Anataka nimuoe, nahisi wameniunganisha naye

Anataka nimuoe, nahisi wameniunganisha naye

kumbe wenzetu mnaongea na mungu na hamtuambii?
MUNGU anongea na watu,,sema wengi hatuzingatii wala kuisikia na kuelewa,,Kupitia mawazo,Sauti,watu n.k tatizo lipo kwetu,,mfano unaweza ukachelewa usafiri ukalaumu halafu baadae unasikia limepata ajali,,unafikiri ni weww ndo umeepusha? Ishi maisha ya kumpendeza MUNGU utaanza kusikia Sauti yake ,,Barikiwa.
 
MUNGU anongea na watu,,sema wengi hatuzingatii wala kuisikia na kuelewa,,Kupitia mawazo,Sauti,watu n.k tatizo lipo kwetu,,mfano unaweza ukachelewa usafiri ukalaumu halafu baadae unasikia limepata ajali,,unafikiri ni weww ndo umeepusha? Ishi maisha ya kumpendeza MUNGU utaanza kusikia Sauti yake ,,Barikiwa.
kiazi wee
 
Habari ya uzima wenu wapendwa,,namshukuru MUNGU kwa kutulinda na kuwa hai mpaka sasa ni kwa kusudi lake.

Mimi ni kijana nina umri wa miaka 29,ni mlokole nasali kanisa la T.A.G
MAADA:
Kuna changamoto ambayo nimeamua kushare nanyi naamini kuna ushauri ntapata kupitiia ninyi,,
Kuna mabinti kadhaa wamekuja kwa nyakati tofauti wakidai wananipenda ni wa hapo kanisani pia lakini wengi nilipowapima wanataka uasherati baadae ndoa kiukweli nilikuwa nikiwakatali nakuwambia ni dhambi na nilaana kweli walikuwa wakinielewa,,,katika Maombi MUNGU alikuwa anawafunua kuwa njia zao hazipo sawa maana yake hawajajikana na kuubeba msalaba,,

NISIWACHOSHE:
Kuna Mama mmoja ambae ni jirani na nilipo panga,,huyu mama amekuwa akisafiri ananiacha kwa nyumba yake ili nikae pale akiwa kasafiri nimekuwa nikifanya hivyo hadi anapo rudi ,,tunaitana Kaka na Dada hajaenda sana kiumri,
Ilitokea kuniamini saana kutokana na maisha yangu kijamii na kikubwa zaidi ninavyo mtumikia MUNGU kwa bidii,maana amekuwa akirudi anakuta mambo ni Safi+Usalama katika nyumba yake,

POINTI KUU:
Alipata mfanyakazi wa ndani kutoka pande za BK(Mhaya) ana kama miezi 7 hivi kama sikosei yupo pale,,tukazoeana nae kama majirani baadae nikamuulizia mambo ya imani akadai alikuwa akisali E.A.G.T mwanzo alikuwa K.K.K.T baadae nikamwambia tuanze kusali wote asikae bila kusali,,amekuja kama Jumapili 3 hivi akaacha Tena kumfatilia ameenda kusali kanisa jingine E.A.G.T,basi nikamshauri mambo ya kiroho nikamwambia inatakiwa usimame sehemu moja na uwe na Baba mmoja wa kiroho akawa amenielewa baadae nimshawishi akasimama sehemu moja mpaka sasa tunasali nae,,

CHAKUSHANGAZA:
Sikumoja yule Dada wa nyumba ile akaniita niende kwake ilikuwa saa 9 alasiri,nikaenda nikakaribishwa sebleni baada ya kusalimiana na mazungumzo kidogo,,nikaambiwa Y tumekuita hapa kwa jambo zuri tu la KIMUNGU ,nikasema sawa Kaka,,niliyekuwa nazungumza nae ni mme wa yule Dada wa nyumba ,akaniuliza Y unampenda T?! Kiukweli hilo swali skulijibu maana nilishitukizwa sikujua ni nini nimeitiwa nikatafakari bila kujibu,,akaulizwa T,,unampenda Y ?! Akasema ndiyo! Nikawaza moyoni mmh!
Kufupisha story,, Nikitoka pale bila kuwapa jibu nikawaambia wanipe muda.

Baada ya hapo binti amekuwa amekuwa akinganda kwa maswali ya kila aina je,nampenda kweli?,Mara anahisi me simpendi,,Mara Nampa majibu ya mafumbo!

Anasema pale nyumbani wananipenda wanatamani yeye aolewe na Mimi,,maana kwa usminifu wangu ntaishi nae.

Kuanzia hapo binti amekuwa akinitumia jumbe nyingi,,je,nampenda kweli maana anataka me nimuoe,Mara haamini kama nampenda,
Me nimemwambia tuingie kwa Maombi tumuulize MUNGU kama akithibitisha itakuwa,
Wazazi wamekuwa wakimlazimisha aolewe kuwa umri umeenda,hadi wamefikia kumtaftia mwanaume wa kumuoa lakin alikataa,,lakini hayo yote yalitokea kabla ya hili Jambo langu.

MOYO WANGU haujafunguka kabisa juu yake nifanyeje?

Msaada maamzi sahihi yanahitajika maana ndoa ni maisha,,
MUNGU awaongoze vyema.
Dalili za kishoga hizo
 
Ni mfanyakazi wa ndani (Mhaya).
Dada wa nyumba ile alikuita (mazungumzo yakafanyika).
Wazazi wake wanamtaka aolewe.

Mambo ni mengi
 
Huwa nashangaa wale wanawake Wenye kauli mbiu "lazima tutest mitambo Kwanza au tupimane Kwanza" ...naona kijana hapa ndo aliokumbana nao huko kanisan
Unashangaa nini sasa?unataka kununua mbuzi kwenye Kiroba?ngoja uolewe halafu ukute mzee umeme hauwaki
 
Huwa nashangaa wale wanawake Wenye kauli mbiu "lazima tutest mitambo Kwanza au tupimane Kwanza" ...naona kijana hapa ndo aliokumbana nao huko kanisan
Tatizo jinsia zimeongezeka ndio maana wanataka waprove kwanza.
 
BIN Shaib mlokole, basi sawa
mlokole unakuwaje na jina bandia, yaani unatudanganya jina, yaani wewe ni muongo
 
Unavaaga suruali za vitambaa na shati za mikono mirefu unachomekea
 
SEMA UMEOKOKA SIYO MLOKOLE
ameokoka?
aliyeokoka ni yule ambae kamaliza safari.....

huyu alitakiwa kusema "yeye ni mwanafunzi wa Yesu" a.k.a mkristo...... (sema siku hizi hata wasio wanafunzi wanajiita wakristo),

kwenye biblia hatuna walokole, tuna waamini
 
Back
Top Bottom