Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Hii jamiiforums version ya simu yangu itakuwa out of date
Mbona sioni posts mpya au bando au mkuu jona bado hajapona [emoji27] [emoji27]
 
Hii jamiiforums version ya simu yangu itakuwa out of date
Mbona sioni posts mpya au bando au mkuu jona bado hajapona [emoji27] [emoji27]
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 25*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Wakatazama huku na kule, hawakumwona mtu zaidi ya Chong Pyong aliyekuwa amelala chini akihema kama bata. Kutazama dirishani, wakaona li wazi, Lee alikuwa ametoroka kwa kutumia shuka!

ENDELEA

Yule jabali mweusi akaghafirika akipiga ngumi kiganja chake. Haraka akaamuru wenzake washuke kule chini kumtafuta mwanaume huyo wakati yeye akiwa amebaki na Chong Pyong ndani ya chumba.

Akamuuliza Chong Pyong maswali kadhaa. Ma maelezo yake yakazidi kumtia Lee hatiani na kuthibitisha kuwa si mtu wa kubaki hai hata kidogo.

Lazima auawe! Maana tayari atakuwa amefahamu siri yao kuwa Chen Zi aliuawa na si kuzidisha madawa kama vile watu wadhaniavyo.

Lakini pia, wakammaliza na Chong Pyong kwa usalama zaidi. Waliona endapo mtu huyo akiendelea kuwa hai, basi Lee atamtafuta na kupata kila anachokitaka. Kitu ambacho hawakuwa radhi kitokee, hata kidogo!

Yule jabali mweusi baada ya kutimiza agizo la mkuu wake, kummaliza Chong Pyong, akaamriwa aende polisi na kuripoti hilo tukio katika namna ambayo Lee ataonekana kuwa mtuhumiwa wa mauaji hayo tangu amekuwa mkazi wa hilo eneo ambapo Chong amefia.

Jabali hilo likatii na kufanya kama alivyoagizwa. Ndani ya muda mfupi, polisi wakafika eneo la tukio, wakapiga picha kadhaa, wakachukua maelezo toka kwa Jabali yule mweusi kama shahidi, kisha wakaondoka na mwili wa Chong Pyong.

Na kwa msaasa wa kamera za CCTV, zilizokuwako maeneo ya koridoni na huko nje, polisi wakapata picha ya Lee iwasaidie kwenye msako.

**

Saa mbili asubuhi ...

"Vipi? Unaendeleaje?" Marwa alimuuliza Jona aliyekuwapo kitandani akitazama kana kwamba mtu aumizwaye na mwanga mkali.

Ndani ya chumba walikuwa wenyewe tu, na tayari Marwa alikuwa amembembelezea chai mgonjwa na kufanikiwa kwa kiasi chake. Alikula kidogo akasema ameridhika.

Kabla Jona hajajibu, alimtazama Marwa kisha akafumba macho yake kwanguvu kama mtu auguliaye maumivu, alafu akasema kwa kunong'ona:

"Naendelea vizuri."

Mdomo wake ulikuwa mkavu. Macho yake madhaifu yalikuwa yamezungukwa na duara jeusi kwa mbali. Uso wake ulikuwa umekonda na kudhoofika.

"Nipo wapi hapa?" Akauliza akijitahidi kuchanua macho yake. Ila akashindwa. Haraka akayaminya na kuyafumba.

Marwa akamwambia, "Upo kwa Miranda. Unamkumbuka?"

Jona akakunja ndita kwa mbali, alafu akauliza, "Miranda?"

"Ndio, Miranda," Marwa akamjibu akimtazama na tabasamu kwa mbali. Jona hakusema tena, akanyamaza.

Marwa akamtazama kwa muda. Kisha akarudia tena swali, "unamkumbuka?"

Jona akabaki kimya. Ni kama vile alikuwa amepitiwa na usingizi. Marwa akaondoa vyombo na kumwacha peke yake. Ila muda kidogo akarudi na kumtazama. Bado Jona hakuonyesha dalili ya kuamka.

Akaketi kitandani na kuendelea kumtazama kwa muda wa dakika tano, akasikia hodi mlangoni na sauti ya kike. Alikuwa ni Miranda. Akanyanyuka kwenda kukutana naye.

"Vipi hali yake?" Akauliza mwanamke huyo. Marwa akageuza uso kumtazama Jona, kisha akatoka ndani ya chumba na kukifunga.

"Angalau," akajibu akipandisha mabega. "Ameweza kuongea leo, japo kwa muda mchache ... ile antidote imemsaidia!"

Marwa akatabasamu kwa mbali, ila Miranda akatazama chini. Marwa akamuuliza, "Vipi?"

Miranda akatikisa kichwa kisha akaongoza mpaka sebuleni. Wakaketi.

"Ile si antidote ya kumpatia," Miranda akasema kisha akalaza kichwa chake kitini. "Itampa ahueni kwa sasa, kwa kitambo kidogo, ila inabidi atafutiwe antidote ya kudumu. Endapo akiendelea kutumia hii ya sasa, ataishi kupooza mwili."

Marwa akatoa macho kwa mshangao.

"Mbona hukuniambia mapema?"

Miranda akamtazama. "Ingesaidia nini?" Akauliza. Kisha kama mtu aliyejishtukia aidha atakuwa amemkwaza Marwa, akashusha pumzi yake na kunyanyua mkono.

"I am sorry. I didn't mean to be that rude."

"Usijali," Marwa akamtoa hofu. "I understand. It's ok."

"Inabidi tutafute antidote halisi," Miranda akasema. Ila uso wake haukuwa na lepe la matumaini. "Tusipofanya hivyo, tutatibu tatizo moja kwa kuleta jingine."

"Tutaitafutia wapi sasa?" Marwa akauliza. Mara simu ya Miranda ikaita. Kutazama alikuwa ni BC.

**

Saa nne asubuhi ...

BC alichomoa leso yake mfukoni akijifikicha pua. Mafua yalikuwa yanamsumbua. Aliporudisha leso yake mfukoni akanywa fundo moja kubwa la whisky kisha akamtazama Miranda na Marwa waliokuwa wameketi pembezoni mwake.

Walikuwa wapo nje ya nyumba ya bwana huyo wa kizungu. Meza mbili zilikuwa mbele yao, ila ya Bwana BC pekee ndiyo ikiwa na kinywaji. Wote walikuwa kimya wakimtazama bwana huyo wa kizungu kwa hamu.

BC akawatazama kisha akapooza koo lake kwa kunguruma. Akalaza mgongo wake kwenye kiti kidogo cha chuma alichokalia, na kusema kwa sauti kakamavu:

"We have to prepare for any risk so far. To get the actual antidote won't be an easy task at all!" (Inabidi tujiandae kwa hatari yoyote. Kupata antidote halisi haitakuwa kazi ndogo kabisa!)

Miranda na Marwa wakaendelea kumtazama kwa umakini. Na sura zao hazikuonyesha kama watu wanaohofia hatari hizo. Bali wana kiu na kupambana nazo. Na Bwana BC aliliona hilo.

Akanywa fundo moja tena la whisky na kuwaambia haswa lengo lake la kuwaitia hapo.

"Did you hear about that Chinese ship?" (Mmesikia kuhusu ile meli ya wachina?) Kabla hajajibiwa, akasema, "for sure, it might have brought something huge. And I fear, amongst them, is what we need." (Kwa uhakika, itakuwa imeleta kitu kikubwa. Na nadhani, miongoni mwavyo ni kile tunachokohitaji.)

Akaweka kituo akitazama chupa yake ya kinywaji chake. Akafikiri kidogo na kuwataka Miranda na Marwa wafanye jambo kuhusu kile kitakachokuwa kimeletwa na ile meli. Kama kutakuwa na namna ya kuingia ndani ya kambi ya Sheng na kisha kupekua.

"Though it is risky. It worths it." (Japo ni hatari. Ina manufaa.)

Lakini vipi kama hawataikuta antidote huko? Akauliza Miranda.

"Then you will surely see something else!" (Basi kwa hakika mtaona kitu kingine!) Akajibu BC. Na kuongezea, "and it will be equally important!" (Na kitakuwa na umuhimu sawa!)

Lakini pia akawaambia kama njia hiyo haitafanikiwa, basi atawaeleza plan B. Na kwasababu plan A itakuwa haijafanikiwa, basi Plan B itakuwa ndiyo njia pekee iliyobaki na kwa namna yoyote ile iliyopo duniani, lazima itimie!

**

Saa nne usiku ...

"Una hofu?" Miranda aliuliza akimtazama Marwa. Mwanaume huyo alikuwa ameketi kwenye kiti nje ya nyumba akiwa anafikiri na kuyajenga kichwani.

Akamtazama Miranda na kutikisa kichwa. "Hapana, nipo ok." Ila uso wake ulimsaliti. Alikuwa na hofu. Na tumbo lake lilikuwa linauguza woga.

Miranda akamsogelea na kuketi karibu yake. Akamwambia, "usijali. It will be ok. Hatutakufa. Tutafanikiwa kutoka hai na salama."

Lakini kumbukumbu ya Marwa eneo lile haikuwa nzuri. Mara ya mwisho almanusura apate ukilema. Na ni ustadi tu wa Jona ndiyo uliowatoa hai. Hakuwa anaamini kama yeye na Miranda wataweza mudu.

Miranda akatambua shaka lake hilo.

"Unadhani siwezi kukulinda?" Akamuuliza akitabasamu.

Marwa naye akatabasamu, kisha akatazama chini.

"Hapana. Si hivyo."

Miranda hakusema kitu. Akamgusa mgongoni na kumtaka akajiandae kwani muda umeshafika.

Baada ya muda kidogo wakawa tayari wakiwa wamevalia sweta nyeusi zinazobana, suruali nyeusi za kombati na buti. Miranda akajiweka kwenye gari. Ila Marwa akaenda kwanza kumuaga Jona.

Akamtazama kwa sekunde kama tatu. Hakuonekana kama ana fahamu. Akaketi kitandani na kumshika mkono wake. Akamuita, "Jona." Kisha akasema kwa sauti ya chini, "nakuacha kidogo. Mungu akijaalia tutaonana, tukiwa na dawa mkononi."

Alipomaliza kusema hayo akaendelea kumtazama Jona kwa muda kidogo. Mlango ukagongwa.

"Twende, Marwa!"


**
 
Ahsante mkuu, nahisi plan "B" ya BC ni kumteka sheng aonyeshe dawa [emoji23][emoji23][emoji23]hisia zangu nazijua mwenyewe
 
Plan B najaribu kuwaza sijui watamteka nani? Kisa cha sheng kinazidi kuwa kitamu Nimekuwa interested mno kujua kutakacho endelea,
Team popo [emoji111]nasubiri saa5 [emoji91] [emoji91]
 
Ankoo Stive.. kama upo jirani na duka la Mangi mwambie akupe Pepsi Ya bariid upooze koo kdogo, nitalipa sawa eh
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…