Ana milioni 2 na ameomba ushauri wa biashara, wajuzi tumsaidie

Ana milioni 2 na ameomba ushauri wa biashara, wajuzi tumsaidie

Wakuu hivi kwa location ya Songea kwa mtaji huo anaweza akafanya bize gani? Mi niliwaza afungue salon lakini yeye hajui kunyoa. Ndo ilipo changamoto hapo.
Binafsi kwa uzoefu wangu nashauru hivii..
1. Mwenye majibu ya kujua ni biashara ipi afanye ni yeye mwenyewe.
2. Biashara inaenda na interest ya mtu anachopenda kufanya, kwasababu akifanya ambacho hakipendi hatafika mbali na biashara, itakua ni michosho na kulazimishana tu..
3. Kama amesoma shule.. na amefika level flan... atumie ujuz na uzoefu wake kufanya Biashara inaendana na taaluma yake.
Nawasilisha
 
Kwa songea si mwenyeji sana ila ingekuwa mimi huku nilipo ningefungua moja wapo kati ya haya.

1.Duka la maji la jumla(sio zile godown)
na kuuzia wafanyabiashara na wachuuzi wa hapo town.

2.Boxer/TVS pikipiki used kwa 1.5 million na kuanza kupiga mzigo na kuweka 300,000 Kwa mwezi.(Pia ukichoka unauza chombo mana ni asset)

3.Naweka Tigopesa na Mpesa Tu.huku nikiacha mitandao mingine pembeni kwanza ili nikuze mtaji,chenji unaweka kibanda hapo.( ila unaangalia na hapo ulipo mtandao gani unatumika sana)

4.Kupakia dumu za alizeti Singida au dodoma na kuleta na kufungua fremu hapo ulipo na kuuza huku ukisupply kwa masoko ya hukohuko.

5.Gold Fisher ll. ningenunua hichi kifaa cha kupimia dhahabu(tena songea kuna machimbo).
Kwa siku ukiitwa ni laki 1 tena umekaa unafuatwa.
-Tengeneza connections na wachimbaji kila wiki hukosi 400,000 narudia kwa wiki.

6.Biashara ya Mini Kiosk
Watu wanaidharau ila ina hela.Unauza vitoko na viroba na sigara (smart gin, na takataka zingine)
Kuna jamaa namfahamu anauza kwa siku 30,000 faida ni pasu pasu peleka stendi au machimboni au sokoni.

Asante
Kuna wazo nmelipenda hapo ntalifanyia kazi
 
Hivi inakuaje kuaje mpka mtu unamiliki 2milion wakuu ..? Mbona mm sijawahi kushika hata za kuazimwa tu
Hahahaaa,usijali Hela hutembee zitakufikia tu Mungu ni wetu sotee. Swali lakooo la kibingwa sana hata mi nawazagaa.Anyway kwa namna Fulani inawezekana mfano:
1. Kapata mgao wa Urithii(Hana anachojua kwenye utafutaji).
2.Kahongwa na lishangazi/ sponsor ( anataka aanze maisha).
3.Uvivu wa kufikiri mpaka upate ramani ya wazo la kufanya (Hatari yake chap mtani unakwisha....AU kupata kujua vingi zaidi(vya kiambiwa unachanganya na vyako) mambo yanakwenda.
 
Kwa songea si mwenyeji sana ila ingekuwa mimi huku nilipo ningefungua moja wapo kati ya haya.

1.Duka la maji la jumla(sio zile godown)
na kuuzia wafanyabiashara na wachuuzi wa hapo town.

2.Boxer/TVS pikipiki used kwa 1.5 million na kuanza kupiga mzigo na kuweka 300,000 Kwa mwezi.(Pia ukichoka unauza chombo mana ni asset)

3.Naweka Tigopesa na Mpesa Tu.huku nikiacha mitandao mingine pembeni kwanza ili nikuze mtaji,chenji unaweka kibanda hapo.( ila unaangalia na hapo ulipo mtandao gani unatumika sana)

4.Kupakia dumu za alizeti Singida au dodoma na kuleta na kufungua fremu hapo ulipo na kuuza huku ukisupply kwa masoko ya hukohuko.

5.Gold Fisher ll. ningenunua hichi kifaa cha kupimia dhahabu(tena songea kuna machimbo).
Kwa siku ukiitwa ni laki 1 tena umekaa unafuatwa.
-Tengeneza connections na wachimbaji kila wiki hukosi 400,000 narudia kwa wiki.

6.Biashara ya Mini Kiosk
Watu wanaidharau ila ina hela.Unauza vitoko na viroba na sigara (smart gin, na takataka zingine)
Kuna jamaa namfahamu anauza kwa siku 30,000 faida ni pasu pasu peleka stendi au machimboni au sokoni.

Asante
Mkuu hiyo namba 6 iko VYEMA labda mtaji mdogo
 
Mkuu hiyo namba 6 iko VYEMA labda mtaji mdogo

yah huyu nayemfahamu alianza na 200,000
kwasiku anauza mpka 30,000 minimum.

Faida 10,000 kwa mwezi jumla 300,000 na anapiga kazi siku zote bila kupumzika.

Ina maana kama ana million 2 akachukua kifremu na akaamua kuweka vinywaji na bia na vitoko kadhaaa pesa inazunguka.(Friji likitoka home litapunguza gharama)
 
Wakuu hivi kwa location ya Songea kwa mtaji huo anaweza akafanya bize gani? Mi niliwaza afungue salon lakini yeye hajui kunyoa. Ndo ilipo changamoto hapo.
Songea sehemu ganj mzee, za kuyumuka, mwambie afungue mpesa ,,songea saloon nyng na hazilipi kwa sasa, naongea kwa ushahidi,
 
Hahahaaa,usijali Hela hutembee zitakufikia tu Mungu ni wetu sotee. Swali lakooo la kibingwa sana hata mi nawazagaa.Anyway kwa namna Fulani inawezekana mfano:
1. Kapata mgao wa Urithii(Hana anachojua kwenye utafutaji).
2.Kahongwa na lishangazi/ sponsor ( anataka aanze maisha).
3.Uvivu wa kufikiri mpaka upate ramani ya wazo la kufanya (Hatari yake chap mtani unakwisha....AU kupata kujua vingi zaidi(vya kiambiwa unachanganya na vyako) mambo yanakwenda.
🙏🙏 nmekuelewa mkuu
 
Back
Top Bottom