Anayeijua hospitali nzuri kwa matibabu jijini Mbeya anijuze haraka

Anayeijua hospitali nzuri kwa matibabu jijini Mbeya anijuze haraka

ufumawicha

JF-Expert Member
Joined
Mar 16, 2014
Posts
504
Reaction score
209
Ni miezi mitatu nimehamia kikazi hapa jijini Mbeya.Tatizo ninasumbuliwa na tumbo linaniuma sana.Huwezi amini maumivu yamefika kiunoni na mgongo wote hadi shingoni.Nimeenda pale rufaa wamenifukuza eti sina barua ya rufaa wakadai niende mkoani nako sikupata huduma yoyote.Naomba mwenye kujua hospitali yoyote anijuze hata kama ni ya private.Nimeshajaribu na dawa za fadhaget zile za tiba lishe ajabu ndiyo zimeongeza tatizo.Nisaidieni wadau!
 
Kuna zahanati moja iko mbeya nyuma ya hotel ya GR maeneo ya Soweto wako vzr ila jina nimesahau. Cheki ancers
 
mi mbeya sijawai fika ungekuwa mkuu rombo labda ningekushauri uende huruma hospt.au k m c
 
Huu ugonjwa wa ancers ndo upoje? Unashambulia sehemu gani haswa na unasababishwa na nini?
 
Iwe funzo, we unaumwa unaanzia fathergate?

Ungekaa kimya ingetosha kwa mleta mada kusoma watakaomuelewa na kumpa msaada(Ubinadamu kazi kweli kweli)

Pole sana mleta mada nenda kamuona Dr alaka iwezekanavyo mara utakapoelekezwa kimatibabu,
Kila la kheri Mungu akuafuu
 
kwa ujumla mbeya Hamna hospital nzuri zote ni ubabaishaji mtupu
 
Mkuu Aghakan iko wapi au eneo gani hapa MBEYA?Naomba unielekeze mimi niko hapa Iyunga.

Aghakan ipo uhindini jirani na posta. Ukitokea iyunga km unakuja mjini upo kwa daladala njoo mpk RETCo au sigara ni jirani na hapo.
 
Nenda hospitali ya IFISI ipo mbele ya mbalizi kama unaenda songwe njia ya kwenda tunduma. Pia unaweza funga safari ya kwenda hospitali ya IGOGWE mission ipo tukuyu shuka kituo kinaitwa kiwira madukani toka hapo utapelekwa na boda boda. Hao wapo vizuri kimatibabu, pia waweza enda pale nzovwe hospitali ya jkt shuka kituo mbembela pandisha juu mpaka njia panda ya halengo utaiona barabarani tu ila usiogope magwanda. We ingia ndani moja kwa moja
 
Kuna zahanati moja iko mbeya nyuma ya hotel ya GR maeneo ya Soweto wako vzr ila jina nimesahau. Cheki ancers

Inaitwa Ozzane, ni mkusanyiko wa madaktari bingwa wa mkoa wa mbeya.....lakini ufanyaji kazi wake ni jioni
 
Aghakan ipo uhindini jirani na posta. Ukitokea iyunga km unakuja mjini upo kwa daladala njoo mpk RETCo au sigara ni jirani na hapo.

Nashukuru sana amoxyclav,nitaenda hapo uhindini lakini kwa kuwa wewe unapajua gharama zao zikoje?
 
Niwekeni wazi kama hospitali hizo zinatumia bima ya afya au la
 
Back
Top Bottom