Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.

Ni bora tu ubaki kuwa mjinga kuliko kujifanya mwerevu wakati unajua huyo ndio rais wako hadi 2025.

Mambo mengine ya kuwaza waza haya wakati ukijua hakuna chochote unachoweza kukifanya zaidi ya kupigana na hali yako katika kujiletea maendeleo yako wewe mwenyewe bila kusubiri maendeleo ya Magufuli ni upuuzi.

Unasubiri Magufuli akuletee maendeleo. Waliomtangulia wenyewe hawajaleta maendeleo na hata hao tunaowasubiri wakiingia madarakani walete maendeleo tutasubiri sana na wakiingia hawawezi kuleta hayo maendeleo.

Maendeleo yaanze kwa mtu mmoja katika maisha yake. Hayo ya Magufuli yakija au yasipokuja atajua mwenyewe.
 
Kabisa Mkuu! Familia ya watu wachache tu ilimshinda ataweza kuongoza watu zaidi ya milioni 50. Nilisukumizwa! Sasa kama ulisukumizwa huku ukijua fika huna uwezo kwanini USIJIUZULU? Badala ya kuendelea kuivuruga nchi yetu?

Uongozi bora unanzia kwenye familia, kama mtu umeshindwa kuiongoza familia yako sidhani kama utaweza kuongoza kikundi/jumuiya ya watu.
 
nakucorect kidogo msomi international space unayoiona juu mrussia ndio yake bt wana special agreement na marekani,china,japan pamja urope countries..
 
Maendeleo ya kweli yataletwa na watanzania wenyewe na ni kwa kuchapa kazi tu hakuna njia nyingine
MAGUFULI:najua maneno haya ni machungu lakini ndio ukweli asiyefanya kazi na asile
Tulimchagua atuambie ukweli
Hapa ni kazi
 
Magufuli hawezihata ku maintain nchi ibaki hapa ilipo, anaangusha uchumi, anarudisha nyuma siasa.

Sio tu haleti maendeleo, bora angekuwa haleti maendeleo lakini katusimaisha tulipo.

Magufuli anaturudisha nyuma sana.
 
Tena ujinga wa hali ya juu sana
 
hali inaweza kubadilika,

he still have time
Ipo siku humu baada ya miaka kupita baadhi ya watanzania wasiojua maana ya maendeleo watakuja kuwambia watoto wao kuwa wameshindwa kuwapa huduma nzuri kwa sababu ya magufuli[emoji38] [emoji38] [emoji38]
Siku mwanao atakapoenda peku na ukamsingizia magufuli[emoji38] [emoji38] [emoji38]
Siku familia yako itakapojikunyata kwa njaa wewe ukiwa unamfanyia usaili magufuli na ukamsingizia yeye[emoji38] [emoji38]
Siku utakapojikuta cheti chako kimo ndani kama picha za kumbukumbu kwa elimu yako ili hali hakuna mchango wowote wa elimu yako kwa maisha yako na ukamsingizia magufuli[emoji38] [emoji38] [emoji38]

Hizo siku ndizo utakazojua nini maana ya hapa kazi tuu[emoji38] [emoji38] [emoji38] [emoji38]
 
Nawasihi Watanzania wenzangu, tuweke akiba ya maneno. Asante
 
Sigara Kali, uzuri na ubaya wa demokrasia ni kwamba kila mtu, hata mjinga ana haki ya kuamini atakavyo. Mimi binafsi pia nawashangaa wanaoamini kuwa serikali ya magufuli italeta maendeleo katika nchi hii. Hata hivyo sidhani kama wanaomini hayo ni wajinga na kama ni wajinga basi iko siku ujinga utawatoka na wataufahamu ukweli. Wasi wasi wangu ni kwamba yawezekana ni wapumbavu na kama ni wapumbavu tusitarajie mabadiliko katika fikra.

Hata hivyo nina imani kuwa wapumbavu ambao kwa kawaida huwa ni 'wadanganyika' endelevu, wamepungua mno katika nchi hii; yaani sasa hivi watu hawadanganyiki tena.

We subiri uone nini kitatokea pindi wakitindikiwa na uvumilivu!
 
Mpaka leo mnakuja na kutambia Magufuli hafai lakini hamtwambii m badala wake awe nani??

NI UJINGA KWA MTU MWELEWA KUTEGEMEA MAENDELEO KUTOKA KWA MWANASIASA YEYOTE YULE HAPA DUNIANI.

Hakuna nchi hata moja iliyoweza kuwaajiri wasomi wake woooooote waliohitimu kutoka vyuo mbalimbali duniani?

Usomi wa mtu faida yake ni kumtatulia mtu changamoto zake, vinginevyo unakuwa ni utumwa wa aina nyingine tena.

Faida ya msomi ni kutatua changamoto za maisha katika jamii ili jamii ijivunie kusoma kwako, shida inakuja pale wewe mwenyewe unapokuwa changamoto hasi katika jamii yako.

Kuna mifano ya wasomi wachache anbao elimu zao zimetumika kutatua changamoto za jamii zao na hao hutawasikia na kelele hizi.

KILA SIKU UNALIA LIA SERIKALI IKUFANYIE NINI, WEWE UMEIFANYIA NINI TOKA UWEMO HUMU??
 
Baelezeee papaaa
 
Status
Not open for further replies.
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…