Njunwa Wamavoko
JF-Expert Member
- Aug 11, 2012
- 5,757
- 2,368
Wakuu,Nina Dada yangu anasumbuliwa na tumbo kwa muda mrefu sana huwa akienda kupima anaambiwa kuwa ni UTI na Typhoid basi anapewa dawa anatumia tatzo linarudi vile vile ni zaidi ya Mara tatu kila akienda kupima anapewa majibu hayo hayo sasa juzi hali yake ikawa sio nzuri baada ya kwenda hospital wakampiga x-ray wakasema hakuna tatizo maanana miguu nayo ilikuwa inamuuma kiasi cha kushindwa kutembea,
Wakamfanyia na ultrasound wakagundua kuna uchafu kwenye njia ya uzazi wakampa dawa akanywa kazimaliza lakini bado hali yake Iko vile vile tumbo linamuuma japo sio kama awali ila maumivu ya miguu ndo hayajawahi kuachaNaomba wataalamu humu mnisaidie nimshauri atumie dawa gani hapa naona za asili ndo nitakuwa na Imani nazo maana hospital huko kaanza kuhangaika mda mrefu sana ila hadi saizi hakuna nafuu naomba wale wajuzi wa matumiz ya dawa za asili (mlonge,tangawizi,mwarobaini,swaumu,n.k)
Ila hata kwa madaktari au ambao mmewahi kupata tatzo kama hili inaweza kuwa ni tatzo gani na atumie dawa gani.Nawasilisha kwenu
unaelezea kirahisi hivo yaani eti tumbo linauma hausemi...tumbo linauma upande gani,wakati gani?
Ndo maana mnachukiaga tiba za hospitali kama kujieleza kwenye ndo huku mtu unaamua kumuandikia tu mtu vipimo kulingana na uwezo wa kituo chako then unatibu kinachowezekana.
Jifunzeni kwenda hospitali zinazoaminika na sio vituo vya afya na vituo vya vichochoroni!