Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Tutasimama imara kumuombea, hahitaji maombi ya wanafiki na wabwabwaji!

Post sent using JamiiForums mobile app

Kwa mbio hizi anazokimbia Angalie [emoji964] isije ikamshinda usukani. Yapo mazuri anafanya na yapo mabaya anafanya ambayo yamefanya wanachi tugombanie fito wakati tukijenga nyumba moja. Hii nchi ni yetu sote watanzania ni vyema sasa tukae pamoja tushirikiane katika kuijenga ikawa bora zaidi kuliko kilipiana visasi kwa vitu ambavyo vilikuwa vya kibinafsi............Hakika maisha yamekuwa mashaka hususani kwa watanzania wengi wale tunaojitambua ila woga wetu ndio umasikini wetu.
 
Kwa assessment ndogo niliyoifanya basing on facts,ukiitishwa uchaguz mwingine sasa hivi ambao utakuwa ni free and fair election; jombaaa hatoboi ozone layer.

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Tutasimama imara kumuombea, hahitaji maombi ya wanafiki na wabwabwaji!

Post sent using JamiiForums mobile app
Hata ulichoandika huna uhakika nacho. Kudagadesa!

Sent from my Siemens c35 dole-gumba using JamiiForums app.
 
AWAMU ijayo kipitishwe kipengere ktk katiba cha kuwapima afya ya akili na mwili wagombea kabla ya kupitishwa
na NEC
barabara kabisa maana wanasema uchizi sio mpaka utembee na chupi kichwani lazima tuwapime kwakwel maana dereva wetu kichwani kuna nati zimepotea[emoji23] [emoji23]

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Kwa assessment ndogo niliyoifanya basing on facts,ukiitishwa uchaguz mwingine sasa hivi ambao utakuwa ni free and fair election; jombaaa hatoboi ozone layer.

Post sent using JamiiForums mobile app
Awezi kutoboa wanachama wenzake wamekata tamaa na dereva wao mapema kabla ya safari[emoji23] [emoji23] [emoji23]

Post sent using JamiiForums mobile app
 
Wacha leo tukujadili na wewe salary je upo swafi kwa yote uyatendayo hujamdhulumu mtu,usiniambie mtaje!
 
Rais wangu naomba Ujumbe huu ukufikie!
Mimi ni raia mwenye mapenzi na nchi yangu! Mwaka 2015 niliacha kazi kwa hiari baada ya kuchezewa rafu nyingi kazini!
Juzi nilienda PSPF kuanza mchakato wa kuomba fao langu kupitia michango yangu niliyokuwa nakatwa ili niweze kujikimu kimaisha na familia yangu! Nilipewa majibu yafuatayo;
1. Sheria hairuhusu fao la kujitoa hadi nifike miaka 55/60
2. SSR wametoa tamko fao la kujitoa halipo
Nimewauliza tena wamenambia nirudi nikiwa na umri tajwa hapo juu kwa sasa Nina miaka 35!
Kwa sasa sina mpango wa kuajiriwa tena kutokana na experience niliyoipata kwenye ajira! Ninafikaje miaka tajwa hapo juu na watoto wangu 3 wanahitaji kusoma,kula,kuvaa,kutibiwa nk? Nisaidie mkuu tafsiri ya maendeleo kwangu ni nini? Je ni barabara wakati pesa ya nauli sins? Je ni matibabu au hospitality nzuri wakati pesa wala bima ya afya sina? Je ni daraja la kigamboni wakati gari sins? Nk!
Ninauliza tena pesa yangu ambayo ndio mtaji wangu na jasho langu nitaipataje nikiwa ningali haiii? Kama kuna mafunzo ya kusurvive bila pesa mtaani ningeomba ufadhili nikasome mafunzo hayo! Kama ulivowakumbuka wamachinga kama sehemu ya jamii ya wanyinge fumba macho tuondolee shetani huyu aliyetengenezwa na waliekutangulia anatesa watu saaaana! Neno linasema Mfalme mwema atawalapo watu hufurahi!
Naomba kuwasilisha!!!!!
 
Hivi Magufuli ana huruma kiasi hicho? By the way kasanga70 ni mtu wa kanda gani vile?
 
Pesa hakuna mtaani

Hakuna ajira

Hakuna huduma za afya nzuri

Biashara zimekwisha

Ukandamizaji wa demokrasia

Matumizi ya nguvu

Maamuzi ya kukurupuka

Mfumuko wa kutisha wa bei

Uhaba mkubwa wa bidhaa nchini

Halafu eti kuna wanaotaka abaki
mimi natamani aondoke hata kesho huyu ni dikteta mtawala wa mabavu



Ni wakati wa upinzani kuanzisha opereshen ya ng'oa magufuli



Aondoke tu hana faida kwetu

Wanaofaidika naye ni watu wa chato tu
 
Yaaani mdudu huyu wacha tu.

Soon atazima mitandao yote ya mawasiliano kama hatutapiga kelele sasa


Swissme



Swissme
 
Kama hukumchagua Magufuli hutamwelewa na hata Ukielekezwa na wanaomwelewa hutaelewa,cha msingi wafuate ambao hawakumchagua wenzako ambao wamemwelewa wakusaidie kukuelewesha....kukusaidia anza na MADIWANI WA ARUSHA...wao wameelewa watakuelimisha alivyo Magufuli.

Usisahau ASIYEJUA MAANA HAAMBIWI MAANA...ALALAYE USIMUAMSHE...PILIPILI USOZILA ZAKUWASHIANI...AKUNYIMAYE KUNDE AKUPUNGUZIA MASHUZI...



Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni awamu ya watu ambao hawakujiandaa na hawajui principle za uongozi na matokeo yake kila kitu ni matatizo na wamebaki kupiga makelele tu majukwaani.

Ni watu ambao wako outdated kabisa kifikra, kimawazo,n.k na ni kama watu waliokosa kabisa exposure na huko mbeleni hata dunia nzima itaanza kuwazomea.

Ni watu wenye fikra,mitazamo na mbinu za miaka ya 60,70 na 80 katika utendaji wao.Yaani wana fikra za karne ya 20 na wanategemea fikra na mitazamo hiyo iliyopitwa na wakati ndio italeta tija katika ulimwengu huu wa leo!

Baada ya muda mfupi watajikuta wanadharaulika na kila mtu na kila mahali.

People possesing smart phones need smart leaders to match with and not otherwise


Nawaambia pole yao!
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…