SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
-
- #1,141
*ANGA LA WASHENZI --- 48*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbona ameliona gari hilo pale ofisini kwa Kamanda? Akakumbuka pia na taswira ya mwanaume anayemtambua akishuka toka kwenye gari hilo. Alikuwa amevalia suti kubwa ya kahawia - suti inayofanana na ya yule aliyeambiwa na shuhuda kuwa ndiye muuaji wa Jumanne, mshirika wake kwenye biashara ya kuchora na kuuza picha!
Taswira hizo mbili zikamnyima raha. Zikampa ukweli mchungu kuwa Kamanda anahusika na jaribio lake la kumuua, vilevile la kuharibu biashara yake. Haswa kwanini?
Akakumbuka kauli aliyoambiwa na Kamanda kwa mara ya mwisho alipoonana naye ofisini kwake. MAISHA YAKE KAMWE HAYATAKUWA SAWA NJE YA JESHI. Hatomtafuta tena, bali ni yeye atakayemtafuta.
Akashtuliwa na kondakta akidai nauli. Akatoa nauli hiyo na muda si mrefu akashuka toka chomboni, akishkuru kondakta kumshtua kwani hakuwa anafahamu kama alikaribia, kisa mawazo.
ENDELEA
"Umeshampatia chakula?" Akauliza Nyokaa akiwa anamtazama kijakazi wake - mwanaume mrefu mweusi aliyevalia nguo iliyombana kifua chake kipana.
"Bado, mkuu!" Akajibu kijakazi kwa ukakamavu.
Nyokaa akamtazama kwa ukali na kufoka kwanini kijakazi huyo hajampatia Miriam chakula mpaka muda huo? Kijakazi akajibu kwa unyenyekevu kuwa mwanamke huyo hali hata pale anapompatia.
"Kutokula siyo kazi yako, bali kumpatia chakula!" Nyokaa akafoka na kumtaka mwanaume huyo haraka iwezekanavyo kwenda kumpatia Miriam chakula, naye akaenda pasipo kupoteza muda.
Nyokaa akisonya, akaketi chini na kumpigia simu Roba.
Roba alikuwa yupo Dar es salaam. Kazi yake kama alivyoagizwa ilikuwa ni kumtafuta na kumuangamiza Nade ili kumaliza chembe ya ushahidi iliyobakia. Punde simu ilipokelewa, Nyokaa akaulizia ni wapi Roba amefikia.
"Nimeshafika hospitali. Ni kitendo cha muda tu kumaliza kazi."
Nyokaa akamwambia afanikishe hilo upesi arudi Monduli kwani kuna kazi za kufanya. Roba akamuahidi ushindi.
Alipokata simu, Roba akashusha pumzi na kutazama hospitali iliyokuwa imesimama mbele yake. Alikuwa ndani ya taksi, akalipa pesa ya nauli kisha akashuka.
Mwanaume huyu alikuwa amevalia tisheti nyeusi yenye alama ya fuvu jeupe, na chini akijisitiri na suruali ya jeans na moka nyeusi.
Alikuwa na muda mchache wa kumalizana na kazi yake hapo. Alizama ndani ya hospitali na ndani ya muda mfupi akawa ameshafika stoo ya hospitali.
Mwendo wake akifanya kitu moja kwa moja kilithibitisha kwamba ana ramani ya hospitali kichwani mwake, na alishapanga jambo hilo mapema kichwani mwake.
Ndani ya muda mfupi, akawa ameshavalia koti jeupe la daktari, shingoni amezungushia kipima mapigo ya moyo, akiwa anatembea kwa kujiamini.
Akaelekea kwenye wodi za gharama, zikiwa zimegawanywa kwa vyumba vyumba vya wagonjwa binafsi.
Akafungua mlango wa chumba cha kwanza kabisa kukutana nacho, akazama ndani na kumkuta Nade akiwa amejilaza anasaidiwa na mashine kupumua.
Akahakikisha mlango umefungwa vema, alafu akachomoa sindano yenye kimiminika rangi ya 'green' na kukidungia ndani ya mfuko wa dripu. Haraka alipofanya hivyo, akatoka ndani ya chumba hicho na kupotea!
Baada ya muda wa kama dakika kumi, dripu ile ikaishilia mwilini mwa Nade. Zikapita dakika kama tano, mwili wa Nade ukaanza kubadili rangi kuwa wa njano!
***
"Tayari, nimeshakamilisha!" Sauti ya Roba ikavuma kwa simu.
"Sawa sawa. Rudi sasa nyumbani na ndege ya jioni," Nyokaa akanena na kisha akakata simu kabla hajaja kupokelewa na sauti ya kupaza ya kijakaziwe.
"Mkuu, yule mwanamke ametoroka!"
"Mwanamke?" Akastaajabu Nyokaa. "Mwanamke yupi?" Akawahi kuuliza akisimama upesi toka kwenye kiti chake cha kuvinjari.
Kijakazi akasema ni Miriam. Nyokaa kwa hasira akakimbia mpaka kule Miriam alipokuwa amehifadhiwa, hakumkuta!
Akalalama na kutusi. Akaamuru Miriam atafutwe akitishia hakuna mtu atakayebaki hai kama asiporudi na mwanamke huyo.
Wanaume wakazagaa kumtafuta 'teja' huyo kwa udi na uvumba.
***
Saa kumi na mbili jioni.
"Ameshafika!" Miranda alisema kwa tabasamu pana akiangaza getini. Alikuwa ndani ya nyumba ya BC kwa juu kabisa akiwa anaangaza kama atamwona mgeni wake akiwa anakuja.
Alikuwa amependeza kwa kuvalia gauni safi linalometameta dhidi ya giza jepesi la jioni. Nywele zake zilikuwa zimerembwa na uso wake ameupara.
Alikuwa ana hamu sana ya kumwona Boka. Alipoona gari la mwanaume huyo likiwa limefika, moyo wake ukawa wa baridi kwani 'alishampanga' BC vya kutosha.
Boka anakuja kama alivyomuahidi.
"He is here!" (Yupo hapa!) Rhoda alimwambia BC aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha kaunta ndani ya nyumba yake akiwa anakunywa wiski.
BC naye kwa kujiandaa na kikao na Boka, alikuwa 'amekula' suti nyekundu na tai nyeusi. Japokuwa kupendeza ni kawaida yake, leo alikuwa zaidi.
Alimtaka Miranda akampokee mgeni na baada ya utambulisho aende ndani, kila kitu atakifanya yeye.
"Are you sure you won't need me?" (Una uhakika hautonihitaji?) Miranda aliuliza kabla BC hajamtikisia kichwa kama ishara ya ndio. Miranda akaendaze.
Lakini kwa kutaka kujua kitakachoongeleka, akajibana mahali ambapo angepata kusikia maongezi.
"Glad to see you. My daughter's been telling me about you," (Nimefurahi kukuona. Binti yangu amekuwa akiniambia kuhusu wewe,) alisema BC kwa tabasamu akimpatia mkono Boka.
Wakateta kwa muda kidogo kupeana historia juu ya wapi walikutana na kuanza kutengeneza mahusiano na Miranda. Baada ya hapo BC akaenda kwenye kitovu cha kikao.
Pasipo kupepesa macho akamuuliza Boka kama kweli yu radhi kuwa na Miranda. Boka akakubali kwa kuwahi kujibu. Lakini BC akarudia kumuuliza mara tatu kabla ya kumwambia:
"Then there is a little sacrifice you have to make." (Basi kuna sadaka ndogo ya kutoa.)
Boka akasimamisha masikio yake asikie. BC akamweleza kuhusu biashara yake, akihitaji msaada wa mheshimiwa huyo kuingiza 'madawa' yake nchini.
Kwa mara ya kwanza Boka akadhani ni madawa ya kulevya. Moyo wake ukaenda mbio mno kabla hajapata angalau ahueni baada ya BC kumwambia ni madawa ya kutibia binadamu.
"Where are you taking them to?" (Unayepeleka wapi?) Akauliza Boka. BC akamwambia yeye hufanya biashara ya kuuza hayo madawa huko Msumbiji, Zambia na Zimbabwe kwa bei ya juu.
Lakini Boka alikuwa na hofu na hakuweza kutoa jibu la moja kwa moja kabisa kwa BC. Hata mikono yake ilikuwa inatetemeka akashindwa kubebelea kinywaji. Akaomba aende zake.
"So what about it?" (Kwahiyo vipi?) BC akauliza. Boka akabanwa na kigugumizi. Akaomba apewe muda kwani jambo hilo ni zito mno. Si la kulichukulia kiurahisi hata kidogo.
Hakumkubuka hata Miranda, akaenda zake akijawa na mawazo kedekede kichwani.
"Do you think it will work?" (Unadhani itawezekana?) Miranda akamuuliza BC akiketi.
"I don't know. Let's see!" (Sijui. Acha tuone!) BC akajibu alafu akashushia na wiski.
Boka akafika nyumbani akiwa ametingwa na mawazo hata mkewe akafahamu japokuwa hakuwa radhi kumwambia nini kimemsibu.
Akajilaza akiukosa usingizi akiwaza nini afanye. Katikati ya usiku akapokea ujumbe kwenye simu. Mkewe akawa wa kwanza kuinyaka simu.
***
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Mbona ameliona gari hilo pale ofisini kwa Kamanda? Akakumbuka pia na taswira ya mwanaume anayemtambua akishuka toka kwenye gari hilo. Alikuwa amevalia suti kubwa ya kahawia - suti inayofanana na ya yule aliyeambiwa na shuhuda kuwa ndiye muuaji wa Jumanne, mshirika wake kwenye biashara ya kuchora na kuuza picha!
Taswira hizo mbili zikamnyima raha. Zikampa ukweli mchungu kuwa Kamanda anahusika na jaribio lake la kumuua, vilevile la kuharibu biashara yake. Haswa kwanini?
Akakumbuka kauli aliyoambiwa na Kamanda kwa mara ya mwisho alipoonana naye ofisini kwake. MAISHA YAKE KAMWE HAYATAKUWA SAWA NJE YA JESHI. Hatomtafuta tena, bali ni yeye atakayemtafuta.
Akashtuliwa na kondakta akidai nauli. Akatoa nauli hiyo na muda si mrefu akashuka toka chomboni, akishkuru kondakta kumshtua kwani hakuwa anafahamu kama alikaribia, kisa mawazo.
ENDELEA
"Umeshampatia chakula?" Akauliza Nyokaa akiwa anamtazama kijakazi wake - mwanaume mrefu mweusi aliyevalia nguo iliyombana kifua chake kipana.
"Bado, mkuu!" Akajibu kijakazi kwa ukakamavu.
Nyokaa akamtazama kwa ukali na kufoka kwanini kijakazi huyo hajampatia Miriam chakula mpaka muda huo? Kijakazi akajibu kwa unyenyekevu kuwa mwanamke huyo hali hata pale anapompatia.
"Kutokula siyo kazi yako, bali kumpatia chakula!" Nyokaa akafoka na kumtaka mwanaume huyo haraka iwezekanavyo kwenda kumpatia Miriam chakula, naye akaenda pasipo kupoteza muda.
Nyokaa akisonya, akaketi chini na kumpigia simu Roba.
Roba alikuwa yupo Dar es salaam. Kazi yake kama alivyoagizwa ilikuwa ni kumtafuta na kumuangamiza Nade ili kumaliza chembe ya ushahidi iliyobakia. Punde simu ilipokelewa, Nyokaa akaulizia ni wapi Roba amefikia.
"Nimeshafika hospitali. Ni kitendo cha muda tu kumaliza kazi."
Nyokaa akamwambia afanikishe hilo upesi arudi Monduli kwani kuna kazi za kufanya. Roba akamuahidi ushindi.
Alipokata simu, Roba akashusha pumzi na kutazama hospitali iliyokuwa imesimama mbele yake. Alikuwa ndani ya taksi, akalipa pesa ya nauli kisha akashuka.
Mwanaume huyu alikuwa amevalia tisheti nyeusi yenye alama ya fuvu jeupe, na chini akijisitiri na suruali ya jeans na moka nyeusi.
Alikuwa na muda mchache wa kumalizana na kazi yake hapo. Alizama ndani ya hospitali na ndani ya muda mfupi akawa ameshafika stoo ya hospitali.
Mwendo wake akifanya kitu moja kwa moja kilithibitisha kwamba ana ramani ya hospitali kichwani mwake, na alishapanga jambo hilo mapema kichwani mwake.
Ndani ya muda mfupi, akawa ameshavalia koti jeupe la daktari, shingoni amezungushia kipima mapigo ya moyo, akiwa anatembea kwa kujiamini.
Akaelekea kwenye wodi za gharama, zikiwa zimegawanywa kwa vyumba vyumba vya wagonjwa binafsi.
Akafungua mlango wa chumba cha kwanza kabisa kukutana nacho, akazama ndani na kumkuta Nade akiwa amejilaza anasaidiwa na mashine kupumua.
Akahakikisha mlango umefungwa vema, alafu akachomoa sindano yenye kimiminika rangi ya 'green' na kukidungia ndani ya mfuko wa dripu. Haraka alipofanya hivyo, akatoka ndani ya chumba hicho na kupotea!
Baada ya muda wa kama dakika kumi, dripu ile ikaishilia mwilini mwa Nade. Zikapita dakika kama tano, mwili wa Nade ukaanza kubadili rangi kuwa wa njano!
***
"Tayari, nimeshakamilisha!" Sauti ya Roba ikavuma kwa simu.
"Sawa sawa. Rudi sasa nyumbani na ndege ya jioni," Nyokaa akanena na kisha akakata simu kabla hajaja kupokelewa na sauti ya kupaza ya kijakaziwe.
"Mkuu, yule mwanamke ametoroka!"
"Mwanamke?" Akastaajabu Nyokaa. "Mwanamke yupi?" Akawahi kuuliza akisimama upesi toka kwenye kiti chake cha kuvinjari.
Kijakazi akasema ni Miriam. Nyokaa kwa hasira akakimbia mpaka kule Miriam alipokuwa amehifadhiwa, hakumkuta!
Akalalama na kutusi. Akaamuru Miriam atafutwe akitishia hakuna mtu atakayebaki hai kama asiporudi na mwanamke huyo.
Wanaume wakazagaa kumtafuta 'teja' huyo kwa udi na uvumba.
***
Saa kumi na mbili jioni.
"Ameshafika!" Miranda alisema kwa tabasamu pana akiangaza getini. Alikuwa ndani ya nyumba ya BC kwa juu kabisa akiwa anaangaza kama atamwona mgeni wake akiwa anakuja.
Alikuwa amependeza kwa kuvalia gauni safi linalometameta dhidi ya giza jepesi la jioni. Nywele zake zilikuwa zimerembwa na uso wake ameupara.
Alikuwa ana hamu sana ya kumwona Boka. Alipoona gari la mwanaume huyo likiwa limefika, moyo wake ukawa wa baridi kwani 'alishampanga' BC vya kutosha.
Boka anakuja kama alivyomuahidi.
"He is here!" (Yupo hapa!) Rhoda alimwambia BC aliyekuwa ameketi kwenye kiti cha kaunta ndani ya nyumba yake akiwa anakunywa wiski.
BC naye kwa kujiandaa na kikao na Boka, alikuwa 'amekula' suti nyekundu na tai nyeusi. Japokuwa kupendeza ni kawaida yake, leo alikuwa zaidi.
Alimtaka Miranda akampokee mgeni na baada ya utambulisho aende ndani, kila kitu atakifanya yeye.
"Are you sure you won't need me?" (Una uhakika hautonihitaji?) Miranda aliuliza kabla BC hajamtikisia kichwa kama ishara ya ndio. Miranda akaendaze.
Lakini kwa kutaka kujua kitakachoongeleka, akajibana mahali ambapo angepata kusikia maongezi.
"Glad to see you. My daughter's been telling me about you," (Nimefurahi kukuona. Binti yangu amekuwa akiniambia kuhusu wewe,) alisema BC kwa tabasamu akimpatia mkono Boka.
Wakateta kwa muda kidogo kupeana historia juu ya wapi walikutana na kuanza kutengeneza mahusiano na Miranda. Baada ya hapo BC akaenda kwenye kitovu cha kikao.
Pasipo kupepesa macho akamuuliza Boka kama kweli yu radhi kuwa na Miranda. Boka akakubali kwa kuwahi kujibu. Lakini BC akarudia kumuuliza mara tatu kabla ya kumwambia:
"Then there is a little sacrifice you have to make." (Basi kuna sadaka ndogo ya kutoa.)
Boka akasimamisha masikio yake asikie. BC akamweleza kuhusu biashara yake, akihitaji msaada wa mheshimiwa huyo kuingiza 'madawa' yake nchini.
Kwa mara ya kwanza Boka akadhani ni madawa ya kulevya. Moyo wake ukaenda mbio mno kabla hajapata angalau ahueni baada ya BC kumwambia ni madawa ya kutibia binadamu.
"Where are you taking them to?" (Unayepeleka wapi?) Akauliza Boka. BC akamwambia yeye hufanya biashara ya kuuza hayo madawa huko Msumbiji, Zambia na Zimbabwe kwa bei ya juu.
Lakini Boka alikuwa na hofu na hakuweza kutoa jibu la moja kwa moja kabisa kwa BC. Hata mikono yake ilikuwa inatetemeka akashindwa kubebelea kinywaji. Akaomba aende zake.
"So what about it?" (Kwahiyo vipi?) BC akauliza. Boka akabanwa na kigugumizi. Akaomba apewe muda kwani jambo hilo ni zito mno. Si la kulichukulia kiurahisi hata kidogo.
Hakumkubuka hata Miranda, akaenda zake akijawa na mawazo kedekede kichwani.
"Do you think it will work?" (Unadhani itawezekana?) Miranda akamuuliza BC akiketi.
"I don't know. Let's see!" (Sijui. Acha tuone!) BC akajibu alafu akashushia na wiski.
Boka akafika nyumbani akiwa ametingwa na mawazo hata mkewe akafahamu japokuwa hakuwa radhi kumwambia nini kimemsibu.
Akajilaza akiukosa usingizi akiwaza nini afanye. Katikati ya usiku akapokea ujumbe kwenye simu. Mkewe akawa wa kwanza kuinyaka simu.
***