Anayetumia passo ya piston 3(au fundi/mjuzi yeyote) tafadhali nisaidia ubora wake na udhaifu wake

Anayetumia passo ya piston 3(au fundi/mjuzi yeyote) tafadhali nisaidia ubora wake na udhaifu wake

yassin alluy

Member
Joined
Feb 4, 2017
Posts
27
Reaction score
64
Tuambie chochote maana zinakimbiliwa sana nyakati hizi kwasababu ya utumiaje wa mafuta ila je nini udhaifu wake ?
42245811.jpeg


Sent using Jamii Forums mobile app
 
mi ninayo Passo toka 2015,nipo nako hadi leo,ila kangu kana gonga sana miguu ya mbele,niliacha kitengenenza maana nakaa makorongoni nakaumiza we acha tu,...vigari vidogo shida sana,nikimaliza mkopo tu nakauza
Maana nilichukua mkopo sehemu nikaweka kwenyewe ndio dhamana
 
Lakini naona vinasoko sana sijui watu wamegundua nini tofauti na mafuta ulaji wake
mi ninayo Passo toka 2015,nipo nako hadi leo,ila kangu kana gonga sana miguu ya mbele,niliacha kitengenenza maana nakaa makorongoni nakaumiza we acha tu,...vigari vidogo shida sana,nikimaliza mkopo tu nakauza

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ni bora ununue starlet kuliko paso, by the way usihadaike na bei ya io paso itakutesa ukajuta tafuta gari standard usiwe na haraka sana angalau cc 1990 kama hizi premio au allion... Otherwise chukua subaru

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usirogwe kununua vigari vyenye piston tatu vina shida sana, me nilikuwaga na Suzuki Kei ilikuwa ni kila leo niko garage mara kamekata fan belt, mara kameunguza solenoid kwenye gearbox ikabidi nikauze tu. Kama ni gari ndogo chukua Vitz old model, ni vigari imara sana
 
Chukua toyota carina.gar nzur na inanusa mafuta.elf5 unafika mjin

Sent using Jamii Forums mobile app
Ki-ukweli Carina ni gari ngumu .Ni gari inayovumilia shida .Ni gari ya watu wenye kipato cha chini. Gharama za kuitunza ni za chini kabisa.

Labda changamoto ni kuwa gari hii imekuwa ya kizamani sasa. Na nyie vijana mnapenda kwenda na wakati.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom