Andrew Arshavin: Jasusi wa Urusi aliyejificha kwenye mchezo wa soka

Andrew Arshavin: Jasusi wa Urusi aliyejificha kwenye mchezo wa soka

nightwalker

Member
Joined
Jan 29, 2020
Posts
51
Reaction score
75
Unamkumbuka Andrew Arshavin?!

Wengi wanamkumbuka Andrew Sergeyevich Arshavin, kama winga machachari aliyekiwasha ndani ya klabu ya Arsenal. Lakini duru za kijasusi ulimwenguni zinamtambua kama jasusi kutoka katika Shirika la Ujasusi la Urusi, Federal Security Service (FSB) akitekeleza "mission" ngumu ya kuipeleleza serikali ya Uingereza.

Ilikuwaje?!

Mnamo mwaka 2012, kuna nyaraka zilivuja kwenye jengo moja lililopo mitaa ya Fort Meade, huko Maryland nchini Marekani, ambapo jasusi mmoja kutoka katika Shirika la Kijasusi la National Security Agency (NSA) nchini Marekani, aliijulisha serikali ya Uingereza akifichua siri ya kwamba mchezaji wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Urusi, Andrey Arshavin, alikuwa jasusi wa Urusi aliyekuwa na jukumu ya kuipeleleza serikali ya nchi hiyo, akijivalisha uhusika wa Mwanasoka machachari.

Andrew Arshavin, akitambuliwa kwa jina la ‘Red Fox’, aliandaliwa na Kremlin, katika mpango maalumu wa kijasusi, mhusika akiwa Bwana Sergei Rachmaninoff, ambaye anatambulika kama "The Brainchild of Kremlin Chief", kwani ndiye aliyefadhili mafunzo ya Arshavin akiwa kama wakala wake na akashiriki kwa kiasi kikubwa kuhakikisha mchezaji huyo anasajiliwa kwenye ya klabu ya Zenit St. Petersburg ya nchini Urusi ikiwa ni hatua za awali za safari yake ya nchini Uingereza.

Kwa mujibu wa Digital Spy Forum, wanaeleza kuwa, Arshavin alipenyezwa kwenye klabu ya Zenith St. Petersburg akiwa kama mwanasoka ambapo lengo kuu lilikuwa kuhakikisha anasajiliwa kwenye moja ya vilabu vikubwa vinayoshiriki ligi kuu ya nchini Uingereza (English Premier League).

Kabla ya kuanza "mission" yake, Arshavin alipewa jina maalumu (Code Name) akiitwa Red Fox. Akiwa Zenith St. Petersburg zikaibuka tetesi kuwa mchezaji huyo anahitajika na klabu ya Barcelona ya nchini Spain, dili hilo likamsukuma kocha wa Arsenal wakati huo, Profesa Arsene Winger kuingilia kati na kumsajili mchezaji huyo. January 31, 2009 alitangazwa rasmi kujiunga na klabu ya Arsenal maarufu kama The Gunners.

Adrew Arshavin alisakata soka ndani ya klabu ya Arsenal katika awamu mbili. Awamu ya kwanza, kuanzia 2009 hadi 2012, kisha achukuliwa kwa mkopo na klabu yake ya zamani ya Zenith St. Petersburg. May 31, 2012, akarejea tena Arsenal, na msimu wa 2013/14 akaondoka rasmi klabuni hapo na kutimkia Zenith St. Petersburg. Inaelezwa kuwa, hii ni baada ya kukamilisha "mission" yake.

Baada ya kuvuja kwa taarifa hii, ikielezwa kwamba hata taarifa za mchezaji huyo kutakiwa na klabu ya Barcelona hazikuwa na ukweli, bali zilitengenezwa tu kama tetesi ili kumpa thamani mchezaji huyo na kuvivutia vilabu vikubwa vya nchini Uingereza.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba, Warusi wenzake, Roman Pavlyuchenko na Pavel Pogrebnyak, ni majasusi wenzake wa Kremlin, nao walitumwa nchini Uingereza kwa majukumu ya kusaidia ujasusi wa Arshavin, na baadaye kumsaidia katika kutoroka kwake.

Hivi karibuni, Shirika la Ujasusi la Uingereza limefanya mawasiliano na Huduma ya Siri ya Ufaransa wakijaribu kuchunguza kama kocha Arsene Wenger wa Arsenal, alikuwa sehemu ya njama za Warusi.

Mwisho.

Imeandikwa na;- Hilal Kanal
Call/Whats;- +255 718 022 322
Dar es Salaam, Tanzania
September 10, 2024
FB_IMG_1726240449847.jpg
 
Ndio wenzetu walipofika na hata sisi kwa sehemu tumepiga hatua mfano mdogo tu ni udhamini wa goli la mama anachokifanya mh rais ni kuchagiza Simba na yanga ziende mbali zaidi in turn zile team kubwa kama Ahly wydad n.k zinapokuja nchini zinachangia pato la utalii kwa ukubwa sana kwa hapa nampongeza Rais kukuza utalii wa michezo kijanja na kuingizia nchi mapato
 
Source: Trust me bro.

Lakini haikumsaidia kitu Manchester united ikaitembezea Arsenal kichapo kikali cha kikatili bila huruma na kuichabanga kwa kuigaragaza Arsenyani goli 8-2 na yeye akiwepo
 
Turudi ktk FACTS.

Kipindi hicho kulikuwa na tajiri ROMAN ABRAMOVIC ambaye aliimiliki Chelsea kuanzia 2003, kwanini wasingemtumia MRUSI mwenzao kuweka afisa kipenyo mpaka watumie njia ndefu ya kudanganya Barca wanamuhitaji? Then Arsene wenger akurupuke from no where asajili mtu kisa barca walionyesha nia..

Tujiulize maswali madogo tu... ya maana.
 
Unamkumbuka Andrew Arshavin?!

Wengi wanamkumbuka Andrew Sergeyevich Arshavin, kama winga machachari aliyekiwasha ndani ya klabu ya Arsenal. Lakini duru za kijasusi ulimwenguni zinamtambua kama jasusi kutoka katika Shirika la Ujasusi la Urusi, Federal Security Service (FSB) akitekeleza "mission" ngumu ya kuipeleleza serikali ya Uingereza.

Ilikuwaje?!

Mnamo mwaka 2012, kuna nyaraka zilivuja kwenye jengo moja lililopo mitaa ya Fort Meade, huko Maryland nchini Marekani, ambapo jasusi mmoja kutoka katika Shirika la Kijasusi la National Security Agency (NSA) nchini Marekani, aliijulisha serikali ya Uingereza akifichua siri ya kwamba mchezaji wa zamani wa Arsenal na timu ya taifa ya Urusi, Andrey Arshavin, alikuwa jasusi wa Urusi aliyekuwa na jukumu ya kuipeleleza serikali ya nchi hiyo, akijivalisha uhusika wa Mwanasoka machachari.

Andrew Arshavin, akitambuliwa kwa jina la ‘Red Fox’, aliandaliwa na Kremlin, katika mpango maalumu wa kijasusi, mhusika akiwa Bwana Sergei Rachmaninoff, ambaye anatambulika kama "The Brainchild of Kremlin Chief", kwani ndiye aliyefadhili mafunzo ya Arshavin akiwa kama wakala wake na akashiriki kwa kiasi kikubwa kuhakikisha mchezaji huyo anasajiliwa kwenye ya klabu ya Zenit St. Petersburg ya nchini Urusi ikiwa ni hatua za awali za safari yake ya nchini Uingereza.

Kwa mujibu wa Digital Spy Forum, wanaeleza kuwa, Arshavin alipenyezwa kwenye klabu ya Zenith St. Petersburg akiwa kama mwanasoka ambapo lengo kuu lilikuwa kuhakikisha anasajiliwa kwenye moja ya vilabu vikubwa vinayoshiriki ligi kuu ya nchini Uingereza (English Premier League).

Kabla ya kuanza "mission" yake, Arshavin alipewa jina maalumu (Code Name) akiitwa Red Fox. Akiwa Zenith St. Petersburg zikaibuka tetesi kuwa mchezaji huyo anahitajika na klabu ya Barcelona ya nchini Spain, dili hilo likamsukuma kocha wa Arsenal wakati huo, Profesa Arsene Winger kuingilia kati na kumsajili mchezaji huyo. January 31, 2009 alitangazwa rasmi kujiunga na klabu ya Arsenal maarufu kama The Gunners.

Adrew Arshavin alisakata soka ndani ya klabu ya Arsenal katika awamu mbili. Awamu ya kwanza, kuanzia 2009 hadi 2012, kisha achukuliwa kwa mkopo na klabu yake ya zamani ya Zenith St. Petersburg. May 31, 2012, akarejea tena Arsenal, na msimu wa 2013/14 akaondoka rasmi klabuni hapo na kutimkia Zenith St. Petersburg. Inaelezwa kuwa, hii ni baada ya kukamilisha "mission" yake.

Baada ya kuvuja kwa taarifa hii, ikielezwa kwamba hata taarifa za mchezaji huyo kutakiwa na klabu ya Barcelona hazikuwa na ukweli, bali zilitengenezwa tu kama tetesi ili kumpa thamani mchezaji huyo na kuvivutia vilabu vikubwa vya nchini Uingereza.

Taarifa zaidi zinaeleza kwamba, Warusi wenzake, Roman Pavlyuchenko na Pavel Pogrebnyak, ni majasusi wenzake wa Kremlin, nao walitumwa nchini Uingereza kwa majukumu ya kusaidia ujasusi wa Arshavin, na baadaye kumsaidia katika kutoroka kwake.

Hivi karibuni, Shirika la Ujasusi la Uingereza limefanya mawasiliano na Huduma ya Siri ya Ufaransa wakijaribu kuchunguza kama kocha Arsene Wenger wa Arsenal, alikuwa sehemu ya njama za Warusi.

Mwisho.

Imeandikwa na;- Hilal Kanal
Call/Whats;- +255 718 022 322
Dar es Salaam, Tanzania
September 10, 2024View attachment 3095125
Ninchokifahamu mimi usajiri wa huyu jamaa pale Arsenal na mwenzake Pavlyuuchenko pale Tottenham ulitokana na umachachali wa hawa mawinga kwenye mashindano ya EURO 2008 yaliyoiwezesha RUSSIA nadhani kucheza robo fainali.

Arsharvin akitokea pembeni huku Parvulyenko akimaliza nchani pale.
 
Turudi ktk FACTS.

Kipindi hicho kulikuwa na tajiri ROMAN ABRAMOVIC ambaye aliimiliki Chelsea kuanzia 2003, kwanini wasingemtumia MRUSI mwenzao kuweka afisa kipenyo mpaka watumie njia ndefu ya kudanganya Barca wanamuhitaji? Then Arsene wenger akurupuke from no where asajili mtu kisa barca walionyesha nia..

Tujiulize maswali madogo tu... ya maana.
Unauwakika gani kama Abramovic nae sio jasusi wakirusi?
 
Source: Trust me bro.

Lakini haikumsaidia kitu Manchester united ikaitembezea Arsenal kichapo kikali cha kikatili bila huruma na kuichabanga kwa kuigaragaza Arsenyani goli 8-2 na yeye akiwepo
Kwamba licha ya ujasusi wao haukuwasaidia kufurukuta mbele ya maashetani wekundu
 
Ninchokifahamu mimi usajiri wa huyu jamaa pale Arsenal na mwenzake Pavlyuuchenko pale Tottenham ulitokana na umachachali wa hawa mawinga kwenye mashindano ya EURO 2008 yaliyoiwezesha RUSSIA nadhani kucheza robo fainali.

Arsharvin akitokea pembeni huku Parvulyenko akimaliza nchani pale.
Warusi ni hatari dingii
 
Turudi ktk FACTS.

Kipindi hicho kulikuwa na tajiri ROMAN ABRAMOVIC ambaye aliimiliki Chelsea kuanzia 2003, kwanini wasingemtumia MRUSI mwenzao kuweka afisa kipenyo mpaka watumie njia ndefu ya kudanganya Barca wanamuhitaji? Then Arsene wenger akurupuke from no where asajili mtu kisa barca walionyesha nia..

Tujiulize maswali madogo tu... ya maana.
Uwez rahsha ivo ingejulikana mapema kwaiyo walisha waza mapema sana kwaiyo wakatengeneza njia nyingne ambayo waingereza wasingelijua mapema
 
Back
Top Bottom