Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Umesahau hili kundi la tulioumia kwa mbeba maono wetu kupigwa marisasi hadi kufikia hatua ya kuchungulia kuzimu!!
 
Sioni Magufuli akipata hata 30% ya kura. Atapata kura za akina Makonda na ndugu zake wa Chatto anaowapa uteuzi kila siku.

Wa Tanzania wote au wenyewe au ndugu zao amewaathiri kimaisha kwa maamuzi haya:-
-Kuwaondoa wanafunzi wa UDOM waliokuwa wanasoma ualimu wa sayansi
- Kufuta wafanyakazi wa vyeti feki
- Kuwatumbua wafanyakazi bila kufuata sheria
- Kutopandisha mshahara na madaraja
- Kutotoa ajira kwa wahitimu wa vyuo
- Kuvunja nyumba za Kimara na kuachia za Mwanza
- Kubagua maendeleo majimbo ya wapinzani kama Kilwa
- Kuzuia wanafunzi wenye mimba wasiendelee na masomo
- Kumtimua CAG makini kwa vile kuulizia ufisadi wa Tsh 1.5 Trilion
-Kuua wakosoaji kama BenSaa Nane na Azory Gwanda
- Kutumia vibaya fedha za Serikali kama ujenzi wa kiwanja cha Ndege Chato na mbuga ya Burigi
- Kuwaweka rumande wafanyabiashara kwa makosa ya kubambikiza kama Rugemalira
-Kuwabambikiza makosa wakosoaji kama Kabendera
- Kutunga sheria kandamizi
-Kutawala kwa kidikteta.
- Kuvuruga wafanyabiashara kama Yusuf Manji

Nimeikuta sehemu.
 

Attachments

Hii ni kumkumbusha Rais Magufuli. Nakupenda kama binadamu mwenzangu kutoka moyoni, lakini nachukia sana matendo uyafanyayo kwa wapinzani. Kwa kuwa nakupenda kama binadamu mwenzagu sitaki upate shida maishani hasa baada ya kustaafu, hivyo nakukumbusha kuwa Tanzania siyo sovereign (huru) kama matendo yako yanavyoonesha bali kuna mambo yamepandishwa juu na kuwa ya kidunia zaidi na ambayo huwezi kuyaweka chini ya himaya yako upende usipende. Mambo serikali haiwezi kuyaweka chini yake nitayaongea siku nyingine. Kwa leo nina hili pekee.

Ili upate maisha mazuri yenye heri na baraka baada ya kuachia madaraka, japokuwa umekwisha liboronga mpaka sasa, tenda haki kwa wapinzani wako kisiasa kwa muda wako uliobaki. Mbali na hapo utashitakiwa ICC - huko The Hague. Dunia inakuangalia kwa ukaribu sana, inajua ulalapo na uondokapo. Mfano wa wazi ambao unaonesha hauko huru kama unavyofikiria fungua google map utazame namna majina ya kila eneo na barabara ilivyoainishwa online, je hii ni kazi ya wataalam wako?

HAPANA. Pia kila njia unayotumia kwa mawasiliano siyo ubunifu wa Tanzania bali ni wa hao hao unaowaita mabeberu, hivyo wana kumbukumbu ya kila ulifanyalo, na uwaagizalo wasaidizi wako. Uchaguzi wa mwaka huu ni mtego kwako. Chunga sana.

Wape uhuru wapinzani kwani katiba inaruhusu wayafanyayo. Kitendo cha Sugu kukamatwa, ofisi za CHADEMA kulipuliwa na msafara wa Tundu Lissu kupigwa mawe ni doa kubwa sana kwako.

USIKU MWEMA
 
Mwalimu Nyerere aliwahi kusema, "Hatuwezi kuwa na Rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli, hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya Rais au Waziri Mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu.

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je, anajua jinsi ya kututoa?! Anajua anakotupeleka?

Nimejitahidi kuangalia Bunge ili nione labda Mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!
We shall overcome
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom