Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Daah asee ila Steve chonde usimuue Marwa manake ntaumia kweli,,yan hii story kuna sehemu nasoma huku nmeshika moyo roho inauma utafhani ni reality looh,,
Wewe solder gani muoga hivyo?
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 30*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

BC akatikisa kichwa na kusema, "No! Maybe it's somewhere more dangerous than there." (Hapana! Labda ni mahali hatari zaidi kuliko kule.)

Marwa akamaliza mate.

"Where is it?" (Ni wapi huko?) Akauliza.

BC akatazamana na Miranda.

ENDELEA

Kisha wakacheka. Miranda akamtoa hofu Marwa.

"Anakutania tu. Kuna mahali panapotisha kuliko pa Sheng?"

"Ni wapi huko anasemea?" Marwa akauliza kwa uso 'serious'. Miranda akatasabamu kwanza, kisha akamwambia, "ni MSD. Medical Store Department."

"Ghala la dawa la serikali?" Marwa akatahamaki.

"Ndio," Miranda akamjibu. "Huko ndiko tutapata mojawapo ya dawa tunayoihitaji ili tuichanganye na hii kumtibu Jona."

Marwa akatulia. Napo haikuwa rahisi.

"Kama tusipofanikiwa kukipata hiko kitu, basi mambo yatakuwa magumu zaidi. Itatulazimu twende ughaibuni."

"Sawa," Marwa akatikisa kichwa. "Ni lini tutaenda?"

"Leo usiku," Miranda akamjibu. "Hatuna muda wa kupoteza, Marwa. Unaona hali ya Jona ilivyo. Sio?"

Marwa akaafiki. Wakateta kidogo, baada ya muda wakarudi tena kwenye mada yao, mara hii BC akiongea kwa msisitizo.

Akasema punde dawa hiyo atakapoitengeneza, basi ataitoa kwa awamu na kwa masharti. Anataka kujua kama Jona atakuwa upande wake ama lah! Anahofia kuhangaika 'for nothing'.

"You two must make sure, he allies. It is the only thing I can afford to hear." (Ninyi wawili lazima mhakikishe, anashirikiana. Ni kitu pekee ninachotaka kukisikia.)

Miranda akatazamana na Marwa, kisha akarudisha uso wake kwa BC. Akamhakikishia kila jambo litaenda sawa. Hakuna la kutilia shaka. Kwa sasa wazingatie kumkomboa Jona, na kila kijacho kitaangukia panapostahili.

BC akaafiki akitoa onyo. Hakukaa tena sana, akaaga na kwenda zake.

**

"Chai ipo tayari, nakwambia kwa mara nyingine. N'kuletee?" Akauliza Kinoo kwa uso wa kughafirika. Macho yake yalikuwa yanamtazama Sarah aliyejilaza kitandani.

Ni robo saa sasa tangu amwambia mwanamke huyo kuwa chai ipo mezani, na wala hajasogeza msuli wake hata mmoja. Chai inaelekea kupoa sasa ingali iliandaliwa kwa haraka baada ya mwanamke huyo kulalama njaa.

"Nimeshakusikia," Sarah akajibu kwa kujivuta. Na badala ya kuamka aende, akajigeuzia upande wa pili.

Kinoo akatikisa kichwa. Kifuani mwake alijawa na hasira. Aliondoka akaenda zake sebuleni alipoketi na kutazama chai iliyokuwepo mezani. Chapati, mayai manne ya kuchemshwa, soseji tatu, chai ya maziwa.

Kikombe cha chai hakikuwa kikifuka moshi tena.

Akasonya. "Tabu zingine bana," akalalama. Akashika tama akiendelea kungoja. Alichoshwa na hizi kero za mwanamke wake, ila hakuweza kuchukua hatua hata moja.

Lakini cha ziada, hakujua Sarah anateswa pia na msongo wa mawazo juu ya dada yake, Sasha. Alikuwa yu njia panda ya kuchagua aidha asimame na ndugu yake wa damu ama mpenzi, baba wa mtoto wake. Mambo haya yalikuwa magumu. Na hakuweza kuomba ushauri.

Baada ya muda kusonga, mtu hatoki chumbani, Kinoo akakomba vitu vyake mezani na kuvipeleka jikoni. Akavitumbukiza ndani ya 'microwave' na kuvipasha huku chai akiinywa kama maji.

Baada ya dakika kadhaa, akavitoa na chai akamimina nyingine, ya moto, alafu akaongozana na vyakula hivyo, vikiwa kwenye trey, mpaka chumbani. Akaviweka kando ya Sarah na kumtaka aamke ale.

"Kinoo, sijisikii kula."

"Unamaana gani hujisikii kula?"

"Nahisi tumbo limejaa."

"Kwa kitu gani na hujala?"

Sarah akanyanyuka na kuketi kitako. Akamtazama Kinoo.

"Muda si mrefu nitakuwa na ugeni. Sasha anakuja. Nadhani nitakula naye."

Kabla Kinoo hajafunua mdomo wake, hodi ikagongwa huko nje. Wakatazamana na Sarah kisha asiongee kitu, akanyanyuka kuendea mlangoni. Alikuwa ni Sasha. Alivalia blauzi ya zambarau na suruali ya jeans rangi ya bluu iliyokolea rangi.

Akamsalimu na kumkaribisha ndani. Akaketi sebuleni. Punde Sarah akatoka chumbani na kukutana naye. Walikumbatiana na muda si mrefu wakajumuika kwenye kunywa chai.

Kinoo akawapa faragha kwa kuaga anaenda dukani.

"Anakujali sana unh?" Sasha aliuliza kimbea punde Kinoo alipofunga mlango na kupiga hatua kama nne hivi akijiendea.

Sarah akatabasamu na kuguna. "Kwakweli. Namchosha sana. Ila huu ndiyo muda wa kumsumbua."

Wakacheka.

"Hongera sana," Sasha akampongeza. "Wenzako hawapati bahati kama hii!"

Wakateta maongezi hayo kwa muda wa kama dakika tatu, kisha Sasha akaanza kuelekea kwenye lengo lililomleta hapo.

"Vipi? Mmefikia wapi kwenye lile swala? Jamaa amefanikisha?"

"Hapana," Sarah akajibu akitikisa kichwa. "Ameniambia mazingira bado hayajatulia."

"Mazingira yapi hayo?"

"Sasha, sifahamu. Muda mwingine akinijibu kama hivyo, nashindwa kuendelea kuuliza sana."

"Hapana, Sarah!" Sasha akapiga kofi paja lake la kulia. "Unajua nakutegemea wewe. Unataka nife, eti? Upo kwenye nafasi nzuri sana ya kumshawishi. Najua hatotaka kukuudhi ukiwa kwenye hali kama hii."

Sarah akatikisa kichwa. "Unajua si kazi nyepesi kabisa, sister. Inabidi ufahamu kuwa nikimuuliza sana ama kumshawishi sana, anaweza akahisi kuna jambo. Hufikirii hilo?"

"Hamna. Unatumia tu akili, Sarah. Laiti, kama isingelikuwa kule makaoni kuna jambo wanalishughulikia kwa sasa, nisingelikuwa hai. Wangeshanimaliza maana muda wangu wa kufanya nililoagizwa, umeshakwisha."

Sasha akamshika mkono Sarah.

"Maisha yangu yapo mikononi mwako. Know that. Wewe niingize tu nami nitajua namna ya kuenenda ... na na kuhusu Kinoo, nitafanya kadiri ya uwezo wangu kumweka salama."

Mara mlango ukafunguliwa akaingia Kinoo. Wakashtuka, ila hawakuteta. Kinoo akapitiliza kwenda chumbani.

"Unadhani anaweza akawa amesikia?" Sarah akauliza akinong'ona.

"Hapana," Sasha akajibu. "Tulikuwa tunaongea kwa sauti ya chini. Hawezi akawa amesikia."

"Una uhakika?"

"Ndio. Sasa mimi naomba niondoke, tutawasiliana baadae. Ila nakuachia kazi moja, unajua hatujamaliza maongezi yetu, ila hatuna budi kuyakatisha. Mpeleleze na unambie ni nini sasa hivi wanahangaika nacho?"

"Unamaanisha nini?"

Sasha akatazama mlango wa chumbani kisha akarudisha macho yake kwa dadaye.

"Nataka kujua wanahangaikia kitu gani sasa hivi. Lazima kitakuwapo, kimoja ama viwili. Ukivijua, nijuze upesi. Sawa?"

Sarah hakujibu, Sasha akasimama na kusema kwa sauti. "Niitie basi shemeji nimuage!"

Sarah akapaza sauti kumwita Kinoo, akafika na Sasha akamuaga, akaenda zake.

"Sarah," Kinoo akaita muda mfupi baada ya kuketi kitini wakitoka kumsindikiza Sasha. Sarah moyo ukampwita. Alihofu.

"Kuna kitu unanificha?" Kinoo akauliza. Moyo wa Sarah ukazidi kwenda mbio. Vidole vyake navyo vilianza kutetemeka.

"Kitu gani nikufiche, Kinoo?" Akauliza akikunja shingo. "Kwanini unawaza hivyo?"

Kinoo akamtazama Sarah ndani ya kiini cha macho yake kwa sekunde tano asiseme jambo, kisha akanyanyuka na kwenda zake chumbani. Akamwacha Sarah akiwa na mawazo lukuki kichwani.

Akahisi pengine mwanaume huyo amesikia kile walichokuwa wanaongea. Habari hiyo ikamtisha. Ikamfanya ahofie hata kwenda huko chumbani kukutana naye.

**

Saa tatu usiku ...

"Hatuna muda wa kuzubaisha mambo," alisema Miranda. Walikuwa ndani ya gari pamoja na Marwa. Gari hili lilikuwa dogo, Toyota IST rangi nyeusi.

"Tunachotakiwa kukifanya ni kufika hapa," akaonyeshea kidole kwenye ramani kubwa aliyoiweka mapajani. "Tutapita njia hii, ni fupi zaidi. Walinzi wapo wanne tu, na hupendelea kukaa maeneo haya ..." Miranda akaonyeshea kidole maeneo matatu kwenye ramani.

"Na kama ikitokea dharura, basi tutatokea kwa njia ya huku kusini. Ni njia ndefu, ila ina uhakika wa kutoka nje baada ya kukwea makontena yaliyokaribu na kuta."

Kabla hawajatoka, wakavalia barakoa kuficha sura.

Lakini waliposonga muda mchache baada ya kutoka kwenye gari waliloliegesha umbali wa kilomita kadhaa toka eneo la tukio, mara likafika gari moja lililotembea kwa mwendo mdogo na kukoma. Halikuwa limewashwa taa.

Gari hili lilikuwa ni Nissan Patrol rangi nyeupe. Vioo vyake vilikuwa vyeusi usiweze kuona ndani. Punde gari hilo likazimwa na mwanaume mmoja akatoka ndani.

Akalisogelea lile gari lililowaleta Miranda na Marwa.

**
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 31*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Gari hili lilikuwa ni Nissan Patrol rangi nyeupe. Vioo vyake vilikuwa vyeusi usiweze kuona ndani. Punde gari hilo likazimwa na mwanaume mmoja akatoka ndani.

Akalisogelea lile gari lililowaleta Miranda na Marwa.

ENDELEA

Akalikagua na kisha akarudi kwenye ile Nissan Patrol waliyokuja nayo. Ndani ya muda mfupi wakashuka wanaume wanne, wote walikuwa wamevalia nguo nyeusi kuanzia juu mpaka chini. Nyuso zao hazikuwa za kuvutia, bali kutisha.

Walikuwa na miili mipana wakionyesha waja wa shari. Na wasiwe na papara, wakaegemea gari lao na kungoja kwanza muda. Mmoja wao, ambaye alikuwa dereva, akatoa simu mfukoni na kupiga.

Ikaita mara mbili kabla haijapokelewa.

"Yes, boss. Tumewakuta ... ndio, sawa ... tutahakikisha hatufanyi makosa."

Kisha akakata simu na kuidumbukiza mfukoni. Alikuwa ni nani huyo aliyeongea naye? Najua bila shaka unadhani ni Sheng. Hujakosea. Ndiye yeye, lakini alijuaje 'move' hii ya Miranda na BC?

Turudi nyuma kidogo, si mbali sana, bali usiku wa kuamkia leo.

Baada ya taarifa kufika kwake kuwa wamevamiwa, watu kadhaa wameuawa na pia kusababisha hasara kubwa, Sheng hakufurahishwa kabisa na hili. Alikuwa mwekundu kwa hasira, na kwa mkono wake wa kulia akawamiminia risasi wanaume kumi waliokuwa wanahusika na lindo.

Ilikuwa awamalizs wote ila jamaa yake akamsihi asifanye hivyo maana itakuwa hasira ya samaki kujitumbukiza mtegoni. Atamaliza nguvu kazi ambayo bado ingemea matunda.

Lakini haikuwa rahisi hata kidogo kwa Sheng kuwabakizia uhai. Ilibidi mawazo mbadaka yatumike kumshawishi kwamba bado adui anaweza kutiwa mkononi. Hajatokomea kama alivyowaza.

Kwa kuwa, maadui hao waliowavamia waliiba chemical ndani ya maabara basi ni wazi watakuwa washirika wa Jona wakihaha kumtafutia ahueni. Kwahiyo, moja, Jona yu hai.

Na basi kama watu hao watakuwa wana ujuzi wa kemia, watatambua kuwa chemical waliyoichukua, haitakuwa suluhisho, bali kipande chake. Kwa hivyo, watataka kukamilisha antidote. Hapo watatafuta kipande kilichokosekana.

Na kwa mawazo ya haraka, sehemu ya kuipata ni MSD. Watege hapo, watawakamata wahitaji wao. Watu waliowatia hasara kubwa. Watu watakaowasaidia kumpata Jona na kummaliza 'for good'.

Ila likatoka onyo toka kwenye kinywa cha Sheng. Kama mpango huo hautafanikiwa, kama mpango huo hautamea matunda, basi atamwaga damu za wale wote aliotaka kuwamaliza pasi na simile.

Hivyo, ndiye wewe uliyetumwa hapa kuhakikisha unafanikisha kazi, ukitambua kuwa roho yako ipo rehani, utafanya mzaha?

"Itawachukua kama dakika tano tu kufika mahali wanapopataka," alisema Dereva akitazama saa yake ya mkononi. "Kwa makadirio mepesi, baada ya dakika ishirini, inabidi tujiandae. Haijalishi watatokea wapi, ila lazima watarejea kwenye chombo chao cha usafiri."

Huyo dereva aliponyamaza, alimtazama mmoja wa jamaa aliongozana nao, pasipo kusema neno, jamaa huyo akafungua mlango na kutoa begi jeusi, ndani yake akatoa kifaa fulani cheusi chenye umbo la duara.

Akasonga karibu na gari la wakina Miranda, akalala chini na kupachika kifaa hicho uvunguni. Alafu akakibonyeza tip! ... tip! Ikasikika sauti kama ya kitu kinachozunguka kwa kasi, kisha ikanyamaza.

Jamaa huyo akanyanyuka na kurejea garini. Yule dereva akanyoosha mkono wake ndani ya gari, akatoa kifaa kipana mithili ya tablet. Akakibofya bofya mara tatu, mara kiooni ikaonekana ramani, na mahali pale palipokuwa gari la wakina Miranda.

Kumbe walikuwa wameliwekea 'tracking chip'. Sasa hata gari hilo litakapoenda popote pale wataliona na kulifuatilia vema.

Ikapita muda kidogo wakakwea gari lao na kusogea mbali kidogo na hilo eneo.


**

Ndani ya Bohari ...

Miranda akatoa ishara ya mkono, Marwa akasimama upesi akimtazama kwa umakini. Mwanamke huyo akachungulia, akaona mwanaume mmoja aliyevalia ovaroli la bluu na kofia, akikatiza.

Mwanaume huyo alipoyoyoma, Miranda akampa ishara Marwa, wakaendelea kutembea.

Majengo haya yanayohifadhi dawa, yalikuwa yamepangwa katika mistari kana kwamba bweni. Na kila jengo lilikuwa lina milango miwili, mmoja mbele, mmoja nyuma.

Miranda alikuwa anafahamu ni jengo gani wanaliendea, walishayavuka mawili, na lile moja kabla ya la mwisho ndilo alilokuwa analitaka.

Basi wakaendelea kunyata. Walikuwa makini maana si tu walinzi ndiyo waliokuwepo humo, bali pia na baadhi ya wafanyakazi, ambao wengi wao walikuwa wamevalia ovaroli na kinyago cha kuziba pua na mdomo.

Hawakuwa wengi, ila kikwazo kikubwa kilikuwa ni mataa yaliyokuwa yanamulika huku na kule. Mataa makubwa yenye nguvu ya mwanga.

"Tutaingia mule ndani," alisema Miranda akinyooshea kidole jengo la mbele. "Nadhani unajua cha kufanya. Kama kawaida, hatuna muda wa kuchomesha!"

Miranda akachungulia tena, njia ilikuwa nyeupe, akachoropoka haraka akitembea asitoe kelele. Alipofika jengoni, akatazama nyuma. Alikuwa amemwacha Marwa. Upesi akampa ishara ya kumtaka aje.

Marwa akachungulia, kulikuwa shwari. Akatoka mbio, ila akiwa katikati, akajikwaa na kudondoka chini. Akaguna kwanguvu kwa maumivu maana alidondokea sakafuni.

Kishindo chake na sauti ya kugugumia, ikamshtua mmoja wa wafanyakazi wa Bohari aliyekuwa amesimama kwa mbali, akiwa kwenye bomba akinawa mikono yake.

Akatazama na kumwona Marwa akijinyanyua. Akapata shaka. Uso wa Marwa ulikuwa umefunikwa na barakoa. Na hata nguo alizokuwa amevaa, hazikuwa zile za walinzi wala wafanyakazi.

Basi akasonga karibu na lile jengo, akibeba kila tahadhari pamoja naye. Aliposimamisha masikio yake, akasikia lango likifunguliwa, na pia sauti ya watu wawili wakinong'ona.

Akapata shaka zaidi. Kwa hofu, asije jitia hatarini zaidi, akachomoka mpaka kwenye kibanda cha walinzi akatoa taarifa kuwa kule ameona wezi, wamevalia barakoa na nguo nyeusi. Wanazama ndani ya ghala pili toka mwisho!

Ndani ya kibanda hicho cha walinzi, kulikuwa kuna walinzi takribani watatu. Mmoja mwanamke. Mezani kwao kulikuwa kuna bunduki mbili kubwa kuukuu, daftari na virungu viwili.

"Wana silaha?" Akauliza mlinzi akitoa macho kana kwamba pera.

"Niliyemwona mikono yake ni tupu," akasema yule mfanyakazi, na pasi kupoteza muda, wakatoka walinzi wawili waliobebelea silaha, wakaongozana na bwana yule aliyewaletea silaha.

Wakasonga mpaka eneoni.

Walipofika wakanyamaza na kutumikisha masikio yao. Hawakusikia jambo. Wakatazama mlango, ulikuwa umetenguliwa kufuli. Hapa wakaamini wamevamiwa.

Basi wakatumia mafunzo yao ya kijeshi, wakazama ndani ya jengo na kutanguliza midomo ya bunduki. Wakaangaza, hawakuona kitu!

"Wako wapi?" Akauliza mlinzi mmoja akipepesa macho yake makubwa.

Punde, wakasikia sauti huko nje, ya yule bwana aliyekuja kuwapasha habari,

"Wale kulee!"

Basi haraka wakatoka ndani na kwenda huko nje. Yule bwana akawaelekeza, kule mbali kwenye makontena. Ameona kitu huko. Basi walinzi wakakimbilia huko upesi.

Sekunde tano mbele ...

"Twende," sauti ya Miranda ikasema kwa kunong'ona. Kumbe hawakuwa kule ambako walidhaniwa wapo. Ulikuwa ni mtego. Walikuwa wapo nyuma ya jengo walilotoka kukwapua walichokifuata, na walitazama wale walinzi wanapoelekea.

Wakatoka hapo mafichoni, na haraka wakakimbia kwa muda wa sekunde kumi na tano, Miranda akadanda ukuta na kujivuta juu. Akamvuta pia na Marwa wakadondokea nje ya eneo la Bohari!

Hawakupoteza muda, wakaendea usafiri wao. Wakakwea na kutimka.

Sekunde kumi mbele ...

Gizani ndani ya gari, kifaa kikawaka na kuonyesha 'tracking chip' ikiwa inatembea. Dereva akaguna puani. Kisha akasema,

"Wameshatoka.

Gari likawashwa na taratibu likaanza kusonga.


**
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…