Anakatazwa kutoka ndani!!

sawa kabisa....huyu dada amevuka mipaka sasa, yaani anataka kumbinafsisha kaka wa watu na mkaka nae kashalegea...akipata shida huyu kaka huyo mama atamkimbilia nani kama kila mtu kwake mbaya?

Kumbuka wivu ni nature na nature huwezi uka icontrol so dada yupo sahihi.
 
Upo sawa kabisa, lakini huyu ndugu yangu yeye kawa tofauti kila anachoambiwa na mkewe ni kukubali tu.


Kama imefikia hatua hiyo, sidhani kama anaweza tokea mtu yeyote nje kumsaidia.
Mabadiliko yanatakiwa yaanze kwake kwanza. Akubali kuwa ana tatizo, akubali mabadiliko. Bila hivyo, ni sawa na kumpigia mbuzi gitaa.
 
Nadhani hajiamini labda kwa kuwa ni mama wa nyumbani!
Mwambie kuchamba kwingi ni kushika m*vi,unaona sasa jamaa kashaanza kushtuka, sababu ya kutojiamini kwake atampoteza bure huyo my husband wake.
 
Muda wa kutoka kazini unajulikana, na anajua muda ambao jamaa anafika nyumbani kila siku, akichelewa kidogo tu lazima apigiwe simu kuulizwa yupo wapi na yupo na nani.

natamani huyu dada nimpe huyu kichwa maji wangu, cku mbili tu atanirudishia.....sasa kupigiwa cm ishu?....c inaitaga weeee mpaka bac! mwambie rafiki yako aache upuuzi.
 

:lol::lol::lol::lol:
 
sasa watawasaidia nn hapo? ni ishu ndogo tu ya huyo frnd wako kubadilika/kuwa na mcmamo fullstop!


Sawa sawa Nyamayao, bila jamaa kukubali kubadilika watatembea kutafuta wasuluhishi mpaka sori za viatu ziishe!
 
Halafu ukizingatia na wazazi wa huyu binti waliishamwambia huyu jamaa kuwa binti yao ni jeuri pindi akileta za kuleta amshikishe adabu sasa sijui kwanini jamaa anakuwa muoga na mpole kiasi hicho mpaka mwanamke amempanda kichwani anywayz haya mambo ya ndani ya nyumba huwezi kujua ni kitu gani hasa kilichopo humo natamani sana huyo hausigeli angeongea maana atakuwa anajua mambo mengi sana yanayotendeka humo ndani
 
Nahitaji kupoozwa na mtu kama wewe p'se mwone D.A kwa contacts.

Aku ukanifidq goti yangu maana jana ulivyoshabikia??? halafu kwa nini nimtafute DA na wakati wewe upo, au na wewe domo zito?
 
Angalau leo ana afadhali jana ilikuwa sijui ni pilipili kichaa au nini maana nilibaki mdomo wazi mwenzio

Hajatulia kabisa mwenzake bado niko honeymoon asiniletee uskeletoni wake hapa hahahahahahahaaa!
 
natamani huyu dada nimpe huyu kichwa maji wangu, cku mbili tu atanirudishia.....sasa kupigiwa cm ishu?....c inaitaga weeee mpaka bac! mwambie rafiki yako aache upuuzi.

Kuna wanaume wengine kwa wake zao kama majibwa koko hawafurukuti anaweza kudwa hivi hivi mbele za watu na akanywea.

Kuna siku nililikuwa nakunywa sebuleni na jamaa mmoja wa pale pale kitaa sasa jamaa story zimenoga mke wake akawa anamuhitaji nyumbani alikubwa amebanwa na hamu akatuma mtoto mara kwanza jamaa akasema nakuja baada ya dk.5 akarudi tena mtoto jamaa akasema nakuja zikapita dk.10 mama yule akaongozana na mtoto huku yeye akawa amejificha gizani akamwambia kamwite mtoto akaenda jamaa akasema mwambie nakuja yule mama akatoka huko gizani mpaka kwa jamaa akachukua bilauri ya kilaji akamwaga akamwambia nimekwambia nyumbani jamaa akawa mpole wkt pale pale alikuwa anapiga story jamaa ake anavyo nyanyaswa na mke wake basi jamaa huyoo akainuka kama kondoo. Mi nilicheka mpaka nikaharibu beer zangu kwa kucheua dah.
 
Samaki hapati ni mihogo na kisamvu. Huyu mama bana sijui yukoje hajafundwa huyu kha??!!!

Tunajishaua tukishapandishwa chati kama nini, mtu mwenyewe mama wa nyumbani hana mbele wala nyuma halafu anajifanya kuweka sheria, ngoja akamatwe na wajanja atajuta kuzaliwa.mi naona mihogo na kisamvu bado vitamu ngoja ale matobolwa tu huyo
 
Aku ukanifidq goti yangu maana jana ulivyoshabikia??? halafu kwa nini nimtafute DA na wakati wewe upo, au na wewe domo zito?

Mi kuongea siwezi mpaka mtu anianzishie mm ndo niendeleze.

Ya jana yaache leo si siku nyingine mama? Mbona wakumbushia yaliyo pita tugange yajayo.
 

Huyo jamaa yako nae kama poyoyo anatakiwa akaze makota awe shujaa ajiamini amwambie ina maana huniamini navyokwambia? tabia mbaya sana hii ya kujifanya unataka kuongea na watu waliokaa na mpenzi au mume wako kani hawezi kaa na kimwana akawa na rafiki zake?
 
Mi kuongea siwezi mpaka mtu anianzishie mm ndo niendeleze.

Ya jana yaache leo si siku nyingine mama? Mbona wakumbushia yaliyo pita tugange yajayo.
Kaza mdomo huo unaanzishiwa kila kitu au mazungmzo tu
 

haaii..ckujua kama ukicheua beer inaharibika hii mpya kweli, una vituko wewe cjui y humpati mwanamke kama wa jamaa hapa ndio anakufaa huyu.
 

Na mimi ya hivi hayanipi stimu kabisa, ovyoo mtu unajishindwa kujisimamia mwenyewe?
Mwanamme lazima uwe shupavu ukiingia ndani displine yaani mkeo anakuwa na heshima upendo na kawoga kwa mbali kwamba wewe ni baba wa familia mambo ya kipuuzi hakuna utoke uwahi kurudi ili mradi najua uko wapi basi inatosha
 
haaii..ckujua kama ukicheua beer inaharibika hii mpya kweli, una vituko wewe cjui y humpati mwanamke kama wa jamaa hapa ndio anakufaa huyu.

Mbona atakuwa anadundwa kila siku mwili wake utajaa puti

Yeah beer zote nilizicheua ikabidi niingie hasara ya kuanza kunywa upya kufanya coverage
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…