Anakaribia kurithi 300M, hajui biashara ya kufanya, je, ushauri niliompa ni sawa?

Anakaribia kurithi 300M, hajui biashara ya kufanya, je, ushauri niliompa ni sawa?

sky soldier

JF-Expert Member
Joined
Mar 30, 2020
Posts
5,407
Reaction score
19,264
Habarini wadau, Nina rafiki yangu ambae bahati ipo upande wake maana kiukweli linapokuja kwenye swala la uchumi wapo vizuri sana.

Familia yao kiufupi wapo vizuri, kaka na dada zake wanajitegemea na wapo vizuri kiuchumi ila sasa huyu rafiki yangu kwa bahati mbaya shule ilimshinda na biashara kwake ni ngumu, kiufupi ni mtu wa nyumbani ila wazazi wake wanajali, ana gari na pesa anapewa, hana fujo na ni muungwana tu.

Mwezi wa pili walipata msiba mama yao alifariki, sasa amebaki mzee peke yake nae kiufupi maisha yamekuwa magumu baada ya kuondokewa na mkewe, Mzee wao ni mtu msomi akaamua tu aanze kuweka mambo sawa mapema, kuanzia mwezi wa sita alianza kuwapa ramani watoto wake wa kila mali aliyonayo, pamoja na kushughulikia mambo ya mirathi, kuna baadhi ya mali ifikapo mwezi
zitaenda kwa watoto wake hata kama bado yupi hai, na hizi ndizo nazozizungumzia hapa.

Sasa huyu rafiki atachopata ni takribani milioni 320, hizi ni anazipata miezi michache ijayo, mzee wake ndio kaamua kumpa kiasi hicho kama urithi wake wa mwisho kwake, akifeli ni game over.

Kabla sijampa ushauri nilimwambia yeyea anafikiria kuwekeza wapi akaniambia kafikiria mawazo kama kufungua bar kubwa, kujenga sehemu ya kuogelea, kununua bajaji nyingi, nk ni mawazo mazuri lakini nikamwambia yanahitaji mtu awe ana uzoefu kidogo wa biashara.

Sasa binafsi nimemshauri kwavile hajui biashara na hana elimu ni vema akanunue treasury bonds,

Ila na mimi nimempa taarifa juu juu tu, naombeni taarifa za ziada kuhusu hatua za kununua bondi hapa nchini, katika hio milioni 320 je aweke kiasi gani , mambo gani ya kuzingatia, kutambua matapeli, n.k

Na pia kama kuna wazo mbadala itakua vizuri ukiliweka ila sio linalohitaji sana skills za biashara ambazo rafiki yangu huyu kwake ni changamoto
 
Habarini wadau, Nina rafiki yangu ambae bahati ipo upande wake maana kiukweli linapokuja kwenye swala la uchumi wapo vizuri sana.
Kuna biashara nyingi zisizohitaji pressure na uwekezaji mkubwa ... Akiwekeza 50M tu ndani ya mwaka ana 50 nyingine.. Ni biashara ya kukusanya malighafi fulani na soko lake ni hakika
 
Kuna biashara nyingi zisizohitaji pressure na uwekezaji mkubwa ... Akiwekeza 50M tu ndani ya mwaka ana 50 nyingine.. Ni biashara ya kukusanya malighafi fulani na soko lake ni hakika
Ndio tujuzane mkuu, kumbuka huyu rafiki hajui sana mambo ya biashara, yeye labda nlichoona kitamfaa ni kuweka hela na kusubiri mapato ya uhakika ndio nikamshauri hizo bondi maana hazina mambo mengi, nlitaka kumshauri kufungua gym ila bado nikaona huki anaweza kufeli

Ika mkuu tueleezane hio biashara
 
Kuna biashara nyingi zisizohitaji pressure na uwekezaji mkubwa ... Akiwekeza 50M tu ndani ya mwaka ana 50 nyingine.. Ni biashara ya kukusanya malighafi fulani na soko lake ni hakika
Taja basi mkuu inaweza kuwa ni fursa kwa wengine pia.
 
Anunue dogecoins za 300m ndani ya mwaka anaweza akawa bilionea 🐕🤸🤣
images - 2021-07-27T183226.228.jpeg
 
Anunue dogecoins za 300m ndani ya mwaka anaweza akawa bilionea 🐕🤸🤣
Sheria muhimu ya uwekezaji ni kujua unachowekeza, haya mambo ya bitcoins na ma doge naonaga yana risk kubwa, elon musk akisema tu kitu flani mara ishuke mara ipande, full presha yan.

Asante kwa mawazo 😂😂
 
Sheria muhimu ya uwekezaji ni kujua unachowekeza, haya mambo ya bitcoins na ma doge naonaga yana risk kubwa, elon musk akisema tu kitu flani mara ishuke mara ipande, full presha yan
Akijua pa kuingia na kutokea ametajirika wanasema the higher the risk the higher the reward, ila treasury bonds ni much safer and an assured investment kwa mtu aliyepata hela kwa mkupuo kama hivyo
 
Akijua pa kuingia na kutokea ametajirika wanasema the higher the risk the higher the reward, ila treasury bonds ni much safer and an assured investment kwa mtu aliyepata hela kwa mkupuo kama hivyo
Kwa tz Hatua zipoje kupata hizo bondi?

Aweke kiasi gani?

Atapata kiasi gani?

hicho kiasi kinalipwa kila baada ya muda gani?

Achukue bondi za miezi au miaka mingapi?
 
Anunue viwanja ddoma ajenge apartment huku ata huku dar anawweza akawa anpiga peza tu bila pressure kubwa ....ila naona Kaka zake wale wasomi watamshauri nn Cha kufanya coni sababu kuja huku lzm wale wakubwawamshike mkono tu
 
Anunue viwanja ddoma ajenge apartment huku ata huku dar anawweza akawa anpiga peza tu bila pressure kubwa ....ila naona Kaka zake wale wasomi watamshauri nn Cha kufanya coni sababu kuja huku lzm wale wakubwawamshike mkono tu
Mkuu nmeweka wazi rafiki hana taaluma sana kwenye haya mambo ya biashara, sasa huko kwenye kujenga apartments si ndio atapigwa sana na mafundi 😂 kwa juu juu hio milioni 320 kwa mwezi naskia unalamba Milioni 3, huko kwenye apartment vp?

Mkuu ukiona mwanafamilia kaanza kuulizia ushauri kwengine ujue huko kwa kaka na dada zake ushauri waliompa kwake hawezi kuutendea kazi, pia jamiiforums ni mjumuiko wa watu wengi wazoefu hasa katika hili jukwaa maalum la biashara,
 
Mkuu nmeweka wazi rafiki hana taaluma sana kwenye haya mambo ya biashara, sasa huko kwenye kujenga apartments si ndio atapigwa sana na mafundi [emoji23] kwa juu juu hio milioni 320 kwa mwezi naskia unalamba Milioni 3, huko kwenye apartment vp?

Mkuu ukiona mwanafamilia kaanza kuulizia ushauri kwengine ujue huko kwa kaka na dada zake ushauri waliompa kwake hawezi kuutendea kazi, pia jamiiforums ni mjumuiko wa watu wengi wazoefu hasa katika hili jukwaa maalum la biashara,
Sense huko huko kwenye bond ni safe na salama .

Achukue coupon za miaka mingi

Sent from my TECNO P703 using JamiiForums mobile app
 
Tafadhali jaribuni mfike Dar es Salaam Stock of exchange kuhusu masuala ya Ununuzi wa Hisa za makampuni mbalimbali na gawio lao kwa mwezi na mwaka, Hapo mtapata taarifa zote kwa uhakika
 
Tafadhali jaribuni mfike Dar es Salaam Stock of exchange kuhusu masuala ya Ununuzi wa Hisa za makampuni mbalimbali na gawio lao kwa mwezi na mwaka.
Mkuu huko kwenye hisa naskia ni risk endapo zikishuka bei ni hasara ndio maana nimeshauri anunue bondi, naomba unisahishe kama nmekosea maana na mimi haya mambo nayajua kwa juu juu tu.
 
Nunua viwanja Dodoma,Jenga vi apartment vitatu,vya vyumba viwili,kila ki moja 35M,hivi kila kimoja unapat 350K kwa mwezi,nunua hisa/bond za Bot,au crdb,usiwekeze kwenye magari,madaladala utapasuka kichwa.jenga godown,Morogoro,Dodoma weka mpunga,wakutosha,koboa,uza,piga pesa.nunua hisa,Tigo,Voda,kama ni mtu wa town,nunua ka IST,fanya Uber,bolt,unakulaa kiulaiiiini,Ijumaa,au jumapili,masijid,au church unamuomba Mungu,then piga miluzi,
 
Ndio tujuzane mkuu, kumbuka huyu rafiki hajui sana mambo ya biashara, yeye labda nlichoona kitamfaa ni kuweka hela na kusubiri mapato ya uhakika ndio nikamshauri hizo bondi maana hazina mambo mengi, nlitaka kumshauri kufungua gym ila bado nikaona huki anaweza kufeli

Ika mkuu tueleezane hio biashara
Sure mkuu hapo Hana uwoga yeye ni kusubiria. Mfano akipata Bond za bot riba ni 13% so kwa iyo 300M anapata kwa mwaka 39 ambayo kila mwezi ni 3.25M bila kuwaza Sana. Asiingie biashara kichwa kichwa Sana.
Mana kwenye battle field ni tofauti kabisa kwenye mafunzo.
Huko emotions Ina overtake normal thinking brain hii rational brain. Amabyo unapenda certainty Bali uncertainty haupendi.
Ishu nyingine ya uhakika sijui yupo mkoa gani mwambie ajenge nyumba apangishe.
Apige self ya two bedrooms kadhaa hapo apangishe.
Kama Ana kiwanja na sijui yupo mkoa gani kwa fasta fasta Sana 30M unakamilisha two bedrooms afu atapata 2mpaka 5M kwa mwaka so Kama Ana nyumba zake Kama 10 ama tano atakuwaje.

Mwambie aachane na bajaji vijaana wanasumbua hawajaariki kabisa.
Labda huyo rafiki yako awe anaendesha mwenyewe.

Mie mkuu nasisitiza Sana nyumba Mana Haina hasara na value unaongezeka kila siku pia ni maisha kabisa mpaka anakufa anaziacha.

Pia anaweza akawa anazitumia hizo nyumba kukopa benki na kuongezea nyumba zingine.

Yaani akipokea 30M Kodi kwa mwaka at once anachukua benki hata 10M anasimamisha another three bedrooms houses.
So kila mwaka anaweza akawa anajenga nyumba akiwa siriasi .

Mwambie yeye Kama ameachiwa 300M yeye ajitahidi aje kuacha 10× ya hela iyo.

Mwambie apigane Sana.
Biashara nyingine ni kununua fuso tandem awe anakusanyia mazao vijijini na kuuza mjini awe na store ikiwezekana aweke na mashine.adili na nafaka.
 
sky soldier Calculation ya masoko ya hisa ni nyepesi sana wala usiumize kichwa mkuu

Inategemeana na investment yako its either long or short investment, hapo kwenye short ndo huwa kuna hasara nyingi kama ulitegemea baada ya mwaka mmoja niwe nimepata faida yangu utakuwa umefeli ila kwenye long utakuwa umeweza coz unatia mpunga and then unategemea kupata faida yako baada ya miaka 3 au 5,pia ukifika DSE utaweza kujua makampuni gani yana trend nzuri ya biashara yao kwa mwaka, na yapi trend zao sio rafiki,

kumbuka bank ya CRDB miaka mitano ya nyuma faida Waliokuwa wanapata ni ndogo kuliko wanayopata leo hii kwahiyo kama mtu angeweza kuweka mzigo miaka hiyo nyuma leo hii gawio lake Lingekuwa kubwa sana

Kuna hisa za makampuni zinafanya vizuri katika uwekezaji kama Drinking beverages, Cigarettes company etc, Pia Bila kusahau hata hizo treasures bond za serikali pale BOT, it's real deal Mkuu.

Ila kwa kujifunza zaidi jaribuni kutembelea DSE ili muwe na uhakika na mnachotaka kukifanya in more details
 
Aje awekeze hapa.. hostel au hotl kunafaa sana

 
Kwa tz Hatua zipoje kupata hizo bondi?

Aweke kiasi gani?

Atapata kiasi gani?

hicho kiasi kinalipwa kila baada ya muda gani?

Achukue bondi za miezi au miaka mingapi?
Mkuu nachofahamu kwa Treasury bills ambazo ni za muda mfupi, atachagua kulipwa baada ya siku ngapi zinakuwa au 35,91,182,364. Mfano hapo chini angeweka milioni 200 (kwa bei ya mnada uliopita) atakachopata kimeainishwa hapo kwenye (Net gain)
Screenshot from 2021-07-27 19-24-06.png


Kama ni Treasury Bonds ambazo ni kwa muda mrefu, kama angeweka milioni 200 ((kwa bei ya mnada uliopita) kiasi atakachopata kimeainishwa hapo kwenye (Total Gain)
Screenshot from 2021-07-27 19-24-45.png


Niliwahi kufuatilia hiyo opportunity nikawa tu discouraged na returns kwa sababu hela niliyokuwa nataka kuwekeza ilikuwa ndogo sana (5m)
ila kuna video hapa inaelezea kiundani kuhusu uwekezaji huo na faida zake kutoka benki kuu (BOT)
 
Back
Top Bottom