Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Wanaume wa dar ni waoga hata mende anamkimbia huyu ananiambia anaogopa mauzauza ya malkia wa goshen shang'aa malkia ya goshen ina mauza uza gani
Haahaa hao wanaume mko nao huko Dar?mbona nasikia Dar Wadi za wazazi zinafurika sana mpaka watu wanalala chini?
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA II) -- 20*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Ikapita kama dakika tatu wakiwa hapo. Ila walikuwa wanamtazama Lee si mara moja wala mbili, wala tatu.

Na kuna kitu walikuwa wanateta midomoni mwao kisisikike hata kwa majirani.

ENDELEA

Basi Lee akiwa hapo, hakuwatambua hao watu hata akatoka na kulipia kisha akaenda zake. Lakini wale watu wakatoka nao wakiwa wameacha hata vile walivyoagiza hapo mgahawani. Hao wakaongoza kumfuata Lee kama mkia.

Lee akapanda gari na kuketi akiwa peke yake nyuma kabisa. Alipoketi akachomoa kitabu fulani kilichokuwapo kwenye vijindoo vidogo vijishikavyo ukuta mwa gari, akakunja nne na kukipitia kitabu hiko kilichokuwa na mambo matamu yaliyovutia.

Kilikuwa ni kitabu kilichoonyesha mambo kadhaa kadhaa ya kitalii ndani ya China. Maeneo ya kutembelea na vivutio kadhaa ndani ya nchi hiyo. Milima na mabonde. Uoto na utamaduni. Na pasipo kusahau ukuta ule mkuu 'great wall' wa China.

Lee akavutiwa sana na kitabu hicho, akapanga kutembelea moja ya vivutio vile kwani alikiri kifuani mwake kuwa japo alikuwa yu mchina, hakuwa anajua mambo mengi kuhusu nchi yake, maana amekuwa wa kutembea sana huku na kule.

Hakutulia nchini mwake tangu alipotwaliwa na familia ya Wu, baada ya hapo akasafiri na kwenda kuishi nchi nyingine kabisa, kwa hivyo amekuwa mgeni katika nchi yake. Na ana hamu ya kujua mambo kadhaa zaidi.

Kwa muda akatekwa na hicho kitabu, gari likasonga na kusonga. Alifungua kurasa na kurasa akivutiwa na anachokiona. Hata hakujua kama ndani ya gari lile walipanda wale wanaume watatu ambao kwa namna moja ama nyingine walikuwa wanamzingatia.

Akafika kituoni na kushuka. Akatembea kuelekea jengo fulani lenye urefu wa wastani. Nyuma yake kama hatua kadhaa, wale wanaume nao wakawa wanajongea taratibu kumfuata.

Lee akapapasa mifuko yake, na mara akatoa kiasi fulani mfukoni mwake na kuzama ndani ya duka moja kubwa 'Mi Hao supermarket', humo akapate kutazama baadhi ya mahitaji yake kabla hajarejea nyumbani.

Alipozama humo ndani wale wanaume wakasita kuzama. Wao wakaamua kungoja kwa nje. Lee akazurura taratibu ndani ya duka akipitia shelvu moja baada ya nyingine. Hakuwa na haraka. Hakuwa na ratiba nyingine zaidi ya kurejea nyumbani kupumzika, na kwa namna moja ama nyingine mahali pale palimsahaulisha mawazo yake kwa muda kidogo.

Basi akiwa anautumia muda wake kiasi humo, mara mlinzi aliyekuwa amekaa ndani akatoka nje kwenda kuwakuta wale mabwana kule nje maana aliona wamekaa kwa muda mrefu hapo wasionekane kama wana shughuli yoyote ya maana.

Na kwa kiasi kimoja ama kingine, mwonekano wao ulizua mashaka. Walionekana wahuni. Si watu wa kuamini. Japo mlinzi alikuwa mwembamba asiye na nguvu, akatumia madaraka yake kuwauliza wanaume wale majabali ni nini walikuwa wanafanya hapo.

Basi wakatazamana na kisha mmoja akasema, wanamngoja mwenzao aliyeingia humo ndani na maelezo waliyotoa wakamlenga Lee. Basi mlinzi akaachana nao na yeye akazama ndani.

Moja kwa moja akamwendea Lee na kumuuliza kuhusu hilo. Hapo ndiyo akawa ametibua mambo. Sasa Lee akajua kuna watu. Na kwa kutumia kamera za mapokezi akawaona watu hao. Hakuwa anawatambua. Na kwa kumbukumbu yake hafifu, aliwaona mahali.

Hakujua ni wapi, ila kama aliwaona, aliwaza.

Basi akamaliza kuchukua vitu vyake naye akalipa na kutoka nje, hakuwasemeza wale wanaume. Alitaka kuona kama watahangaika naye. Nao hawakusumbuka. Ila wakaunga nyuma kama mkia.

Lee akatembea akiwa anawaza kichwani mwake namna ya kufanya. Na akiwa anawaza wale watu ni wakina nani. Akaona si busara kwenda nyumbani kwake moja kwa moja. Na hakuwa na haja ya kuwakimbia wale wanaume maana wapo ndani ya uwezo wake kabisa.

Basi akatafuta kichochoro alipozama humo. Ilikuwa ni kaupenyo kadogo kakuongoza kutokezea upande wa pili ambapo huko kuna bahari kwa kama umbali wa hatua hamsini kwa mbele.

Njia ilikuwa nyembamba, na kwa wale wanaume majabali iliwawia vigumu kidogo kupita kwa kujinafasi kama walivyokuwa wakifanya barabarani.

Humo njiani Lee akaona ni mahala pema pa kufanya alichokuwa anawaza kichwani - kuwakabili wale wanaume ambao aliamini kuwa maadui.

Basi akasimama na kuweka vitu vyake kando. Kisha akakung'uta mikono na kugeuka kuwatazama wale wanaume ambao nao walisimama punde Lee alipofanya hivyo.

Akawauliza wao ni wakina nani na kwanini wamfuata. Wanaume wale kwa kebehi wakamwambia kabla hawajamfuata, yeye ndiye aliyewafuata. Lee akashangaa.

Hakuwa anataka kusumbuka sana, akawauliza wanataka nini toka kwake. Wale wanaume wakasema wana maongezi naye, na kama hatojali basi aongozane nao kwenda huko wanapomtaka kuteta.

Lee akasita. Vipi kama watu hawa wanatafuta mahali pa kummalizia? Kama kweli walikuwa na hitaji basi ni kwanini walikuwa wakimfuata kimya kimya hivyo? Akakataa, akema kama wana hitaji basi walieleze hapo hapo na si vinginevyo.

Wale wanaume wakatazamana. Na basi akasema kama hakuwa anahitaji kwenda kwa hiyari, basi watamlazimu maana wametumwa vivyo.

Wakamfuata wakitaka kumnyakua, lakini Lee akajiandaa kwa mapambano. Akajiweka sawa na kuanza kupambana. Alikuwa mwepesi kukwepa na kuutupa mwili tofauti na maadui zake.

Japo ilikuwa pevu, akaimudu ndani ya dakika kadhaa. Alikuwa amechoka kwani wale majamaa walikuwa majabali haswa kwa hivyo kuwalaza chini wakiwa hawajiwezi, haikuwa kazi rahisi hata kidogo.

Akakusanya vitu vyake na kuondoka. Ikiwa hakuonekana na yeyote yule zaidi ya wale waliobakia hoi sakafuni.

**

"We are already here!" Sauti ilivuma garini. Lilikuwa ni gari refu jeusi, Limousine. Dereva akashuka na kwenda kufungua mlango wa nyuma, akatoka mwanaume mfupi mchina aliyevalia suti nyeusi. Mkononi mwake alikuwa ana sigara kubwa iliyokuwa inafuka moshi mwingi. Na macho yake yalikuwa yamefunikwa na miwani meusi.

Mwanaume huyo akavua miwani na kuangaza huku na huko. Mara akawaona wale wanaume majabali wanne wakiwa wanajikongoja kuja garini. Mwanaume huyo ndani ya suti akawatazama kwa uso wa ghafira, alafu akaingia ndani ya gari na kutulia.

Wale wanaume nao wakaingia na kisha gari likahepa wasipate hata kuongea. Kwa muda kukawa kimya.

Baada ya muda wa dakika kadhaa humo katika gari hilo la kifahari, mwanaume yule jabali mwenye rangi nyeusi, akamtazama yule bwana aliyekuja kuwachukua, akamsihi mambo hayakuwa kama vile walivyotaraji.

Lakini yule bwana hakujali. Mdomo wake aliutumia kuvuta sigara badala ya kuteta. Alikuwa 'bize' uso wake ukitazama mbele, na ubaya miwani yake iliyokuwa imeficha macho, haukutuonyesha wapi au nani anamtazama.

Hatukupata uhakika kilichoendelea maana baada ya dakika kadhaa hivi, limousine hiyo ikazama ndani ya jengo moja refu hapo Hongkong, likaendea eneo la maegesho ya gari.

Lakini kitu pekee ambacho tulikuja kupata hakika nacho ni kuwa, wale mabwana, majabali waliogaragazwa na Lee, waliuawa na maiti zao zikafungiwa mawe makubwa na kutupiwa baharini!

Aliyesalimika akawa ni mmoja tu, yule bwana mweusi. Naye usiku akajikuta kitandani akiwa amefunikwa mdomo wake na karatasi pana. Akainyofoa akilalama kwa maumivu makali.

Na kwenye ile karatasi kulikuwa kuna ujumbe ulioandikwa kwa wino mweusi kwa lugha ya kichina ukimtaka ahakikishe anampata Lee ndani ya siku mbili tu, la sivyo maisha yake yatakuwa katika rehani kubwa.


**

Alipoweka glasi yake ndefu mezani, akakohoa kidogo kisha akamtazama Miranda aliyekuwa amekaa kando. Akamuuliza;

"How is he now?" (Anaendeleaje sasa?)

Miranda akanywa kwanza naye kinywaji chake glasini. Ulikuwa ni mvinyo mwekundu. Akagida mafundo matatu, alafu akamtazama Bwana Brown almaarufu, BC, ambaye kama kawaida yake alikuwa ndani ya suti tamu iliyomkaa mwilini. Mguu ameukunja nne, na vidoleni amebebelea sigara kubwa.

"He is still far from being ok," (Bado hayuko sawa,) Miranda akasema kwa vuli la huzuni, alafu akashusha pumzi ndefu na kuufumbata mdomo wake.

"We have to get the cure, otherwise he will die in our hands," (inabidi tupate tiba, vinginevyo atafia mikononi mwetu,) Miranda alisema akiwa anamtazama BC kwa kina.

Kukawa kimya kidogo. Wakinywa na pia BC akivuta sigara yake. Baada ya muda kidogo, BC akaulizia kuhusu antidote iliyoletwa na kijana aliyemfahamu kwa jina la Marwa.

Alipata kumwona kijana huyo hapo kwa Miranda na kisha akatambulishwa kama mkazi wa eneo moja na Jona.

"That antidote makes things worse! He almost died the last time I gave it to him!" (Antidote huaribu mambo kabisa! alikaribia kuca nilipompatia mara ya mwisho!") Miranda alitema cheche. Basi BC akanyamaza kidogo. Na kama ilivyo hulka yake akiwa mawazoni, akawa anavuta sana sigara kuliko kunywa.

Kwa hivyo, Miranda akanyamaza akingojea jibu maana alikuwa ana uhakika bwana huyo atateta baada ya muda fulani.

Hakuwa amekosea, baada ya muda BC akafungua mdomo wake mkavu kuteta. Akamwambia Miranda, Bwana Sheng atakuwa ametambua kuwa Marwa alikuwa na antidote hivyo akabadili virusi vya kumtilia mwilini.

Basi wasihangaike sana, yeye anahitaji kiasi kidogo cha mate ya Jona, akienda nyumbani kwake ayafanyie utaratibu wa kuyapembua kwenye maabara yake binafsi wajue cha kufanya.

"I am sure, after two days he will be dead if he wont be taking antidote." (Nina uhakika baada ya siku mbili atakufa kama hatakuwa anatumia antidote.) Bwana BC akateta. Na huu ulikuwa ukweli mtupu mana Jona alikuwa amekwisha mno, hajiwezi kitandani.

Kama ungelikuwa na roho nyepesi, machozi yangalikutoka ukimwona.

Na basi kwa uzito wa swala hilo, hata ule mvinyo aliokuwa anakunywa Miranda hakuwa unasuuza koo lake kabisa. Hakuufurahia maana kichwa chake kilikuwa kimetingwa na mawazo lukuki.

Basi wasipoteze muda hapo, ndani ya muda mfupi baada ya BC kumaliza sigara yake, Miranda akapata mate ya Jona kwenye kijifaa kidogo cha chupa, na haikuwa ngumu kwake kupata mate hayo kwani Jona alikuwa akiyatiririsha ya kutosha.

Akamkabidhi BC na bwana huyo akaondoka zake.

**

"Nadhani amelala sasa," alisema Marwa akirudishia mlango wa chumba alicholazwa Jona. Mbele yake alikuwa amesimama Miranda akiwa amekumbatia mikono yake, ametazama chini akizimeza lips zake.

Alikuwa amesimama hapo koridoni maana hakuwa anataka kwenda kumtazama Jona chumbani akihofia kusononeka moyo. Kila alipomwona Jona macho yake yalibadilika rangi kuwa mekundu, na akihisi moyo wamuuma haswa.

Baada ya kupewa taarifa taarifa hiyo na Marwa, wakaongozana kwenda sebuleni. Na punde alipoketi, simu yake ikaita. Alikuwa ni BC. Akapokea na kuiminyia simu sikioni.

"I have never seen such a virus like this before!" (Sijawahi kuona kirusi kama hiki hapo kabla!) Sauti ya BC ilinguruma simuni. Miranda akabana pumzi kwa mshangao. Moyo wake ulianza kwenda mbio.

Akauliza kwa hofu, "So what shall we do??" (Sasa tutafanya nini??)


***
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…