Ana Mke lakini nina Mtoto wake, Naomba ufafanuzi juu ya jambo hili kisheria

Ana Mke lakini nina Mtoto wake, Naomba ufafanuzi juu ya jambo hili kisheria

Ulichemka sana kumzalia mtoto bila mapatano.kwa sasa usimtibue kabisa maana hutaamini kitakachofuata.cha msingi ukitaka uendelee na jamaa ni kuhakikisha unamlindia ndoa yake kwa kila hali.

Mtu anayechepuka usidhani haipendi ndoa yake.Yoyote anayechepuka akigundua mahusiano yenu yanaelekea kuharibu ndoa yake. Anachofanya ni kukuacha na kutafuta mchepuko mwingine.

Huu pia ni ushauri mwingine kwa wanaotaka kudumu na waume za watu.hakikisha hujimilikishi ukajisahau hadi ukaanza kumletea usumbufu na ndoa yake.wewe endelea kuwa mwizi tuuu. Mchepuko unataka siri siku zote. Siyo mambo ya kutambulishwa tambulishwa.

Mwisho ni kwamba huna haki yoyote.tena ukimpandisha mashetwani anaweza hata akamkataa huyo mtoto pia ijapo wewe mwenyewe unadha kwa kuwa mkewe hajamzalia basi ndiyo kigezo.by the way unaweza kuta mko wengi
 
Ninyi hua ni wanawake wapumbavu sana. nasema WAPUMBAVU kwa macho makavu maana hiki kilinitokea,baada ya kumpa ujauzito mwanamke ambaye alikua anajua kabisa mimi ni mume wa mtu na sikumlaghai, nilimuweka wazi kua nina mke na tukazungumza kua asije kuzaa mtoto tukakubaliana maana kwanza kabisa alinipenda yeye mwenyewe tukiwa kazini huko mkoani.

Lakini tukaenda enda na siyo kwamba tulikua tunakutana mala kwa mala,kaibuka tu siku moja na kusema ana mimba yangu,nilipo hamaki na kuanza kumhoji vzr ndipo ugomvi ulipoanza na kuanza kutukana matusi familia yangu na mimi mwenyewe.

Haikuishia hapo nilipiga moyo konde nikahudumia ile mimba lakini niliendelea kutukanwa na akitukana familia yangu sana. Kiasi mpaka nikaja kuchoka hata kutumia senti yangu kwa ajili yake maana mtu ananitukana nampaje pesa?

Mpaka mtoto anazaliwa na kukua sasa hv ana miaka mitano,mwanamke yule ni mgomvi tu. Hua najaribu kufikiri kua yamkini ni mwehu au vipi..stor hii naifupisha tu lakini ukweli wanawake kadhaa mna ujinga na upumbavu mkubwa sana. Kwanza wewe uliye ropoka hapa ungekua karibu yangu hata ningekuchapa kofi kabisa japo siyo tabia yangu.

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Anajikosea heshima mwenyewe wala sio mke wa jamaa. Nduguze watamuona Hana adabu na kashindwa kupata mwanaume wake amuoe.
Hao wanajamii na ndugu kumfahamu haihalalishi kua huyo ni mumeo. Kwanza unapata wapi guts za kuishi na mume wa mwenzako hadi unamtambulisha kwa ndugu, mbona unamkosea heshima mwanamke mwenzako mwenye mume wake.

Wewe utabaki kua mchepuko/ baby mama.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hapo kama huna ndoa utaachiwa manyoya labda uende ustawi wa jamii.

Sent using Jamii Forums mobile app


Wanawake huwa mnashauriana vibaya. Cha muhimu ulipaswa kumwambia azidishe mapenzi kwa baba mtoto wake ili mzee amkubali na ikibidi a pay attention zaidi kwake. Suala la kuzaa na mume wa mtu ni kosa ila kosa kubwa zaidi ni kuwa na mahusiano naye. Sasa hilo limeshatokea, finding solution sio kwenda ustawi wa jamii kwa vile hajasema amenyimwa matumizi.

Huyo mtoto atakosa matunzo na mapenzi ya baba endapo huyo mwanamke ataanza mambo ya ustawi wa jamii au dawati la jinsia.

Uvumilivu hulipa.
 
Nmependa majbu ya wanaume...hao wanaoendelea kujilengesha muwe mnawafundisha Adab hivyo hivyo maana wanawake wengi akili sijui zimeenda wap utakuta mtoa mada alishajaribu kumroga na uyo kaka...lakini nipende kukazia tu kua wewe dada ujielewi muombe Mungu akupe mume wako acha kumtesa mwanamke mwenzio maana machozi ya huyo mama hayatakuacha salama

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ninyi hua ni wanawake wapumbavu sana. nasema WAPUMBAVU kwa macho makavu maana hiki kilinitokea,baada ya kumpa ujauzito mwanamke ambaye alikua anajua kabisa mimi ni mume wa mtu na sikumlaghai, nilimuweka wazi kua nina mke na tukazungumza kua asije kuzaa mtoto tukakubaliana maana kwanza kabisa alinipenda yeye mwenyewe tukiwa kazini huko mkoani...

Kwa maoni yangu, mpumbavu ni wewe kwa kuwa hukutaka kutumia kinga. Hapo alipata mimba tu lakini hujiulizi ingekuwaje angekuambukiza ukimwi?

Endapo una mke, ridhika naye na ukishindwa, please condomize. Samahani kwa kutumia lugha kali ingawa kwenye sentence yako ya kwanza umetumia lugha hiyo kwa huyo mwanamke.
 
Hahaha wewe Mzee upo?
Heshima yako Baba. Kule kwetu mwanaume anaamkiwa shkamoo kubwa kabisa (tuko kimkakati zaidi).
Nimefurahi kukuona hapa.


Missing you.
Kulikuwa na wimbi kubwa sana la watoto waliingia humu JF nilikuwa nawasubiri wakue, naona wengi wameshakuwa wakubwa kiakili sasa.

Thread ilikuwa inaharibiwa within a minute!
 
Ulichemka sana kumzalia mtoto bila mapatano.kwa sasa usimtibue kabisa maana hutaamini kitakachofuata.cha msingi ukitaka uendelee na jamaa ni kuhakikisha unamlindia ndoa yake kwa kila hali.

Mtu anayechepuka usidhani haipendi ndoa yake.Yoyote anayechepuka akigundua mahusiano yenu yanaelekea kuharibu ndoa yake. Anachofanya ni kukuacha na kutafuta mchepuko mwingine...
Kwahiyo wewe ukitaka kuzaa na mtu lazima uweke makubaliano...[emoji3][emoji3]
Makubaliano kama yapi?

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwa maoni yangu, mpumbavu ni wewe kwa kuwa hukutaka kutumia kinga.
Hapo alipata mimba tu lakini hujiulizi ingekuwaje angekuambukiza ukimwi?
Endapo una mke, ridhika naye na ukishindwa, please condomize.

Samahani kwa kutumia lugha kali ingawa kwenye sentence yako ya kwanza umetumia lugha hiyo kwa huyo mwanamke.
Wewe ni MPUMBAVU..amini hivyo na si mimi

JAH Rastafari Morning Africa.Trust JAH respect nature
 
Mleta mada anakula za uso tu, sio kwa wanaume wala kwa wanawake. Mtasababisha aigope simu yake. Anyway, mleta mada aliingia kwenye hayo mahusiano akiwa na calculations zake kichwani. Sasa anaanza kushtuka wakati tayari yuko in the tragedy of her miscalculations. TOO LATE!
 
Kwa jinsi unavyosema eti mwaka jana ukafanikiwa kupata ujauzito maana yake ni kitu ulikuwa unakitafuta kwa jamaa, umejilengesha. Hii ni mbaya sana, wewe unajijua ni mchepuko na jamaa ana mke we unajibebesha limimba. Na hakika ndani ya akili yako ukawaza kwa kuwa mkewe hajazaa basi tayari kwa wewe kuzaa na jamaa umejihalalisha na bila haya unauliza eti haki zako...
Kambaku umemaliza. Hii tabia ya mleta mada kujilengesha ili apate mimba alafu eti adai kutunzwa na mwanae ikome kabisa.

Kwa taratibu za dini ya kiislamu huyu mwanamke amemsababishia maisha magumu kwani licha ya kua hana haki yoyote kwa anaedaiwa kua baba, pia hawezi kuswalisha wenzie, hawezi kutoa ushahidi popote pale na ukaaminika.

Mwana haramu ni mtoto wa mama yake na stahiki zake zote ni lazima azipate kwa mama yake.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wanawake huwa mnashauriana vibaya.
Cha muhimu ulipaswa kumwambia azidishe mapenzi kwa baba mtoto wake ili mzee amkubali na ikibidi a pay attention zaidi kwake. Suala la kuzaa na mume wa mtu ni kosa ila kosa kubwa zaidi ni kuwa na mahusiano naye. Sasa hilo limeshatokea, finding solution sio kwenda ustawi wa jamii kwa vile hajasema amenyimwa matumizi.

Huyo mtoto atakosa matunzo na mapenzi ya baba endapo huyo mwanamke ataanza mambo ya ustawi wa jamii au dawati la jinsia.

Uvumilivu hulipa.
Hyo comment yangu haikuwa hvo moderator aliedit comments nyingi kwenye Uzi huu na nyingine kufuta ambazo zingemsaidia huyu dada, so my comment were edited na nyingine kufutwa maana Mimi sikumshauri hata kwenda ustwai nilimwambia a relax akifikiria mke wa ndoa kujua ndo atapendwa

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom