Anachokisema Hans Pope kina ukweli au ndo janja janja?

Opera Min

JF-Expert Member
Joined
Nov 28, 2013
Posts
890
Reaction score
658
Nimemskiliza kwa makini sana,eti anasema Asante Kwasi sio mchezaji anayemilikiwa na Lipuli,ni mchezaji yupo chini academybya ghana kupitia kwa Agenti wake, so Lipuli wakizingua wanamchukua juu kwa juu...hii kitu mbona kama haiingii akilini?
Simba waache ujanja wa kizamani...
 
Hans Pope hazimtoshi hata kidogo. Kwani wamiliki hawajui yupo Lipuli? Lazima wana makubaliano nayo na lazima yaheshimiwe. Hii inaitwa third party ownership. Ina usumbufu wake EPL wamepiga marufuku wachezaji wenye third party ownership. Iliwahi kutokea kwa Carlos Tevex akiwa West Ham United kabla ya kwenda Man U
 
Kuna haja Simba kuwatoa hawa wanao ji ita kamati ya usajiri... Simba ina hela iwape watu wanao jua kufanya usajiri na kufanya utafiti wa wachezaji
 
Ila kuna sehem anajichanganya mwenyewe kwa kukubali kuwa kwasi anamilikiwa na academy, agent na lipuli!
 


Huyu makofia anajipigia tu pesa za usajili hapo mikiani.

Halafu hizi figisufigisu za kizamani ndio zinazosababisha soka letu bara halikui.
 
Ni vizuri wameamua kufata utaratibu japo wamechelewa. Wangeandika barua na kukaa na lipuli mapema hili suala lingekuwa limeshaisha siku nyingi sana. Tatizo la hizi timu kubwa hazitaki kufuata utaratibu zinataka zitumie ubabe. Ningekuwa kiongozi wa lipuli huu ndio wakati wa kuwapiga hao simba pesa ndefu ya kutosha kusajili wachezaji wawili wenye uwezo wa kwasi ili mwakani waje tena kusajili kwa sababu wamejitoa ufahamu hawataki kufanya scouting ya wachezaji wanasubiri waletewe.
 
Hans Pope ni haini,anafikiri kila kitu ni kupindua tuu
 
Kuna haja Simba kuwatoa hawa wanao ji ita kamati ya usajiri... Simba ina hela iwape watu wanao jua kufanya usajiri na kufanya utafiti wa wachezaji
Tuwatoe tumweke nani?Nyika wa yanga anaesajili akina Mkomola na kufunga usajili
 
Tuwatoe tumweke nani?Nyika wa yanga anaesajili akina Mkomola na kufunga usajili
‘Akina’ kwa Kiswahili inamaanisha ni mjumuiko wa zaidi ya mtu mmoja, hata kama ni wawili. Kwa tafsiri ya neno hilohilo, Simba wamesaini ‘akina’ nani?
 
Wamchukue juu juu kisha akacheze ligi za mbuzi ila sio VPL
watu kama hanspope ndo wanaoshusha hadhi mpira wa Tanzania na kuonekana kanuni na sheria zilizopo si chochote
 
Siyo vizuri, kwa sababu taratibu tayari zilikwishakiukwa. Makibaliano yoyote ya Simba na Lipuli kwa sasa nayatafuta kasoro kwamba Simba walimrubuni, kumficha, kuzungumza naye na hatimaye kumsainisha Kwasi akiwa tayari na mkataba na Lipuli. Hatua dhidi ya kosa hilo ni lazima zichukuliwe, hasa kwa sababu Lipuli yenyewe ilikwishalilalamikia rasmi jambo hilo TFF. Lakini hata isingelalamika, bado kosa limefanyika na linahusu Ligi nzima siyo Lipuli peke yake. TFF, Simba na Lipuli wanachotaka kukifanya sasa ni upuuzi sawa na wa kuchinja kuku aliyekwishafariki ili nyama yake iwe halali kwa waumini wahusika!
 
Huyu Pope na kamati yake sijawahi kuwaelewa. Wao akihitajika beki wanasajili mshambuliaji akihitajika mshambuliaji wanasajili kiungo. Una mabeki zaidi ya wanne wa kati pamoja viraka wawili wanaoweza cheza beki ya kati halafu unaenda sajili tena beki badala ya kutafuta washambuliaji wawili wenye akili, mashuti, chenga, wenye uwezo binafsi wa kupasua msitu wa mabeki imara, wanaojua kucheka na nyavu, washambuliaji ambao mechi ikiisha mabeki wanaenda kulala na viatu, washambuliaji wanaoweza badilisha matokeo hata dakika ya 90.

Haya sasa simba tumevuna tulichopanda - tulipanda kwasi tumevuna kutolewa kwenye mashindano raundi ya kwanza.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…