Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

*ANGA LA WASHENZI --- 48*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Mbona ameliona gari hilo pale ofisini kwa Kamanda? Akakumbuka pia na taswira ya mwanaume anayemtambua akishuka toka kwenye gari hilo. Alikuwa amevalia suti kubwa ya kahawia - suti inayofanana na ya yule aliyeambiwa na shuhuda kuwa ndiye muuaji wa Jumanne, mshirika wake kwenye biashara ya kuchora na kuuza picha!

Taswira hizo mbili zikamnyima raha. Zikampa ukweli mchungu kuwa Kamanda anahusika na jaribio lake la kumuua, vilevile la kuharibu biashara yake. Haswa kwanini?

Akakumbuka kauli aliyoambiwa na Kamanda kwa mara ya mwisho alipoonana naye ofisini kwake. MAISHA YAKE KAMWE HAYATAKUWA SAWA NJE YA JESHI. Hatomtafuta tena, bali ni yeye atakayemtafuta.

Akashtuliwa na kondakta akidai nauli. Akatoa nauli hiyo na muda si mrefu akashuka toka chomboni, akishkuru kondakta kumshtua kwani hakuwa anafahamu kama alikaribia, kisa mawazo.

ENDELEA

"Umeshampatia chakula?" Akauliza Nyokaa akiwa anamtazama kijakazi wake - mwanaume mrefu mweusi aliyevalia nguo iliyombana kifua chake kipana.

"Bado, mkuu!" Akajibu kijakazi kwa ukakamavu.

Nyokaa akamtazama kwa ukali na kufoka kwanini kijakazi huyo hajampatia Miriam chakula mpaka muda huo? Kijakazi akajibu kwa unyenyekevu kuwa mwanamke huyo hali hata pale anapompatia.

"Kutokula siyo kazi yako, bali kumpatia chakula!" Nyokaa akafoka na kumtaka mwanaume huyo haraka iwezekanavyo kwenda kumpatia Miriam chakula, naye akaenda pasipo kupoteza muda.

Nyokaa akisonya, akaketi chini na kumpigia simu Roba.

Roba alikuwa yupo Dar es salaam. Kazi yake kama alivyoagizwa ilikuwa ni kumtafuta na kumuangamiza Nade ili kumaliza chembe ya ushahidi iliyobakia. Punde simu ilipokelewa, Nyokaa akaulizia ni wapi Roba amefikia.

"Nimeshafika hospitali. Ni kitendo cha muda tu kumaliza kazi."

Nyokaa akamwambia afanikishe hilo upesi arudi Monduli kwani kuna kazi za kufanya. Roba akamuahidi ushindi.

Alipokata simu, Roba akashusha pumzi na kutazama hospitali iliyokuwa imesimama mbele yake. Alikuwa ndani ya taksi, akalipa pesa ya nauli kisha akashuka.

Mwanaume huyu alikuwa amevalia tisheti nyeusi yenye alama ya fuvu jeupe, na chini akijisitiri na suruali ya jeans na moka nyeusi.

Alikuwa na muda mchache wa kumalizana na kazi yake hapo. Alizama ndani ya hospitali na ndani ya muda mfupi akawa ameshafika stoo ya hospitali.

Mwendo wake akifanya kitu moja kwa moja kilithibitisha kwamba ana ramani ya hospitali kichwani mwake, na alishapanga jambo hilo mapema kichwani mwake.

Ndani ya muda mfupi, akawa ameshavalia koti jeupe la daktari, shingoni amezungushia kipima mapigo ya moyo, akiwa anatembea kwa kujiamini.

Akaelekea kwenye wodi za gharama, zikiwa zimegawanywa kwa vyumba vyumba vya wagonjwa binafsi.

Akafungua mlango wa chumba cha kwanza kabisa kukutana nacho, akazama ndani na kumkuta Nade akiwa amejilaza anasaidiwa na mashine kupumua.

Akahakikisha mlango umefungwa vema, alafu akachomoa sindano yenye kimiminika rangi ya 'green' na kukidungia ndani ya mfuko wa dripu. Haraka alipofanya hivyo, akatoka ndani ya chumba hicho na kupotea!

Baada ya muda wa kama dakika kumi, dripu ile ikaishilia mwilini mwa Nade. Zikapita dakika kama tano, mwili wa Nade ukaanza kubadili rangi kuwa wa njano!

***


"Tayari, nimeshakamilisha!" Sauti ya Roba ikavuma kwa simu.

"Sawa sawa. Rudi sasa nyumbani na ndege ya jioni," Nyokaa akanena na kisha akakata simu kabla hajaja kupokelewa na sauti ya kupaza ya kijakaziwe.

"Mkuu, yule mwanamke ametoroka!"

"Mwanamke?" Akastaajabu Nyokaa. "Mwanamke yupi?" Akawahi kuuliza akisimama upesi toka kwenye kiti chake cha kuvinjari.

Kijakazi akasema ni Miriam. Nyokaa kwa hasira akakimbia mpaka kule Miriam alipokuwa amehifadhiwa, hakumkuta!

Akalalama na kutusi. Akaamuru Miriam atafutwe akitishia hakuna mtu atakayebaki hai kama asiporudi na mwanamke huyo.

Wanaume wakazagaa kumtafuta 'teja' huyo kwa udi na uvumba.


***

Saa kumi na mbili jioni.


"Ameshafika!" Miranda alisema kwa tabasamu pana akiangaza getini. Alikuwa ndani ya nyumba ya BC kwa juu kabisa akiwa anaangaza kama atamwona mgeni wake akiwa anakuja.

Alikuwa amependeza kwa kuvalia gauni safi linalometameta dhidi ya giza jepesi la jioni. Nywele zake zilikuwa zimerembwa na uso wake ameupara.

Alikuwa ana hamu sana ya kumwona Boka. Alipoona gari la mwanaume huyo likiwa limefika, moyo wake ukawa wa baridi kwani 'alishampanga' BC vya kutosha.

Boka anakuja kama alivyomuahidi.

"He is here!" (Yupo hapa!) Rhoda alimwambia BC aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha kaunta ndani ya nyumba yake akiwa anakunywa wiski.

BC naye kwa kujiandaa na kikao na Boka, alikuwa 'amekula' suti nyekundu na tai nyeusi. Japokuwa kupendeza ni kawaida yake, leo alikuwa zaidi.

Alimtaka Miranda akampokee mgeni na baada ya utambulisho aende ndani, kila kitu atakifanya yeye.

"Are you sure you won't need me?" (Una uhakika hautonihitaji?) Miranda aliuliza kabla BC hajamtikisia kichwa kama ishara ya ndio. Miranda akaendaze.

Lakini kwa kutaka kujua kitakachoongeleka, akajibana mahali ambapo angepata kusikia maongezi.

"Glad to see you. My daughter's been telling me about you," (Nimefurahi kukuona. Binti yangu amekuwa akiniambia kuhusu wewe,) alisema BC kwa tabasamu akimpatia mkono Boka.

Wakateta kwa muda kidogo kupeana historia juu ya wapi walikutana na kuanza kutengeneza mahusiano na Miranda. Baada ya hapo BC akaenda kwenye kitovu cha kikao.

Pasipo kupepesa macho akamuuliza Boka kama kweli yu radhi kuwa na Miranda. Boka akakubali kwa kuwahi kujibu. Lakini BC akarudia kumuuliza mara tatu kabla ya kumwambia:

"Then there is a little sacrifice you have to make." (Basi kuna sadaka ndogo ya kutoa.)

Boka akasimamisha masikio yake asikie. BC akamweleza kuhusu biashara yake, akihitaji msaada wa mheshimiwa huyo kuingiza 'madawa' yake nchini.

Kwa mara ya kwanza Boka akadhani ni madawa ya kulevya. Moyo wake ukaenda mbio mno kabla hajapata angalau ahueni baada ya BC kumwambia ni madawa ya kutibia binadamu.

"Where are you taking them to?" (Unayepeleka wapi?) Akauliza Boka. BC akamwambia yeye hufanya biashara ya kuuza hayo madawa huko Msumbiji, Zambia na Zimbabwe kwa bei ya juu.

Lakini Boka alikuwa na hofu na hakuweza kutoa jibu la moja kwa moja kabisa kwa BC. Hata mikono yake ilikuwa inatetemeka akashindwa kubebelea kinywaji. Akaomba aende zake.

"So what about it?" (Kwahiyo vipi?) BC akauliza. Boka akabanwa na kigugumizi. Akaomba apewe muda kwani jambo hilo ni zito mno. Si la kulichukulia kiurahisi hata kidogo.

Hakumkubuka hata Miranda, akaenda zake akijawa na mawazo kedekede kichwani.

"Do you think it will work?" (Unadhani itawezekana?) Miranda akamuuliza BC akiketi.

"I don't know. Let's see!" (Sijui. Acha tuone!) BC akajibu alafu akashushia na wiski.

Boka akafika nyumbani akiwa ametingwa na mawazo hata mkewe akafahamu japokuwa hakuwa radhi kumwambia nini kimemsibu.

Akajilaza akiukosa usingizi akiwaza nini afanye. Katikati ya usiku akapokea ujumbe kwenye simu. Mkewe akawa wa kwanza kuinyaka simu.










***
 
*ANGA LA WASHENZI --- 49*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA


"So what about it?" (Kwahiyo vipi?) BC akauliza. Boka akabanwa na kigugumizi. Akaomba apewe muda kwani jambo hilo ni zito mno. Si la kulichukulia kiurahisi hata kidogo.

Hakumkubuka hata Miranda, akaenda zake akijawa na mawazo kedekede kichwani.

"Do you think it will work?" (Unadhani itawezekana?) Miranda akamuuliza BC akiketi.

"I don't know. Let's see!" (Sijui. Acha tuone!) BC akajibu alafu akashushia na wiski.

Boka akafika nyumbani akiwa ametingwa na mawazo hata mkewe akafahamu japokuwa hakuwa radhi kumwambia nini kimemsibu.

Akajilaza akiukosa usingizi akiwaza nini afanye. Katikati ya usiku akapokea ujumbe kwenye simu. Mkewe akawa wa kwanza kuinyaka simu.

ENDELEA

Moyo wa Boka ulikuwa unapiga mafundo makubwa makubwa pindi mkewe alipokuwa anatazama simu yake. Aliwaza atakuwa ni nani amemtumia ujumbe, na kwa haraka akili yake ikaegemea kwa BC.

Hakutaka mkewe ajue kinachoendelea kati yake na mwanaume huyo, sasa akadhani siri yao imeingia mchanga.

"Ni nani huyu?" Akauliza mwanamke akimkabidhi simu Boka. Boka akaipokea na kutazama, akajikuta anashusha pumzi ndefu baada ya kugundua si kile alichokuwa anakiwaza.

Alikuwa ni mfanyakazi mwenzake akimsihi kesho awahi kazini wapate kupangilia mambo ya kikao.

Lakini haikupita muda, simu yake ikaingia ujumbe. Ilikuwa ni bahati yake kwani kwa sasa ujumbe ulikuwa umetokea kwa Miranda na simu ikiwa kiganjani mwake.

Kwa muda kidogo akachat na Miranda, muda huo mkewe akiwa anadhani anachati na rafiki yake.

Mwanamke huyo, Miranda, alikuwa anamjulia hali na akimtaka amwambie ni wapi amefikia kwenye maongezi na 'baba mkwe' wake bwana BC.

Pasipo kusita, Boka akaonyesha hofu yake juu ya kile alichoambiwa na 'mkwewe' lakini kwa wakati huo akijitahidi kumwonyesha Miranda kuwa anampenda na si kwamba hafanyi jitihada.

Naye Miranda kwa maringo, akiwa anajua kidonda kipo wapi, akafanya kumtia hamasa Boka kwamba anataka kuwa naye kwa hali na mali.

"Tafadhali, fanya juu chini mpenzi. Tusiishie njiani."

Boka akiwa ameshikwa na kigugumizi cha vidole akamwomba ampatie muda kidogo. Na pia mazingira hayakuwa mazuri kuteta kwani mkewe anaweza kumpoka simu muda si mrefu.

Hivyo, wakakata maongezi. Tena baada ya Miranda kumtumia mwanaume huyo maneno matamu ya kumpa moyo. Na kisha bwana Boka kufuta chati zao za kidhalimu.

Akaweka simu kando na kumtazama mkewe, alikuwa amelala. Akashusha pumzi ndefu na kutazama paa. Hakujua ni muda gani usingizi ulimnyakua.


***


Saa mbili asubuhi, ofisi ya kamanda polisi mkoa...


Hodi ndogo iliita kisha ikaruhusiwa kuingia ndani. Alikuwa ni Jona akiwa amevalia suti rangi ya udongo, aliketi kisha akamsalimu kamanda.

"Naona umefika on time!" Kamanda akasema akitabasamu. Pasipo kupoteza muda akanyanyuka na kwenda kabatini alipotoa kiboksi cha chuma alichokiweka mezani na kukifungua, alafu akamsogezea Jona.

Ndaniye kulikuwa kuna vitu ambavyo Jona alivikabidhi siku alipoacha kazi.

"Tulijua utarejea, shida hatukujua ni siku gani haswa," alisema Kamanda akiketi. Akamwambia Jona kuwa kila kitu kipo sawa, na haikuwa shida sana kwani hakuwa amemuondoa kwenye orodha ya watumishi wake, na siku zote hizo alikuwa akihesabu kama anaumwa.

Lakini kabla ya kuendelea na majukumu yake, Kamanda akamsihi Jona kwamba kila atakachokuwa anafanya hatakuwa na budi kueleza kwa mkubwa wake.

Naye hakuwa mwingine bali Alphonce!

Jona akastaajabishwa na hilo, lakini hakuweka bayana. Alifahamu fika, yeye na Alphonce walikuwa sawa kwa cheo, iweje awe chini yake?

Kabla hajanyanyuka, Kamanda akamwambia kuna kazi kedekede za kuzifanya tangu uongozi mpya uingie madarakani. Wamekuwa wakihofia usalama wa nchi kutokana na kulegalega kwa mahusiano ya kidiplomasia na nchi jirani, kwahiyo atakuwa akisafiri mara kwa mara, haswa mikoa ya mipakani, ajiandae kwa hilo.

"Unajua mimi ni kama daraja tu la kukufikia wewe ... unahitajika nchi nzima, na kila mtu ndani ya jeshi anatambua mchango wako. Wanategemea makubwa kutoka kwako."

Baada ya maongezi hayo, Jona akanyanyuka na kwenda zake. Huku nyuma Kamanda akapiga simu na kumtonya Alphonce yaliyoendelea.

Jona alienda kantini akaketi hapo akinywa kikombe cha chai taratibu, akiwaza. Alikuwa aking'amua na kupanga nini aanze kufanya sasa kati ya yale yaliyomrejesha jeshini.

Akaona ni busara akifanya kazi ya mikono misafi kwanza, kisha akamalizana na ile itakayomchafua. Aanze kwanza na maadui wa nje, alafu atarudi nyumbani.

Akiwa hapo anakunywa chai kusindikizia mawazo, akaona gari lile prado nyeusi ikiingia. Kwa macho yake thabiti akafuatilia lile gari, akamwona Alphonce akishuka, amevalia koti refu jeusi akaangaza na kuzama ndani.

Kifuani mwake alikuwa ana jambo la wazi linalomkereketa kumhusu huyu mwanaume. Aliamini siku yake itafika na atajaa mikononi mwake, akiomba msamaha abakiziwe roho yake.

Baada ya Alphonce kupotea, Jona akarejea kwenye mawazo yake ya awali. Akalipia chai na kutoka ndani ya eneo lile la ofisi ya Kamanda, akaelekea Aga Khan hospital kwa lengo la kuonana na Nade.

Alishapata taarifa kuwa mwanamke huyo yupo huko akiwa hajifahamu tangu tukio la mauaji ya Mheshimiwa lipate kutokea. Alikuwa ana machache ya kuongea naye.

Akawaza sana kwanini mwanamke huyo alimgeuka ilhali alimsaidia dhidi ya mikono ya mbwa mwitu wasio na huruma. Ilikuwaje upesi wakamgeuka na kulenga kumuua?

Akakiri na moyo wake kwamba kuna kitu kikubwa ambacho hawakutaka kabisa akifahamu. Na sasa Mheshimiwa ameenda na siri yake kifuani.

Kama Nade asipokuwa hai, basi hakutakua na masalia yoyote sasa.

Aliomba Mungu amkute kama alivyodhamiria.

Akawasili hospitali na basi kwa kutumia kitambulisho chake akapata mwanya wa kumfikia daktari aliyekuwa anahusika ma mlengwa wake.

Daktari huyu alikuwa mwanaume mnene mwenye asili ya India. Alimtazama kwanza Jona kisha akamwambia ana bahati sana, kwani mgonjwa alikuwa amepitia tundu la sindano kubaki kuwa hai.

"Alizidiwa?" Jona akataka kujua.

"Hapana!" Daktari akatikisa kichwa. "Aliwekewa sumu kwenye dripu!"

Wakati huo walikuwa wanatembea kwenda kumwona Nade.

"Nani alimtilia sumu?"

"Hakuna anayejua. Ila kuna videos za CCTV zilizomuonyesha mtu huyo ambaye hatujamtambua mpaka sasa."

Wakafika kwa mgonjwa, Jona akamtazama kwa ukaribu. Alikuwa ana rangi ya njano kwa mbali ngozini, anahema kwa msaada wa mashine na kucha zake zilikuwa zina michirizi meusi.


"Kama tungekawia hata kwa sekunde tatu, asingekuwa hai!" Daktari akasema kwa kujiamini.

Jona akamwomba ampeleke akaone hizo video za CCTV.


***
 
*ANGA LA WASHENZI --- 50*

*Simulizi za series*


ILIPOISHIA

Daktari huyu alikuwa mwanaume mnene mwenye asili ya India. Alimtazama kwanza Jona kisha akamwambia ana bahati sana, kwani mgonjwa alikuwa amepitia tundu la sindano kubaki kuwa hai.

"Alizidiwa?" Jona akataka kujua.

"Hapana!" Daktari akatikisa kichwa. "Aliwekewa sumu kwenye dripu!"

Wakati huo walikuwa wanatembea kwenda kumwona Nade.

"Nani alimtilia sumu?"

"Hakuna anayejua. Ila kuna videos za CCTV zilizomuonyesha mtu huyo ambaye hatujamtambua mpaka sasa."

Wakafika kwa mgonjwa, Jona akamtazama kwa ukaribu. Alikuwa ana rangi ya njano kwa mbali ngozini, anahema kwa msaada wa mashine na kucha zake zilikuwa zina michirizi meusi.

"Kama tungekawia hata kwa sekunde tatu, asingekuwa hai!" Daktari akasema kwa kujiamini.

Jona akamwomba ampeleke akaone hizo video za CCTV.

ENDELEA


Pasipo kusita daktari akamuongoza mpaka mahala pa kutazamia video alipowakuta wanaume wawili waliomsalimia na kumsaidia kuiona video aitakayo.

Alipotazama vema, akajikuta anatabasamu mwenyewe na kujisemea kifuani.

"Nilijua tu," baada ya kumwona Roba akiwa anatoka ndani ya chumba.

Sasa alikuwa amethibitisha aliyeshiriki tendo la kumuua Nade ni Roba, yaani Nyokaa. Na wao pasipo shaka ndiyo ambao walifanya tukio lile la kumuua Mheshimiwa Eliakimu!

Akapata mawazo sana alipokuwa hapo. Mosi, wapi Miriam atakuwapo? Wanamfanyia nini na kwanini hao wanaume wanamhitaji kiasi hicho? Pili, wanahusika na biashara gani haswa?

Akajikuta ana kazi ya kwenda tena kule alipomuokolea Nade akawakute wanaume hao. Lakini pia apate mwanya wa kuonana na Nade, akipata ahueni, ili apate kumweleza anachokijua.

Akashusha pumzi ndefu kisha akaandikisha baadhi ya maelezo na kwenda zake baada ya kuahidi atarejea. Lakini akasihi juu ya usalama wa Nade, kwa upande wake atahakikisha anapatikana askari wa kuja kumlinda.

Akatoka ndani ya hospitali na kuangaza magari yakikatiza, akaweka mikono mfukoni na kuambaa akifuata kituo cha magari.

Lakini kuna mtu alikuwa anamtazama. Mtu huyu alikuwa amevalia koti refu na kofia ya kizee iliyomeza kichwa chake.

Baada ya Jona kusonga umbali wa kutosha toka hospitali, mtu huyu akatoka alipokuwa amejibanzia, mstimu, kisha akazama ndani ya hospitali akitembea kwa tahadhari.

Mwanaume huyu alikuwa ni Alphonce!

Kazi yake hapa ilikuwa moja tu, kujua nini Jona amekuja kufanya hapo? Ndani ya muda mfupi, akitumia nafasi yake, akawa amefika mbele ya kitanda cha Nade akimtazama mwanamke huyo kama mtu aliyemfananisha.

Kichwani kwake alikuwa anafikiria mambo kadhaa. Alisonya alafu akatoka kuongea na daktari.

"Kuna kingine?"

"Hapana, yote tumeshaeleza kwa askari aliyekuja awali."

"Nataka unieleze na mimi pia hayo yote!" Akaamuru Alphonce. Basi ikambidi Daktari arejelee yale aliyomwambia Jona, na tena zaidi kwani Alphonce alikuwa anataka kila ambacho Jona alikifanya.

Alipomaliza akatoka zake ndani mpaka kwenye gari lake alipotulia na kupiga simu kwa Kamanda akampa taarifa.

"Sijajua, ila bado wanamuwinda kumuua!"

"Na picha umeiona?" Akauliza Kamanda.

"Ndio, ila sura ni ngeni. Bila shaka ndiyo hao hao waliomuua Eli! ... kuna haja ya kuifuatilia?"

"Hapana! Anayejua ya kesi hii kwa undani ni Jona. Kuna vitu anavifahamu kuliko sisi, na kama alikuja huko ina maana ameamua kuivalia njuga. Mwache aendelee nayo, cha muhimu ni kumfuatilia tu!"

Alipokata simu, akakanyaga mafuta na kuyoyoma toka eneoni.

Ambacho hakukijua ni kwamba, hata wakati anatoka, Jona alikuwa anamuona! Alimwona tangu anaingia ndani ya hospitali na hata pale alipotoka!

Ni vile alikuwa anajua kwamba atafuatiliwa.

Akatikisa kichwa chake akibinua mdomo. Gari la Alphonce lilikuwa linaishia machoni. Akakuna kidevu chake na kushusha pumzi ndefu, kisha akajikuta anatabasamu.

"Keep your friends close, but your enemy closer!" (Waweke marafiki zako karibu, lakini maadui karibu zaidi!) Jona alijisemea kisha akanyanyua mguu kuchukua hatua.


***


"Ameamka!" Mtoto mdogo wa kike alimwambia mama yake. Haraka mama akaamka na kukimbilia ndani kutazama.

Ndani ya nyumba hii iliyochoka, kulikuwa kuna samani mbovu, mazingira yasiyovutia. Joto na pia kiza.

Mwanamke huyu akiwa ameongozana na mtoto wake, walifika ndani ya chumba chao kimoja, wakatazama kitandani. Kulikuwa kuna mwanamke amejilaza hapo kitandani kana kwamba mtu asiyejiweza. Mwanamke huyu hakuwa anaonekana vema kwasababu ya giza. Dirisha lilikuwa moja tu, dogo, na limezibwa magazeti na majarida ya zamani.

Mwanamke aliyeambatana na mwanae akawasha kibatari na kuangaza. Kumbe mwanamke aliyekuwa kitandani alikuwa ni Miriam!

"Habari yako dada?" Akasalimu mwanamke mwenye nyumba akisogeza kibatari chake auone uso wa Miriam. Macho ya mwanamke huyu yalikuwa makubwa na yenye kujali. Miriam alikuwa anamtazama kwa mbali mdomo wake ukiwa wazi.

"Habari yako dada? Naitwa Mili, wewe ni nani?"

Akajitambulisha, kumbe anaitwa Mili. Alikuwa anamtazama Miriam kwa kina akitegemea kusikia lolote toka kwake karibuni. Lakini haikuwa hivyo, Miriam hakuweza kuongea.

"Tulikukuta shambani kwetu ukiwa hujiwezi. Tungekupeleka hospitali lakini hatuna uwezo huo. Unaweza ukatuambia umetoka wapi? Wewe ni nani?" Akauliza Mili. Lakini Miriam hakuweza kutia neno. Alikuwa anasikia pia kuona lakini akishindwa kusema.

Mili akakata tamaa. Akamtazama mwanaye na kumwambia inabidi wakatoe taarifa kwa mwenyekiti wa kijiji. Alikuwa anahofia sasa yule mgeni anaweza kuwafia pale wakakosa la kusema.

Haraka mtoto akaamka, lakini ghafla Miriam akaanza kuguguma kama mtu anayesikia maumivu huku akitoa ishara kwa kutikisa kichwa! Kwa tabu akamtaka Mili asifanye alivyoadhimia.

"Msi ... en ... de ... pop...pote!" Akasema kisha akakusanya pumzi kwanza kana kwamba mwanariadha aliyekata utepe wa mwisho wa marathoni.

Mili akamtaka mwanaye amletee viazi vilivyopo kwenye bakuli kabatini, akamlisha Miriam akimsindikizia na maji ya kunywa. Angalau Miriam akapata nguvu.

Kwa taabu, akipambana na hisia za maumivu, na kwa ufupi akamweleza Mili wapi alipotokea na yeye ni nani kisha akawasisitizia Mili na mwanaye wasije wakamwambia yeyote juu yake.

"Hapa ni mbali sana toka huko!" Akasema Mili. "Siku ya kwanza walikuja wanaume wawili hapa wakatuulizia kumhusu mwanamke mwenye sifa zako, lakini tulihofia, tukakanusha kukuona."

Miriam akamuuliza kwanini alifanya hivyo. Mili akamjibu ni kwakuwa waliwaona wanaume hao wakiwa wameficha bunduki ndani ya nguo zao, wakafahamu si watu wema.

"Hata jana mwanangu alipata kumwona mmoja wa wanaume wale akirandaranda na kuangaza huku na huko!" Akamalizia Mili, kisha akamtaka Miriam apumzike wataongea zaidi baadae.


****
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…