Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Yule jamaa aliyedhalilishwa mbele ya taifa ningekuwa mwandishi ningemuhoji kwa siri nifahamu hisia zake za kweli kabisa za ndani.aliposema baki na mafi yako ndo hakuonekana tena maskinii
Na huo nao unaona ni utetezi?nitajie mtu mmoja ambae hana mapungufu?
kama kweli basi hii nchi imelaaniwa huyu mtu ni tatizo tuuu
nitajie mtu mmoja ambae hana mapungufu?
Ukiona VP amekuwa Bashiru au mtu yeyote wa genge lile. Tegemea kurudi kulekule.Nadhani sasa sisi ndo tumekua huru tena
Nitamkumbua Magufuli kwa ukatili wake wa kutisha
1. Kuvunja nyumba za wananchi wa Kimara - Mbezi bila chembe ya huruma ila wale wa mwanza aliwaachia
2.Kupora Korosho za wananchi wa mikoa ya kusini kwa mtutu wa bunduki, hii hali iiwatia wananchi umasikini
3. Bila kujali kuwa watu wameshahudumu serikalini kwa muda mrefu na wanategemea kustaafu, akapitisha hoja ya uhakiki na kuwafukuza maelfu ya watu hao Huku akiwaacha bila kuwagusa wanasiasa na wateule wake katika hilo zoezi
4. Kubabikizia watu kesi za uhujumu uchumi, kuwatesa kupitia mfumo wa mashitaka na kuzisababishia familia zao maumivu makubwa na hali ngumu
5. Kuendelea kuwashikilia mamia ya masheikh walioko jela huku akisamehe wabakaji akina Babu Seya
6. Kukataa kuwapa watumishi wa serikai stahiki zao kwa wakati, ikiwemo kupandishwa madaraja na nyongeza za ishahara
7. Kuharibu chaguzi zote zilizofanyika chini ya serikali yake, kuanzia zile za marudio, serikali za mitaa na uchaguzi mkuu, Alidhuluu haki ya wananchi kuchagua viongozi wao
8. Magufuli alitunga sheria kandamizi, na kuvuruga misingi ya katiba. Kafanya kia jitihada kulifanya bunge liwe butu, kuiweka mahakama mfukoni etc
9. Magufuli alikuwa na kauli mbaya zisizo na staha mfano "sisomeshi wazazi, serikali siyo iliyoleta tetemeko, baki na mavi yako nyumbani, nitapiga mashangazi.. etc"
10. Alikuwa na miradi kadhaa au mpango wa miradi kadhaa ambayo ni white elephant mfano, uwanja wa ndege Chato, Midege,Mpango wa Uwanja wa mpira Chato
11..Magufuli alikuwa mkabila, huhitaji kuwa mwanasayansi wa elimu ya jamii kuona kuwa teuzi zake ziliaia sana watu wa kanda na kabila lake.
12. Magufuli alikuwa haheshimu katiba waa sheria pale zinapokinzana na anachokitaka yeye, mfano haki ya kufanya siasa kwa vyama vya siasa iliyokuwepo kikatiba hakuiheshimu
13. Magufulu hakuthubutu na wala hakujali kufanya uchunguzi juu ya kupotea kwa Ben Saanane, Azory Gwanda, Kanguye na waliompiga risasi Lissu
Kwa hiyo mimi nakichukulia kifo cha Magufuli kama nafasi muhimu ili Taifa letu lipone.
Na sisi kama Taifa, tumeona kwa macho yetu namna katiba ya sasa ilivyokuwa hatari kama tunampata mtu mmoja asiyejali, ambaye ana element za udikteta, basi tuitumie nafasi hii kuliponya Taifa
Tangulia Magufuli, uwongo mbaya sitokumiss na sijawahi kukupenda kwa style ya uongozi wako, ninatamani Taifa lisipate Kiongozi mwenye mapungufu ya aina yako, ni mapungufu hatari kabisa
Mlamba viatu mwingine huyu huku anateseka [emoji23][emoji23] too late!nitajie mtu mmoja ambae hana mapungufu?
Kutesa, kuuwa, kurundika watu magezani bila hatia ni worst than mapungufunitajie mtu mmoja ambae hana mapungufu?
Upo sahihi sana.Msubirie kwanza tuone mwelekeo wa huyu mama, huenda akawa mchungu zaidi kutegemeana na makamu wa Rais atakae mchagua.
Ulifaidika nini na hiyo Tanzani huru miaka zaidi ya 50 kabla ya JPM ? Au ndio unatafuta kichaka cha kuficha uzembe wako. Haya subirini sasa naona soon mtaanza kutajiwa idadi ya wagonjwa wa corona nchini ili mridhike na nafsi zénu