Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Ni aibu sana kujitambulisha kama mtanzania.....aibu sana,aibu kubwa,

Nchi ina mifumo vizuri kabisa....halafu inaachwa mifumo,watu wanajifanya wao ndio mifumo
Si aibu kujitambulisha wewe ni MTANZANIA sema ni AIBU wewe kujitambulisha ni KIJANA toka TANZANIA.....maana sifa moja wapo ya kijana wa kitanzania kama wewe NI mmbwia VIROBA
 
Hii kauli ya "masikini na wanyonge" inatia ukakasi,nikajua kwamba sisi na wao wote ni masikini tuateteana ili tuinuane,

Salalee!!

Kumbe wenzetu matajiri wa kupindukia,

Nashauri kauli mbiu ibadilike ili twende sawa
 
Hii kauli ya "masikini na wanyonge" inatia ukakasi,nikajua kwamba sisi na wao wote ni masikini tuateteana ili tuinuane,

Salalee!!

Kumbe wenzetu matajiri wa kupindukia,

Nashauri kauli mbiu ibadilike ili twende sawa
Na kibaya zaidi wanakwambia CCM imekufanya masikini wakati wao ni matajiri, ina maana hiyo CCM inabagua watu wa kuwafanya masikini
 
Hamkumuona mama Kijo lile gari alilopata nalo ajari? Kuna aliyekuwa anaelewa huyu mama anaweza kuwa anaishi maisha ya hivyo wakati yeye anaonekana mtetezi wa wanyonge?
 
Na kibaya zaidi wanakwambia CCM imekufanya masikini wakati wao ni matajiri, ina maana hiyo CCM inabagua watu wa kuwafanya masikini
Hivi nyie jamaa niaje? Kwani ni kosa matajiri kumtetea maskini?! Trump maskini? Yaani laiti ningekuwa na pesa ya kutosha ningewapatia. Badala ya buku saba ningewaongezea buku mbili ijifunge kumi ili muache kuudhalilisha utu wenu.
 
Hamkumuona mama Kijo lile gari alilopata nalo ajari? Kuna aliyekuwa anaelewa huyu mama anaweza kuwa anaishi maisha ya hivyo wakati yeye anaonekana mtetezi wa wanyonge?
Hela za maafa zilifika?
 
Hamkumuona mama Kijo lile gari alilopata nalo ajari? Kuna aliyekuwa anaelewa huyu mama anaweza kuwa anaishi maisha ya hivyo wakati yeye anaonekana mtetezi wa wanyonge?
Kujifanya unatetea wanyonge ni biashara inayolipa sana
 
Hivi nyie jamaa niaje? Kwani ni kosa matajiri kumtetea maskini?! Trump maskini? Yaani laiti ningekuwa na pesa ya kutosha ningewapatia. Badala ya buku saba ningewaongezea buku mbili ijifunge kumi ili muache kuudhalilisha utu wenu.
Sisi buku 7 ninyi kengeza na mamvi wanawaliapaje ?
 
Nani saa hizi anawaza nini kinachoendelea kuhusu uhaba wa chakula na mifugo inayokufa?

Nani saa hizi anawaza kuna wahitimu wa vyuo vikuu wa mwaka 2015/2016 wamenyimwa vyeti kutokana na bodi ya mikopo kutolipa ada?

Nani saa hizi anakumbuka kuna vijana wamekosa mikopo na saa hizi wanasota mitaani?

Nani saa hizi anawaza kuna vijana wamemaliza vyuo na wamekosa ajira?

Nani saa hizi anawaza kuna watumishi hawajaongezewa mishahara?

Nani saa hizi anawaza kuna watumishi hawajapandishwa vyeo?

Nani saa hizi anakumbuka kauli kuwa serikali haina shamba?

Nani saa hizi anakumbuka kuna wanafunzi walisitishiwa ufadhili wa masomo nje ya nchi?

Nani saa hizi anawaza wanafunzi wa kidato cha kwanza wanatakiwa kufanya mtihani wa mchujo kuchagua wanaotakiwa kuendelea na masomo na watakaofeli imekula kwao?

Nani saa hizi anawaza kuhusu matokeo mabaya ya mtihani wa kidato cha nne kwa mkoa wa Dar-es-salaam?

Nani saa hizi anawaza nini kinaendelea huko Chato?

Nani saa hizi anawaza kuhusu biashara zinazofungwa?

Nani saa hizi anaongelea tena habari za uchumi kuyumba?

Nani saa hizi anaongelea swala la bei ya unga?

Swala la shisha limeishia wapi?

Kampeni ya usafi nchi nzima imeishia wapi?

Ni lini tumewahi kuwa na live coverage kujadili au kuongelea maswala kama ya kupanda bei za vyakula,biashara kufungwa,mizigo kupungua bandarini, upungufu wa chakula,n.k.

Ni kweli tatizo la madawa ya kulevya ndio tatizo kubwa kuliko mengine yote?

Nguvu hii ya kupambana na madawa ya kulevya mbona hatuioni katika kuwatafuta wanaotuhumiwa kuochota mabilioni ya Escrow kupitia benki ya Stanbic?

Mbona CCM mkoa wa Dar-es-salaam hawakujitokeza kwenye vyombo vya habari kuongelea swala matokeo mabaya ya mkoa Dar-es-salaam kama walivyofana leo?

Kama hii ndio ilikuwa agenda,mbona kamishina wa Tume ya kudhibiti madawa ya kulevya alikuwa hajateuliwa siku zote hizo?

Tume hii imetengewa fedha kiasi gani katika bajeti ya mwaka wa fedha 2016/2017 ili kupambana na biashara hii?

Likiisha hili tusbiri tukio lingine.
 
mada kuu ni VIWANDA VIWANDA VIWANDA VIWANDA hapo hawawezi kutotoa kwenye reli
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…