Anajuuta kuchukua mume wa mtu

Hata angekua sio mune wa mtu bado angeambukizwa virusi vile vile.

Aende akapime sasa apate uhakika ili kama anao aanze kuishi kwa kuzingatia masharti.

Hivi ni kwanini watu wote mna assume kuwa huyo baba ndio atakuwa amemuambukiza huyu mama, mimi naona wote wameambukizana.. huyu dada anaweza kabisa kuwa ndio kamuambukiza huyu baba kwani yeye alikuwa hajaolewa... lakini all in all uzinzi haulipi... tuache.....
 
Mpe pole tu,
Cha kufanya akapime tu kwan anaweza akawa hajaambukizwa,
Na km akiwa positive atapata ushauri na maisha yataendeleatu,
Jaman ngono zembe ni hatari km hatuwezi kupima basi tutumien condom.
 
Muambie akapime ngoma aliendeleze libeneke, ila ahame mtaa manake kama mie ndo yule dada aliemtukana coz yeye alijiona mshindi kuiba mumu, ningekutana nae ningemcheka sana. Unajiona mjanjaaa kumbe umebeba gunia la kinyesi, lol!
Mjini kugumu sana,kha!
 
kwanza mpe pole kwa misukosuko yote ya kimaisha .. kawaida wanadamu tumeumbwa na upofu huwa hatuangalii tuendako wala tulikotoka kwani tunaamini kila kinachokuja kina umuhimu hata kama si kwa wakati huo...

mwambie asijute ila apokee hali kama ilivyo na aende kituo cha ushauri ili ajipage na aina ya maisha
 
hv unatembeaje na mtu hujui hiv status yake tena kwa ngono zembe enzi hz?
mimi ukinitaka angaza kwanza
ndo maana sina mpenzi maana tukipanga kwenda angaza huwa siwaoni tena

i like you...
 
DUh! pole sana binti. Mimi sina cha kusema. yote namwachia Mungu aamue
 
Mh!..kwanza Mume wa mtu,second bila kinga,.ila maybe hajaskia the researchz that married people are more prone to hiv..akapime tu ajue status and live with it.
 
Reactions: BPM
Angekuwa karibu yangu ningempa ushauri. Mume wa mtu wa nini lakn?? Kha!
 
Dah sina hata haja ya kumlaumu sana kwani tatizo ndo limeshatokea sasa tunasonga mbele na maisha ,mpeleke akafanyiwe cancelling juu ya hali hiyo,apimwe na ajue status yake mpaka sasa kama ni positive aanze kuishi kwa matumaini ,na kama atakuwa negative ajipange upya kimaisha
 
life goes on...akapime ajue ajipangaje in life.akumbuke ana mtoto mdogo so priority yake iwe mtoto.......ukimwi nooooooma
 
huwaga nawachukia sana tena sana wazinifu hvy ushauri wangu utamuweka pabaya bora nisimshauri
Hakuna binadamu asiye na kasoro hapa duniani, kama wewe sio mzinifu lkn una kasoro nyingine ambayo waifahamu wewe na Mungu wako. Usimnyooshee kidole huyo mzinifu aliyeombewa ushauri, je wewe ni mkamilifu kwa kila kitu hapa duniani??? :juggle:
 
hv unatembeaje na mtu hujui hiv status yake tena kwa ngono zembe enzi hz?
mimi ukinitaka angaza kwanza
ndo maana sina mpenzi maana tukipanga kwenda angaza huwa siwaoni tena

mi ntakufaa Smile..
Labda kigezo kingine..
 
Hakuna binadamu asiye na kasoro hapa duniani, kama wewe sio mzinifu lkn una kasoro nyingine ambayo waifahamu wewe na Mungu wako. Usimnyooshee kidole huyo mzinifu aliyeombewa ushauri, je wewe ni mkamilifu kwa kila kitu hapa duniani??? :juggle:

dada yetu akapime.. Huenda hata hajaambukizwa ugonjwa wenyewe..
 
haha utamu wa muhogo ....sasa ngoma aicheze tuu
 
Kila mtu katika nyakati fulani za maisha alishawahi kufanya kosa kubwa ambalo halisahau.Kwa rafiki yako akubali kosa na kwamba si peke yake aliefanya makosa kama yake, halafu asimlaumu yeyote na akubali kuchukua vipimo.Jibu lolote atakalopata ndio ndio hasa matokeo ya kukiri kosa na kwa kuwa tayari amekubali kosa atabaki kuwa na amani.

Asali,ajipange upya na itakuwa usiku itakuwa mchana maisha yanaendelea.
 
Hakuna binadamu asiye na kasoro hapa duniani, kama wewe sio mzinifu lkn una kasoro nyingine ambayo waifahamu wewe na Mungu wako. Usimnyooshee kidole huyo mzinifu aliyeombewa ushauri, je wewe ni mkamilifu kwa kila kitu hapa duniani??? :juggle:
uko huru kupenda unachokipenda namimi niko huru kuchukia ninachokichukia, nachukia uzinzi full stop
 
majuto ni mjukuu, yy si aliona raha kumkimba kijana ambaye alizaa naye na kupora mume wa mtu, haya ndiyo malipo yake
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…