Nitajitahidi kuandika ufupi kwa kwenda moja kwa moja kwenye suala ambalo kwangu linanichanganya. Nina rafiki wa kike ambaye tumefahamiana kwa takribani miaka miwili na tumekubaliana tuwe wachumba na nimeshamtambulisha kwa baadhi ya ndugu zangu akiwemo mama yangu.
Tatizo ni kwamba ni bahati kupita mwezi hajaumwa. Sasa naomba kupata uzoefu kwa yeyote ambaye ameshakumbana na hali kama hii.
Lengo langu ni kutaka kujua endapo hali kama hii itabadilika au ndo mtu anakuwa hivyo maisha yote(mgonjwa mgonjwa). Binti ndo mwenye hili tatizo(kuugua ugua mara kwa mara)