama kupitia bashite hadi kwenye mpira timu ya taifa.
 
Kocha wa Kenya alisoma game mapema na akafanya sub dakika ya 32 huku watu wakishangaa how come anafanya sub "mapema" hivyo. Baada ya hapo game ilichange kabisa. Kocha wetu yeye alikuwa amekunja mikono tu. Sijui ndio yalikuwa maagizo ya Prince DAB?
under total control of bashite
 
Fei Toto ambaye mechi ya Kwanza alichemsha ndani ya dakika 10 tu

Mpira sio ujanjaujanja ni mipango na TZ hatuna mipango
Huyu hata challenge cup hawezi kuchukua. Simba wamemuacha Kotei sababu za kucheza kama Himid. Kiungo mkabaji ambaye hawezi kuchezesha timu inafanya timu ilemewe tu. Bora angeingia Fei Toto angeongeza pressure kwenye kiungo.
 
Licha ya Amunike kuwa c mzuri kwa kiwango cha soka cha kisasa, hata wachezaji wetu viwango vyao ni vya chini. Tunacheza bado mpira wa 1980s wa kufuata ulipo mpira badala ya kukaba na kufuata wapinzani. Kocha angesisitiza wachezaji wa "press" ..wasiwaachiwe wapinzani muda wa kutoa pasi...

Binafsi naona tatizo pia ni kuwa viongozi wetu c wapenzi sana wa soka na michezo kiujumla. Wanatokea tu wakati tuhafanya vizuri...
 
Amunike alichemsha kwenye selection ya timu! Akachemsha tena kwenye upangaji wa timu! Akachemsha kwenye game approach!techniques and substitution! Nani alimleta huyu plumber??
 
Back
Top Bottom