Ukiona Baba akiulizwa swali anakuwa mkali ujue hana jibu,
Hajui akujibu nini,
Hajui anakifanya kitamfukisha wapi,
Amepoteza mwelekeo anatafuta pa kutokea.
CCM sasa hivi Polisi ndio kimbilio lao,
Mwananchi akihoji kitu Jela,
Mwaandishi wa Habari akiandika kitu kuhusu Serikali Jela,
Vyama vya Siasa haviruhusiwi kufanya Siasa, Vikifanya Jela,
Na tena hii ni mbaya maana CCM wao kila siku wanafanya mikutano ya Kisiasa kupia Raisi, wakuu wa mikoa, Wakuu wa Wilaya, kiujumla CCM inafanya Siasa pekeyake kwa kutumia nguvu.
Ukiishiwa Sera ndio nguvu hutumika, CCM nguvu huwa zinazidiana kuweni makini.