Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Anayejua Rais Magufuli anatupeleka wapi atuambie, naona kama tumepotea

Status
Not open for further replies.
Mwl Nyerere aliwahi kusema "hatuwezi kuwa na rais ambaye hatujui kesho ataamka amefikiria nini au ameshauriwa nini na mke wake". Kwa wakati ule kilionekana ni kijembe kwa mzee Mwinyi lakini leo kauli yake inaonyesha maana.

Hatujui mwelekeo wa nchi kiukweli hatujui kesho atafukuzwa na nani au ziara ya rais au waziri mkuu itakuwa wapi. Hatujui kama tutaamka tunafagia barabara au tutaingia ofisini kwetu kama kawaida.

Hatujui tunaanza na nini, kujenga viwanda au kuboresha miundombinu na kuimarisha kilimo ili tupate malighafi.

Hatujui tatizo la sukari kwa mfano linaondoka kwa kurekebisha viwanda vyetu na kuongeza uzalishaji wa miwa au kuruhusu sukari ya nje au tuvamie magodauni ya watu

Ukimuangalia usoni na ukasikia anachotamka unakiri ana nia kabisa ya kututoa hapa. Swali ni je? anajua jinsi ya kututoa?

Anajua anakotupeleka? Nimejitahidi kuangalia bunge ili nione labda mawaziri wake wanaweza kuonyesha mwelekeo, huko nikachanganyikiwa zaidi.

Mwanamtandao mmoja alisema unaweza kuwa na dereva mzuri anayefuata sheria zote za barabarani lakini hajui anaenda wapi!

Hivi unaposema " Hatujui" ni wewe na nani? Nani kakutuma umsemee?!!! Au ndiyo kutaka kujifanya mko kundi au kikundi chenye mawazo kama yako?!!! Semea nafsi yako... Kama mpaka sasa huelewi nini anafanya Rais JPM ... Basi tulia fanya shughuli zako za halali lipa kodi stahiki hayo mengine watafanya wanao husika na wewe utaona tu matokeo .....
 
Kujitegemea sio jambo la mzaha .
Kinachofanyika ni kurejesha Maadili na nidhamu ya Taifa Tuweze Kujitegemea.
 
Hivi unaposema " Hatujui" ni wewe na nani? Nani kakutuma umsemee?!!! Au ndiyo kutaka kujifanya mko kundi au kikundi chenye mawazo kama yako?!!! Semea nafsi yako... Kama mpaka sasa huelewi nini anafanya Rais JPM ... Basi tulia fanya shughuli zako za halali lipa kodi stahiki hayo mengine watafanya wanao husika na wewe utaona tu matokeo .....
Kama wewe hujachanganyikiwa umechelewa. Ukiwa unachanganyikiwa labda mimi ntakuwa naanza kuelewa tunapoelekea
 
Jamani au mimi ndo sielewi mnieleweshe?? Maana niliyotegemea kutoka kwa Magufuli ni tofauti na ninayoyaona

Nilichokitegemea ni uchapakazi uliopitiliza na mkazo mkubwa katika ukusanyaji wa kodi kutoka katika makampuni makubwa na migodi ambayo ilikuwa ikilipa kodi ndogo na mingine ikiwa hailipi kabisa

Kwa sababu alitwambia tanzania ni tajiri sana na atatumia utajiri wetu kututoa katika umaskin

Utajiri huo ni kama migodi,gesi,maji,mbuga nk

Sasa mbona hatutolei umaskin kutoka kwenye huo utajiri tulionao zaidi ya kuendelea kutukamua sisi maskini?

Kodi kwetu zimekuwa nyingi mpaka kero

Mfano mtu anamiliki mpesa:- analipia reseni tra na pia katika halimashaur husika analipa kodi,kwenye miamala serikali inakata kodi,kwenye malipo anayopata kutoka kwa kampuni anakatwa kodi,hela aliyolipwa akitaka kuitoa kwenye simu anakatwa kodi na sasa akitaka kumtumia mtu itabid akatwe kodi

Huyo mtu mmoja anakatwa kodi tano heeeee!!

Nahisi tutaisoma namba
 
Na mvimbe mpasuke, mtajijua wenyewe, mliipenda wenyewe mkadai kuwa nichaguo lenu milele, acha tuisome namba
 
Ni kweli, wengi mlidhani CCM ni ile ile...mlitegemea atakuwa upandewenu...kamwe haitakuwa hivyo
 
Hizo hela wanazohangaika kuandaa maandamano, kufungua kesi ,sisi wanachadema tunapendekeza wajenge ofisi za chama.

Ofisi ya chadema pale ufipa inatia kinyaa
 
Kiukweli,tukubali au tukatae,Nchi haina mwelekeo,hakuna anayejua kesho kuna nini wala hakuna mwenye dira ya kwamba tunaelekea wapi ni mizuka tu ya papo kwa hapo alafu inazima nziiiiiii!!

.....kweliiiii
 
Magufuli atafanya yaliyoko kwenye ilani na atapimwa kwa ilani ya CCM iliyopendwa na wapiga kura wengi....waliokosa muelekeo ni wale walioahidi kwenda kuchunga ng'ombe mara wakaahidi kwenda ICC na mara waahidi kuzunguka nchi na blah blah kibao.

Wakati wa Uchaguzi tuliwaonya sana muache kuwa Nyumbu na wazungusha mikono na badala yake msikilize sera na kupima kama zinatekelezeka....

Kama mngesikiliza Ilani ya CCM kama ilivyonadiwa na Magufuli usingekuja kuuliza pumba hizi unazouliza leo hii...

Magufuli aliahidi kupambana na Rushwa(Ni mgombea pekee aliyeongelea rushwa kwa hisia na kweli)....Mwezi wa Saba Mahakama ya Mafisadi inaanza kazi

Magufuli aliahidi kushughulikia Tatizo la mikopo elimu ya juu....Wanafunzi wamepata mikopo,bodi imefumuliwa na mikopo imeanza kurejeshwa.

Magufuli aliahidi elimu bure...Imeshaanza pamoja na changamoto zake.

Magufuli aliahidi kukusanya kodi na kuondoa viushuru vya ajabu ajabu...Salamu za bandari za nchi kavu umezisikia na kama unafuatilia kuna viushuru vya kwenye kahawa vimeanza kuondolewa.

Magufuli aliahidi kupunguza msongamano Dar....Mabasi ya mwendo kasi yameanza ns hapa majuzi kitwanga anaongelea kuhusu flyover kuanza kujengwa...

Magufuli aliahidi kurejesha nidhamu kwa watumishi wasio waadilifu....unataka niongee??

Magufuli aliahidi kuwanyang'anya mashamba wale wasioendeleza ....unataka kuniambia hujamsikia lukuvi??

Hivi hujasikia kiwanda cha tiles kilichoanza kujengwa Mkuranga ?hivi hujamsikia rais akiwaasa NSSF PPF kujenga viwanda badala ya maghorofa yasio na tija??

Pale Muhimbili CT SCAN ilikuwa ni kipimo adimu sana kukipata nadhani unaweza kuona nini kinaendelea Baada ya Rais kuzuru Muhimbili consistently (Changamoto ya dawa na vifaa tiba kuwepo kwenye vituo pamoja na ujenzi wa zahanati)....universal coverage ya bima ya afya ni sheria inayonukia mwezi septemba.

kuhusu maslahi ya wafanyakazi PAYE imeanza kufikia single digit as per july this year.

Kuhusu kuulinda muungano...Rais ametuvusha salama salmini bila tone la damu kumwagika kule Zanzibar pamoja na hila zenu zilizokosa uzalendo na za kuwategemea mabwana wa kizungu.

Ndio maana narudia tena kuwaita Nyumbu au pengine ni fisi mnaofuata mzoga ulipo maana hamjielewi mshike kipi.....

Matatizo yenu ya kupokea makapi na mizoga muyamalize huko huko msituletee shombo sisi wastaarabu!!!


MAGUFULI AMEFANYA ZAIDI KABLA YA MUDA WAKE KUANZA!!
Sukari vepee?
 
Akupeleke kwani wewe umekuwa zombie? Raisi Magufuli hayuko hapa kukupeleka wewe popote pale, bali wewe ndiyo unatakiwa ujipeleke mahali kwingine, wewe ndiyo unatakiwa ujitoe hapo ulipo na kwenda sehemu nyingine, wewe ndiyo unatakiwa ujifungue minyonyoro uliyofungwa na fisadi Lowasa, Mbowe & Co. na kuwa mtu huru Raisi Magufuli hawezi kulifanya hilo na wala siyo kazi yake!

Hilo ndio tatzo la watanzania, wao wanataka kila kitu wafanyiwe, hawajui wao ndio wa kufanya, wao ndio wa kubuni cha kufanya. Back in time pale raisi wa marekani alipo waambia wananchi Wake USIULIZE NCHI IKUFANYIE NINI, WEWE NDIO UJIULIZE UTAIFANYIA NINI NCHI YAKO.
My fellow Americans, ask not what your country can do for you, ask what you can do for your country.
 
Alivyosema zungusha zaidi hamkumwelewa kuwa mtazungushwa mpaka mpate kizungu zungu ccm mlisema mbele kwa mbele sasa ndio mlio kwenye masaburi mnaisoma no.
 
CCM imepoteza DIRA By Horace Kolimba(R.I.P.)
 
Watanzania jana walishuhudia kusomwa kwa bajeti ya kwanza ya awamu ya tano. Kwa vipindi tofauti Rais amekuwa akiomba aombewe kwa mwenyezi Mungu ili atende haki.

Kwa bajeti iliyosomwa jana, naamini kuna haja ya kuendelea KUMUOMBEA ILI ASITUPELEKE KWA NAMNA AMBAVYO BAJETI IMEWATENDA WANANCHI HASA WANYONGE.

1. TUMUOMBEE AACHE KUWAGANDAMIZA WANANCHI WANYONGE.
2. TUMUOMBEE AACHE KUGANDAMIZA DEMOKIRASIA YA USAWA WA SIASA HURU.
3. TUMUOMBEE AACHE KUJIONE YEYE NI FIKRA PEKEE HAPA NCHI NA HAKUNA WENYE MAWAZO MBADALA.


TUMUUOMBEE AWAOGOPE NA ASIWADANGANYE WANANCHI KWA MWAMVULI WA HAKI.
 
Waisalamu watatumia mwezi mtukufu huu kwa kufanya sala kwa ajili yake, wAkristo tusubir kwa rezma tutaomba, walokole waitishe Maombi ya dharula kwa kufunga wiki mojA, kwa ajili ya mh
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom