Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Mwaka huu lazima ninenepe, hii Dozi sio mchezo.

Shukuran Mollel.
 
BC asijaribu kabsa kugusa Moto wa Jona, atakwenda na maji..
 
*ANGA LA WASHENZI II -- 45*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Miranda akatahamaki, “me!"

“yes, you!" BC akabweka. “kill him!" Alisema akiwa ametoa macho. Akasisitiza zaidi, Jona auawe. Na isichukue hata siku mbili awe amemletea kichwa cha mwanaume huyo mfukoni!

ENDELEA

Jambo hili lilikuwa si jepesi hata kidogo. Miranda alienda zake akiwaza mno namna gani atalitekeleza. Yaani ina maana kazi yote ile waliyoifanya, wakahatarisha na uhai wao, ni bure!

Alikosa usingizi. Hata alimtazama Jona kwa macho ya maswali hata wenzake wakajua hayuko sawa.

“vipi hujapenda chakula?" Marwa akauliza. Alijua wazi shida si chakula. Alitafuta pa kuanzia tu.

Miranda akatabasamu kiuongo alafu akaguna. Akasema, “hamna bana. Chakula ni kitamu sana tu."

Akakaa kimya kidogo. Alafu akaendelea. Hakuwa anamtazama mtu bali chakula chake.

“kuna mambo flani tu nawaza. It's not a big deal!"

“ni kuhusu Mr. Brown?" Jona akauliza akimtazama mwanamke huyo ambaye hakutaka kumtazama. Aliendelea kuangushia macho yake kwenye sahani yenye chakula alichopika Marwa. Wali na njegere.

“hapana," Miranda akatikisa kichwa. “si kuhusu yeye. Ni mambo mengine tu yananitatiza. Ila kama nilivyosema ..." Hapa akawatazama upesi. “it's not a big deal, guys. Msijali!"

Kukawa kimya kidogo. Sauti za sahani na kijiko zikivuma, na kwa mbali watu wakitafuna.

Kama dakika mbili hivi, Jona akauliza, “bila shaka ulienda kuonana na BC. Anasemaje kuhusu taarifa yangu?"

Miranda akangoja atafune na kumeza kwanza. Ila pia awaze cha kusema kichwani.

Akasema, “sikufanikiwa kuonana na BC. Alikuwa ametoka hivyo sijapata kujua msimamo wake kwenye hili. Japo najua litamkwaza kwa kiasi kikubwa."

Jona akanyamaza. Aliendelea kutafuna na baada ya muda kidogo, Miranda akanyanyuka na kuwaaga anaenda kulala.

“Unadhani yupo sawa?" Marwa akauliza punde baada ya kusikia Miranda akifunga mlango.

“hayupo sawa," akajibu Jona. “na ni kwasababu ya BC."

“BC?"

Jona akatikisa kichwa kuafiki. “japo hakutuaga, atakuwa alikwenda kwa BC. Na bila shaka alichomwambia ndicho kinamnyima raha. Najua BC hatakubali kwa urahisi kile nilichokisema."

Ila akapuuzia.

“tule bana," akamwambia Marwa. “kila kitu kitajulikana kutokana na muda. Hatuna haja ya kuhofia sana mwisho tukapoteza appetite ya kula chakula kitamu kama hiki!"

Ila kiuhalisia Jona hakuwa ‘amelipotezea' hili jambo. Na tangu hapa alifahamu fika kuwa inabidi awe makini zaidi maana lolote linaweza kutokea.

**

Saa tano asubuhi ... Shanghai, China.

Katika asubuhi hii, Lee alikuwa yupo katika chumba fulani ndani ya ghorofa refu katika jiji la Shanghai. Ndani ya chumba hichi, kitandani kulikuwa kuna begi jeusi na kuna bunduki moja ndefu, yenye kiwamba chembamba cha kumezea sauti.

Na juu kidogo ya bunduki hiyo kulikuwa kuna kifaa cha kumwekea mlengwa ‘targetini'. Kioo cha ku-zoom. Hapo mtu anapojaa kiooni na mlengaji akabofya kitufe, basi tunahesabu ashakuwa mfu!

Bunduki hii, Lee aliipa jina la ‘Death lullaby' kumaanisha wimbo mzuri wa kubembelezea kifo. Wimbo huu unapopigwa basi lazima mpigiwaji alewe na afe kifo kitamu kisicho na maumivu.

Na hicho ndicho ambacho Lee amekuja kukifanya hapa Shanghai. Amekuja kumletea mtu wimbo wa kifo. Mtu huyo aitwa bwana Chow, balozi wa Umoja wa mataifa.

Alishapata taarifa kuwa mtu huyo yupo katika hoteli hii maarufu. Yani si hii ambay Lee yupo bali ile ambayo anaitazama tangu saa kumi na mbili asubuhi.

Katika hoteli hiyo chumba namba mia thelathini, bwana Chow alikuwa amechukua hifadhi na ndani alikuwa na mwanamke kahaba. Hivyo basi ujio wake hapo hotelini ulikuwa ni wa faragha, hata mwanamke huyo alikuja hapo kama mteja mwingine tu, na chumba akalipia kabisa.

Yote hayo kwasababu ya kutotengeneza ombwe la siri kuvuja. Na pale mlangoni kulikuwa kumesimama wanaume wawili walinzi. Wamevalia suti nyeusi wakisimama kama masanamu.

Basi baada ya kungoja sana, hatimaye Lee anapata anachokitaka. Anamwona mwanamke yule kahaba akielekea ndani ya bafu akiwa amefunga taulo kifuani.

Haraka anazamisha jicho lake kwenye kioo cha lenzi na kumweka mwanamke huyo tagetini. Ila si yeye anamtaka, lah! Alifahamu tu kama mwanamke huyo anaelekea bafuni basi nyuma yake atakuwapo bwana Chow.

Na kweli. Bwana huyo akiwa amevalia taulo kiunoni naye alitokezea kwenye kamwanya kadogo kiooni akielekea bafuni. Alipita kwa kasi sana. Lee alitaka kubofya kitufe cha bunduki, ila akawahi kujizuia.

Akatulia kwanza. Akaona ni vema akavuta subra kwani endapo akitupa risasi na ikamkosa bwana huyo basi atakuwa amefanya kosa kubwa sana. Na itamgharimu muda na pesa kumpata tena bwana huyo kimyani.

Akashusha pumzi ndefu alafu akaendelea kukaa tenge kungoja. Hapa hakutaka hata mbu amsumbue. Ni kazi iliyohitaji uangalifu wa hali ya juu. Ana sekunde kama tatu tu za kufanya hilo tukio kwani kamwanya kadogo kalicho dirishani kangechukua sekunde tatu tu mtu kukapita asionekane tena.

Kwa hivyo, japo hakujua Bwana Chow atatoka muda gani bafuni, alilazimika kukaa tayari muda wote kwa jicho lake kuwa kiooni na kidole chake kupapasa kitufe tayari kwa ajili ya tukio.

Moja ... Mbili ... Tatu ... Nne ... Alikuwa anavuta pumzi akiwa ametulia katika hali ya juu. Ni pumzi yake tu ndiyo iliyosikika. Zaidi ya hapo hakuna kitu. Hata yale magari yaliyokuwa yanakatiza huko chini yakipiga honi ama kunguruma, hayakuwa yanasikika!

Lee hakuwa anayasikia.

Basi baada ya kungoja kama mwendo wa dakika ishirini na kitu hivi, mlango wa bafuni ukafunguka. Binti akatoka kutangulia. Lee akakaza kidole kwenye kitufe cha bunduki.

Sekunde mbili mbele, akatoka bwana Chow. Mlengwa. Akapiga hatua mbili tu kufika kwenye kale kamwanya ka dirisha. Alipofika hapo hakunyanyua hata mguu, Lee akafyatua risasi, ikatoboa paji la uso la bwana Chow.

Asipige hata kelele, akadondoka chini mfu. Yule mwanamke kahaba akapaza kelele za hofu kwanguvu! Wale walinzi wawili wakazama ndani. Mmoja akamtazama bwana Chow, mwingine akaangaza macho yake dirishani. Akaona tobo la risasi!

Akapaza sauti, ni mdunguaji! Basi wale wanaume wakatoka na kuanza kukimbilia kule kwenye jengo alilokuwa Lee.

Hata kabla hawajatoka ndani ya hoteli yao walikuwa tayari wameshachelewa sana. Kwani Lee ‘alishayeya' muda mrefu ndani ya sekunde kumi tu baada ya tukio.

Alitumia kamba kutoka katika dirisha la chumba chake hivyo akapotea ndani ya eneo hilo pasipo hata mapokezi kujua.

Sasa akawa ametimiza mtu wa sita kumuua kwa mkono wake. Kwenye orodha alibakiza watu wawili tu ambao kimahesabu alipangia kuwamaliza msibani.

Yaani watakapohudhuria msiba wa bwana Chow.

**

Saa kumi na mbili jioni ..

BREAKING NEWS!

Sauti nzito ilivuma redioni. Kisha ikatafsiri, habari zilizotufikia hivi punde... Baada ya hapo sauti ya kike ikadakia ikisema,

‘kamanda mkuu wa polisi nchini, amekutwa mfu nyumbani kwake baada ya kusemekana amevamiwa na watu wasiojulikana ambao walimshindilia risasi nane kifuani mwake kabla hawajaondoka katika namna ya ajabu. Habari zaidi itawafikia majira ya saa mbili usiku.'

Taarifa hiyo ikasambaa kwa upesi sana ndani ya jiji na ndani ya nchi. Ikazidi kuzua tafrani na hofu kwa wananchi kwani hata lile la mauaji ya Kamanda wa mkoa halikuwa limepatiwa ufumbuzi.

Ni nani aliyemuua Kamanda mkuu? Je ni yule yule aliyemmaliza Kamanda mkoa?

Na basi katika namna ambayo ilileta hoja nzito, serikali ya Uingereza ikahusishwa kwenye hili ikihesabiwa huenda ikawa ni kisasi cha kifo cha bwana Henry Marshall na ukamatwaji wa mtu wao, yaani Bwana Brown Curtis.

Ila hayo yote hayakuwa sahihi, kwani aliyemuua Kamanda huyo alikuwa ni bwana Sheng. Sasa yupo ofisini kwake na habari alishazipata.

Kamanda ilibidi afe tu, hakukuwa na namna. Ilibidi afe kwani anajua siri za Sheng na alijitoa mkondoni. Atabaki vipi hai?

Sheng akazima redio baada ya taarifa hiyo na kwa kujipongeza, akachomoa mvinyo kwenye jokofu akajimiminia na kupiga mafundo kadhaa.

Na akiwa hapo anakunywa, mara mlango wake ukagongwa. Akameza kwanza kinywaji kisha ndio akaruhusu mgongaji azame ndani ...

Bwana huyo mlangoni alikuwa anahema kwanguvu mpaka Sheng alisikia akiwa ndani. Na kwa kujihami alishavuta droo yake yenye silaha...

***

“we've finished!" Alisema bwana mzungu akimtazama bwana Brown aliyekuwa amekaa kitini. Walikuwa wamesimama wanaume watatu waliovalia suti, warefu na wenye miili mipana.

Wanaume hawa ni miongoni mwa wale waliotoka Uingereza wakija hapa nchini kutenda kazi. Na sasa walikuwa wameshaifanya. Wapo hapa krejesha ripoti.

“are you sure about that?" Brown Curtis aliuliza akijitengenezea kitini. Hata sigara aliacha kuvuta akawatazama watu wake kwa makini.

“yes, we are sure," akasema mwanaume mwingine. “his head's swallowed ten of our bullets!"

Bwana Brown akacheka sana mpaka akakohoa. Hakuamini kama bwana Sheng angekufa kwa urahisi hivyo. Alicheka na kulaani sana. Ila pia akawapongeza vijana wake kwa kuwamiminia kinywaji kwenye glasi.

Basi wakanywa sana na hata wakapiga soga ndefu kuhusu Uingereza. Ila ikafikia mahali bwana Brown akawaambia, “there is one simple task I want you to do."

Wale wanaume wakampatia masikio. Bwana huyo akawaeleza juu ya Jona. Anataka mwanaume huyo afe kwani aliyempatia hiyo kazi haamini kama ataitekeleza.

Pia akawasihi, “if the woman trouble you, jus kill her."

**
 
Kwa kweli mie hata sijaelewa vizuri!!

Maana hili anga sasa linazidi kuchafuka.

Ila nadhani shao kishadanja.

Mmmmhhhh, let's wait n' see!!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…