Rais wangu naomba Ujumbe huu ukufikie!
Mimi ni raia mwenye mapenzi na nchi yangu! Mwaka 2015 niliacha kazi kwa hiari baada ya kuchezewa rafu nyingi kazini!
Juzi nilienda PSPF kuanza mchakato wa kuomba fao langu kupitia michango yangu niliyokuwa nakatwa ili niweze kujikimu kimaisha na familia yangu! Nilipewa majibu yafuatayo;
1. Sheria hairuhusu fao la kujitoa hadi nifike miaka 55/60
2. SSR wametoa tamko fao la kujitoa halipo
Nimewauliza tena wamenambia nirudi nikiwa na umri tajwa hapo juu kwa sasa Nina miaka 35!
Kwa sasa sina mpango wa kuajiriwa tena kutokana na experience niliyoipata kwenye ajira! Ninafikaje miaka tajwa hapo juu na watoto wangu 3 wanahitaji kusoma,kula,kuvaa,kutibiwa nk? Nisaidie mkuu tafsiri ya maendeleo kwangu ni nini? Je ni barabara wakati pesa ya nauli sins? Je ni matibabu au hospitality nzuri wakati pesa wala bima ya afya sina? Je ni daraja la kigamboni wakati gari sins? Nk!
Ninauliza tena pesa yangu ambayo ndio mtaji wangu na jasho langu nitaipataje nikiwa ningali haiii? Kama kuna mafunzo ya kusurvive bila pesa mtaani ningeomba ufadhili nikasome mafunzo hayo! Kama ulivowakumbuka wamachinga kama sehemu ya jamii ya wanyinge fumba macho tuondolee shetani huyu aliyetengenezwa na waliekutangulia anatesa watu saaaana! Neno linasema Mfalme mwema atawalapo watu hufurahi!
Naomba kuwasilisha!!!!!