Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

steve uliahidi kila siku ,mbona leo kimya au umebanwa na majukumu mkuu
 
Comment Yangu hii ni ya mwisho Steve anamwaga story nasi tunamwaga macho.
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 32*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Gizani ndani ya gari, kifaa kikawaka na kuonyesha 'tracking chip' ikiwa inatembea. Dereva akaguna puani. Kisha akasema,

"Wameshatoka

Gari likawashwa na taratibu likaanza kusonga.

ENDELEA

Basi Miranda pamoja na Marwa wakiwa hawana habari yoyote, wakaswaga na chombo chao wakikata mitaa. Na sasa mioyo yao ikiwa misafi maana wameshakamilisha kazi.

Sasa walikuwa wanatazamia Jona apone, kisha arejee kwenye uwanja wa mapambano. Ni wazi walikuwa wanamhitaji. Ni wazi picha zake enzi za 'uhai' wake zilikuwa zinasumbua akili zao.

Basi kupunguza kuboreka ndani ya gari, Marwa akanyoosha mkono wake na kuwasha redio kisha akajilaza kitini akikonga moyo kwa nyimbo zilizokuwa zinarushwa.

Miranda akatabasamu, akamtazama mwanaume huyo na kumuuliza; "ni wapi unakumbuka?"

Redioni kulikuwa kunarushwa nyimbo za kale ya miaka ta themanini na tisini za mapema.

"Mbali sanaa!" Marwa akasema akitikisa kichwa. Na huku macho yake akiwa ameyafumba anasikiza muziki kwa hisia.

"Mbali wapi na wakati wewe ni wa juzi?" Miranda akatania. Marwa akaamka na kumkodolea macho.

"Wa juzi? Nani wa juzi?" Akauliza.

"Wewe 'apo wa juzi. Unataka kubisha nini sasa?" Miranda akatamba. "Unamjua mwenye hii gari?"

Marwa akalaza kichwa kitini kisha akafumba macho akiendelea kula muziki.

"Si yule jamaa wako wa vibodi?"

Miranda akacheka. "Sasa huwezi amini yule ni mdogo wangu, tena wa pili!"

Marwa akaitikia kwa kumridhisha.

"Nakwamba ukweli. Sikutanii!"

"Haya, dada. Shikamoo."

"Ewaa. Marhaba. Sasa umekua."

"Hivi ..." Marwa akanyanyuka na kuketi vema kitini. "Unataka kunambia tunapeleka gari kwa yule jamaa?"

"Ndio," Miranda akajibu akitazama mbele. "Umesahau makubaliano yetu?"

"Aaagh! Nimechoka asee. Kwanini tusimpelekee kesho?"

"Kesho? Hapana! Siku nyingine hutopewa ukiomba. Tutunze ahadi tuliyoiweka."

Marwa hakuridhia, ila hakuwa namna. Aliona uvivu kushuka na kuanza kutafuta usafiri mwingine. Kweli lilikuwa ni swala la kuchosha.

Basi akakaza macho yake saa hii akiwa amegemea kioo. Sijui nini alikuwa anawaza. Macho yake yakatazama 'side mirror' kwa muda mrefu na akili yake ikiwa inawandawanda huku na kule.

Japo hakuweka mazingatio kiooni, baada ya muda fulani, alitambua jambo. Alitilia shaka kuwa wanafuatwa. Kuna kitu cheupe chaenenda kila wanapokwenda.

Akakaa vema na kutazama. Akaweka mazingatio. Akatambua kitu hicho cheupe ni gari aina ya Nissan patrol.

Akasema, "Miranda, ile hadubini yako ipo begini?"

Miranda akamwambia ndio. Na akauliza anaitakia nini? Marwa hakujibu. Akarukia nyuma na kufungua begi, akatoa hadubini na kuivesha machoni. Akajitengenezea kitini na kubakisha hadubini tu juu. Akatazama.

Miranda akapata walakini. Akamtazama mwanaume huyo kwa kutumia 'sight mirror' ila hakupata wasaa wa kumzingatia kwa kina maana gari lilikuwa kwenye mwendo.

Baada ya muda kidogo, Marwa akarejesha hadubini kwenye begi kisha akatazama akiwa na uso wa hofu.

"Marwa, kuna nini?" Miranda akauliza. Ilikuwa imebakia dakika kama sita tu kuwasili kwa Kinoo. Tayari njia ya vumbi ya kuelekea huko walikuwa wameshaishika.

Marwa akashusha kwanza pumzi, kisha akamjuza Miranda kuwa wanafuatiliwa na Nissan huko nyuma. Miranda akaangaza, kweli akaliona.

"Sure?"

"Yah! Kwa muda mrefu sasa. Ndani kuna wanaume zaidi ya watatu waliovalia mavazi meusi."

Hapa kichwa cha Miranda kikaanza kuzunguka kama tiara. Nini afanye. Ni wazi sasa endapo akilipaki gari hilo kwa Kinoo, atakuwa ameuza kesi. Na inaweza ikawa huo ndiyo mwisho wao endapo adui wao anatafuta tageti ya kuwamaliza.

Basi akakanyaga mafuta kwanguvu, gari likaanza kupepea. Akaendesha kama mwehu, ila kwa ustadi na japo njia ni nyembamba.

Ndani ya muda mrefu akatokea kwenye barabara ya lami, akakata kona kuchubua barabara, akajiweka sawa, akatimka kama kishada. Ndani ya muda mfupi akawa amewapoteza maadui zake.

Haikujalisha namna gani Marwa alitazama na hadubini, hakuwaona abadani.

Ila hawakuwa wanajua. Wanaweza kukimbia ila si kujificha. Na maadui zake wakiwa wanatambua hilo, hawakuangaika kukimbizana naye. Kikubwa walichojua ni kwamba tayari Miranda ameshafahamu kuwa wameunga mkia.

Basi wakiwa wanaendesha gari lao kistaarabu kabisa, wakawa wanatazama kifaa chao namna kikienenda. Mara kinakata kona. Mara kinanyoosha.

Yule bwana dereva akawaamrisha washike silaha zao vema maana tukio linalofuata huenda likahusisha kutupiana risasi kwani tayari tageti yao imebumburuka. Wale wanaume walipofanya hivyo, basi dereva akaongeza mwendokasi.

**

Gari lilitulia tuli na kuzima. Kisha kukawa kimya kana kwamba hamna kitu hapo. Miranda na Marwa wakatazamana. Kisha wakatazama huko nje. Walikuwa wamezingirwa na nyumba zilizotulia kimya na vichaka vya hapa na pale.

Walidhani wapo eneo salama. Hakukuwa hata na watu waliokuwa wanakatiza. Miranda akamwambia Marwa hapo ni sehemu sahihi kwao kutulia wasome na kutazama mambo yanavyoenenda.

Endapo kukiwa shwari, basi wanaweza kutoka na kuendelea na safari yao. Na wakitoka hapo, waelekee moja kwa moja nyumbani, si kwa Kinoo tena.

Basi dakika zikasonga. Hawakusikia wala kuona kitu cha kutilia mashaka. Ila ilipohitimu dakika ya nane. Wakastaajabu watu watano wanasimama wakinyooshea bunduki gari lao!

Watu hawa walikuwa wamevalia barakoa na nguo nyeusi ti. Miili yao ilikuwa imetuna kwa misuli. Bila shaka walikuwa ndiyo wale jamaa wa Nissan Patrol!

Kufika hapo waliacha gari lao kwa umbali kisha wakatambaa chini kama nyoka. Ni kuja tu kustaajabu watu wananyanyuka na silaha!

"Tokeni nje upesi!" Wakaamuru. Miranda akataka fanya ujanja, ila wakamwonya. Wanamwona kila anachofanya. Aweke mikono juu na atoke nje kwa usalama wake kabla hawajamiminia risasi gari likawachakaza na wao waliomo ndani.

Basi sasa wakina Miranda wakawa hawana ujanja. Wakatoka wakiwa wameanika mikono yao juu. Na kama walivyoamriwa, wakapiga magoti. Wanaume wawili wakazama ndani ya gari lao na kupekua, mmoja wao akatoka na begi la Miranda ambamo humo ndimo kuna dawa waliyotoka iba bohari.

"Mwisho wenu umewadia. Mlidhani ninyi ni werevu sana, sio?" Akasema jamaa mmoja. Kisha akatazama zile dawa zilizokwapuliwa kule bohari kama uhakiki. Jamaa huyu ni wazi alikuwa ndiye yule dereva.

Aliporidhika na zile dawa, akazirejesha mkononi mwa aliyemkabidhi kisha akamtazama Miranda na kumwambia,

"Sasa tutafanya biashara kati yetu nawe. Upo tayari kubadili maisha yako kwa yale ya Jona?"

Miranda akamuuliza, "una maanisha nini?"

Basi yule bwana akajibu, "nikabidhi Jona nami nitakuacha na uhai wako."

Miranda akamtazama Marwa. Marwa akamtikisia kichwa akiwa amekunja uso. Miranda asijali, akarudisha uso wake kwa yule bwana na kusema, "nimekubali!"

Marwa akapayuka, "Hapana! Hapana, Miranda usifanye hivyo!!"

Miranda hata hakumtazama. Akarudia kusema kuwa ameridhia.

"Miranda!" Marwa akaita kwa uchungu. "Mirandaa!" Na mara akazirai.

"Vipi huyu?" Akauliza yule bwana.

"Ana matatizo ya kupoteza fahamu akiwa over excited!" Miranda akajibu. Basi mabwana wawili wakambeba Marwa na kumtia garini. Naye Miranda akaamrishwa asimame waelekee huko alipo Jona.

Wakamtia garini na safari ikaanza. Wakatembea kwa umbali wa kilomita moja, bwana dereva akauliza:

"Ni wewe ndiye ulimtoa Marwa kituoni?"

"Ndio, ni mimi." Miranda akajibu na kisha kukaa kimya.

"Unaonekana mwerevu sana wewe. Na jasiri haswa. Ila umefanya makosa sana maana upande uliopo si sahihi. Hakuna aliyeanzisha vita na Sheng akashinda.'

Miranda akakaa kimya.

"Ni nani bosi wako wewe? Na kwanini ulimtoa Jona kituoni?"

"Sina bosi," Miranda akajibu. "Jona ni rafiki yangu mkubwa, bila shaka hiyo ni sababu ya kumhangaikia."

Yule bwana dereva akaguna kwa cheko.

"Unajifanya mjanja sio? ... laiti usingekuwa umeingia makubaliano nami basi ningelikuwa nishakumaliza muda mrefu uliopita. Ila ntaheshimu makubaliano yangu nawe ..."

Akaendelea kulonga na kulonga, ila sasa Miranda akawa hamsikii tena. Alikuwa amezama fikirani akiwaza mambo kadhaa. La kwanza ikiwa ni namna gani atajinasua.

Alikuwa amezungukwa na 'mababa'. Na kando yake akiwa amelala Marwa. Kule viti vya mbele walikuwa wamekaa tena wababa wawili.

Ni wazi mazingira yalikuwa magumu kujikomboa hapa.

Alipotoka fikirani, akastaajabu kuona tayari wameshafika getini. Gari linasimama.

"Bila shaka ni hapa bibie?" Akasema dereva.


**
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…