Anga la washenzi na Joana anaona kitu usiku

Hatimaye nimewafikia!!
Riwaya nzuri kwa kweli.

Hongera mkuu kwa kazi nzuri.
 
Kwahiyo mkuu ndo unataka kusema marwa atauawa!!??
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 14*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

Miranda akasafisha koo na kuongezea:

"This is the best chance to get Jona in our side!" (Hii ni nafasi yetu kubwa kumpata Jona kwenye upande wetu!)

ENDELEA

BC akasafisha koo lake. Hakuwa anajua mengi kumhusu Jona ukilinganisha na Miranda. Miranda akachukua fursa hiyo kumweleza BC juu ya uwezo wa Jona.

Ni mwanaume wa shoka. Mwanaume ngangari, mtu wa kazi!! Endapo wakimpata mwanaume huyo basi wasijali kabisa kuhusu ulinzi na usalama. Na wala Sheng hatakuwa tena mtu wa kumhofia.

"Let's get the best out of this. It is obvious Jona's lost all of his interest in Police army. To him, they are now traitors and cruel organ." (Tufaidike na hili. Ni wazi Jona ameshapoteza hamu yake yote ndani ya jeshi la polisi. Kwake, sasa ni wasailiti na wakatili.)

Maelezo haya kwa namna fulani yakagonga kichwa cha BC. Alitokea kuvutiwa nayo. Akampa Miranda kazi ya kuhakikisha hilo linatokea. Yaani kumshawishi Jona aingie upande wao.

Hapo Miranda akakumbuka na agizo la Kinoo juu ya wale wanawake wawili: Sarah na Sasha. Akataka kumweleza BC lakini akaona huo si muda sahihi.

Wacha kwanza wapambane na hili lililopo mezani. Hili lililo kubwa. Hayo mengine yatafuata baadae. Hata hakumtonya BC juu ya hali ya Jona kule gerezani kuwa yu hoi na ameshapandikiziwa virusi.

Alihofia BC anaweza akabadili mawazo. Aidha akamchukulia Jona anaweza kuwa mzigo badala ya msaada kwao.

"So what way we gonna use?" (Sasa njia gani tutatumia?) Akauliza Miranda. Aliona wameshakubaliana wanataka kumtoa Jona. Kitu pekee kilichobaki ni namna tu.

BC akavut sigara kwa dakika kama mbili pasipo kusema kitu. Alipoweka sigara yake chini akabinua mdomo wake mkavu alafu akajitengenezea vema kumtazama Miranda.

"We need plan in this," (tunahitaji mpango kwenye hili,) akanza kutambulisha wazo lake. Miranda akamuazima masikio yote.

"We have to force him out. You know we can't do it while he's in the police station. It is better if we get the chance to have him in the truck!" (Inabidi tulazimishe atoke nje. Unajua hatuwezi akiwa ndani ya kituo cha polisi. Ni bora kama tukipata nafasi akiwa ndani ya gari!)

Mpango wa BC hapa ulikuwa ni kumchomoa Jona toka garini kwa kuliteka gari hilo ama kulipindua, aidha likiwa linatoka mahakamani ama kwenda!!

Lakini kwa Miranda alikuwa ana wazo jingine. Hili la BC aliliona ni gumu kutekelezeka kwa minajili kwamba polisi watampeleka Jona mahakamani pindi tu atakapokiri kama kweli alihusika na tukio la mauaji ya RPC kitu ambacho Jona hatakifanya abadani.

Japo wanatumia virusi kumlazimisha afanye hivyo, Miranda aliamini Jona atakuwa mgumu kuridhia.

Sasa wafanye nini?

Akili yake ikawa hii: wamchomoe Jona akiwa hapo hapo kituoni!!

"Serious??" BC akatahamaki. Lakini kabla hajamkatisha mwanamke huyo, akampatia nafasi kwanza amweleze.

Miranda akafunguka kuwa anahitaji 'tiny gas containers' kwa gharama yoyote ile. Atahitaji kama kumi hivi na ndani ziwe zijazwe na Fluothane, Neothyl pamoja na Penthrane'.

Kwa kutumia watu wawili atakaoongozana nao, basi atakamilisha zoezi la kumtoa Jona ndani ya rumande!!

"Are you sure??" BC alikuwa na wasiwasi. Kupata gesi hizo haikuwa shida hata kidogo, lakini utendaji ulimstaajabisha.

Hakutaka kumkatisha tamaa Miranda. Japo hakuelewa namba mpango huu utakavyotekelezwa, akaamua kumwamini na kumpatia nafasi. Ila akampa tahadhari.

"You have to be very careful!" (Inabidi uwe makini sana!)

"I know to keep my ass safe!" (Najua kujiweka salama!) Miranda akajibu kwa kujiamini.

Kwa asilimia zote alikuwa anaamini mpango wake utatimia!!

**

Usiku wa saa tatu...

"Naomba utupatie faragha," Miranda aliongea akimtazama Sarah. Ilikuwa ni punde kidogo tu baada ya kusalimiana na Kinoo na kujuliana hali. Sarah akanyanyuka na kuwapisha kwa kwenda nje lakini hakuwa anapenda kitu hichi hata kidogo.

Alikunja sura yake, akabinua mdomo na kutembea kwa kasi kuelekea huko nje. Mimba nayo ilikuwa inachangia. Aliona anasumbuliwa, na aidha Miranda hakuwa anajali hali aliyomo.

Kinoo akamtazama Sarah akiishia akijaribu kuhisi alichonacho mwanamke huyo kifuani. Alijua wazi Sarah alikuwa amekwazika na hakupenda kitu hicho kitokee.

Alikuwa anampenda Sarah. Na mimba yake tumboni ilimfanya amjali maradufu.

"Kwani tusingeweza kuongea akiwapo hapa?" Kinoo akauliza.

"Kama nani?" Miranda akajibu kwa swali, kisha akaongezea: "mahusiano baina yako na yeye hayahusiani hata kidogo na kazi yetu!"

"Ndiyo maana nikakusihi uwaingize!" Kinoo akatema cheche. "Tutaendelea kumtoa hivi kila tukiwa tunaongea mpaka lini? Anajihisi vibaya."

"Kinoo," Miranda akaita. "Unadhani sijali? I do care but it takes time. Be patient. Kuna kazi tunatakiwa kuifanya hapa, tuweke nguvu zetu zote hapo, punde itakapokamilika, mambo yote haya yatakuwa mepesi kama kumsukuma mlevi!"

Kinoo akatikisa kichwa akishushia pumzi puani. Akajaribu kutuliza moyo wake.

"Kazi gani hiyo?" Akauliza.

"Kumtorosha Jona kituoni!" Miranda akamjibu kana kwamba ni kazi ya kumuua mbu.

Kinoo akashangazwa. Ulikuwa ni mpango hatari huo. Yani sawa na kwenda kucheza na domo la mamba!!

Miranda akamtuliza.

"Inawezekana. Na kama kila kitu kikifanyika poa, tutatumia dakika tano tu kukamilisha zoezi hilo pasipo kumwaga tone lolote la damu!"

Kisha mwanamke huyo akatiririka kumwelezea Kinoo namna gani watafanikisha zoezi lao. Kinoo akasikiliza kwa umakini.

**

"Siku nyingine usinilete huku, uje mwenyewe!" Sarah alifoka akimtazama Kinoo kwa jicho la vita. Walikuwa ndani ya gari wakirudi nyumbani baada ya kumalizana na Miranda. Kinoo alikuwa ameshikilia usukani asionyeshe kukwaza na kauli ya 'mkewe'.

"Haitojirudia tena, usijali."

"Mara ya ngapi hii?" Akabweka Sarah. "Ya pili! Nikija mwanitoa nje. Wanileta huku ili un'toe nje?"

"Ila nilikuambia ubakie nyumbani ukakataa," Kinoo akajitetea akiwa anatazama barabara.

"Kwahiyo ndiyo maana ukaamua kuja kunikomoa, sio?" Miranda akatema cheche. "Wewe ulitarajia uniache nyumbani na nani? Nikae peke yangu nimekuwa mchawi na unajua kabisa hali yangu?"

"Nisamehe, Sarah," Kinoo akaamua kukatisha maongezi. "Halitajirudia tena nimekuahidi."

Lakini hilo halikuwa jepesi kwa Sarah. Na si tu Sarah, bali kwa wanawake. Kuna muda unaweza jikuta unahitaji 'earphones' kwani wakianza kuongea hawatakupa hata mapumziko ukanywa maji!

Kinoo hakujua ni muda gani Sarah aliacha kuongea. Alihamishia akili yake yote barabarani. Na akiwaza kazi ambayo ipo mbele yao.

Aliporudi fahamuni kuwa yupo na mtu pembeni yake, tayari mazingira yalikuwa kimya. Angalau akahema. Akamwambia sasa Sarah kuwa kuna kazo wanatakiwa kuifanya hapo mbeleni japo hakumuweka wazi ni ipi hiyo.

Sarah akapuuzia. Alikuwa analipiza kile Kinoo alimfanyia kwa kumnyamazia wakati anaongea hapo nyuma. Kinoo naye akalitambua hilo, hakuangaika naye.

"Naomba tupitie kwa Sasha," baada ya dakika mbili Sarah akanena.

"Kufanya nini huko saa hii?" Kinoo akauliza.

"Nataka nikalale huko leo. Sina hamu kabisa ya kuwa na wewe."

"Eh!" Kinoo akaguna.


**
 
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 15*

*Simulizi za series*

ILIPOISHIA

"Kufanya nini huko saa hii?" Kinoo akauliza.

"Nataka nikalale huko leo. Sina hamu kabisa ya kuwa na wewe."

"Eh!" Kinoo akaguna.

ENDELEA

Hakutaka kusema jambo akaamua kutimiza agizo la mpenzi wake huyo kuepusha maneno. Lakini bado alikuwa amekosea. Sarah akawaza pengine Kinoo alikuwa amemchoka.

Yani amemwambia akalale kwa dada yake alafu anakubali pasipo hata kubisha? Akavuta mdomo mpaka wanawasili. Walipofika ndipo akatoa ya moyoni.

"Naona umefurahi mimi kuja huku!"

Kinoo akatikisa kichwa asiseme jambo. Aliona angeongea angesababisha vingine ambavyo hakuvitarajia. Akaongoza njia mpaka getini, akagonga na wakakaa kungoja.

Ndani ya muda mfupi geti likafunguliwa na akatoka mwanamke mmoja mtu mzima. Wakamsalimu na kumwambia haja yao, kumwona Sasha.

"Mbona amehama hapa siku nyingi!" Mwanamke huyo akawaeleza. Sarah akastaajabu. Inawezekanaje dada yake akahama hapo makazi yao ya muda mrefu pasipo kumwambia??

Lakini pia atakuwa ameenda wapi na ilhali pesa hakuwa nayo? Hakupata majibu.

"Amehamia wapi?" Sarah akauliza. Yule mwanamke akamwambia hafahamu. Kitu pekee anachojua ni kwamba mwanamke huyo amehama.

"Ahsante sana," Kinoo akashukuru na kumtaka Sarah warejee kwenye usafiri waondoke zao.

Lakini wakiwa wapo njiani, Sarah hakuwa na amani. Alikuwa anamuwaza pacha wake. Alihisi atakuwa shidani. Alikosa kabisa furaha.

"Usijali, ni mtu mzima yule. Hawezi akawa amepotea," Kinoo akamtoa hofu.

Angalau hili swala likawaleta pamoja baada ya kuhitilafiana hapa nyuma.

"Mara yake ya mwisho kuonana naye alinambia hayuko vizuri kifedha. Hata nikamtoa nauli. Leo naambiwa amehama. Inashangaza!" Sarah aliongea kwa hisia.

"Au kafukuzwa kodi?" Kinoo akauliza. Lakini kabla Sarah hajajibu, Kinoo akapuuza wazo lake hilo. "Ila haiwezekani! Si angekuja pale nyumbani??"

Sarah akabaki kimya. Punde akatafuta simu yake na kumpigia dada yake. Sijui alikuwa anawaza nini akachelewa kufanya hilo. Aliweka simu sikioni kusikilizia, baada ya ukimya wa sekunde kadhaa, sauti ikamwambia anayempigia hapatikani!

Akajaribu kama mara nne, yote majibu yakiwa hayohayo, HAPATIKANI!! Sarah akazidi kujawa na hofu.

Mpaka wanafika nyumbani alikuwa kimya. Ila kheri alipokuwa anaingia ndani, simu yake ikaita. Kutazama alikuwa ni Sasha! Mwanamke huyo alimtafuta baada ya kukuta taarifa ya kutafutwa punde baada ya kuwasha simu yake.

"Hallow!"

"Hey nambie sis!"

"Mambo?"

"Poa. Unaendeleaje dear?"

"Safi tu. Upo wapi?"

"Mie? Ntakuwa wapi pengine zaidi ya nyumbani saa hii?

"Nyumbani?"

"Ndio. Nipo kwa bi Mwenda hapa."

Bi Mwenda alikuwa ni yule mwanamke aliyewafungulia geti Sarah na Kinoo walipoenda kumtembelea Sasha kule makazini.

"Sasha," Sarah akaita. "Kwanini unaniongopea?"

"Nakuongopea? Kivipi dear?"

"Umehamia wapi?"

Kidogo kukawa kimya.

"Najua umehama. Nambie umehamia wapi?"

"Sarah, yah nimehama. It's a long story. Ntakutafuta tuongee."

Simu ikakata. Sarah akaachwa na bumbuwazi. Akajaribu tena kupiga akaambiwa haipatikani!!

Sasha ana nini?? Akajiuliza akiduwaa.

**

Usiku mzima alikuwa analia kwa maumivu makali! Mifupa ilikuwa inamuuma mwili mzima. Kichwa bado kinagonga na pua inamimina damu!!

Kila alipotaka kusogeza kiungo chake cha mwili, akaishia kulalama na kushindwa. Haki mateso yalikuwa makali mno. Hakuwahi kujihisi mdhaifu kiasi hiki tangu azaliwe.

Hakuwahi kuhisi maumivu makali kiasi hiki tangu atambulishwe duniani. Haya yalikuwa kiboko!! Ni kama vile alikuwa amevunjwavunjwa mwili mzima kisha akadumbukizwa kwenye bwawa la barafu akae humo kwa masaa!

Hakuwa anahisi chochote kwa ngozi yake. Kichwa kilikuwa hakigongi tena bali kinampigia kelele kali! Ushawahi kusikia paka akikwarua bati? Ndivyo Jona alivyokuwa anasikia makelele sikioni!!

Meno yalikuwa yanamuuma. Jasho lilimwagika.

Wenzake hawakuwa na la kumsaidia zaidi ya kumtazama tu kwa huruma. Japo hawakuwa wanajua nini Jona anahisi mwilini, walimwona anateseka sana.

"Jooonnnaaaa!" Sauti kwa mbali ilimfikia masikioni. Kama kawaida sauti hii alikuwa anaisikia kwa mbali sana. Kwa taratibu sana.

Alitamani ajue sauti hii ni ya nani ila hakuweza. Maumivu alikuwa anayasikia. Kelele sikioni iliyokuwa inamuumiza, ilimnyima nafasi hiyo.

Langoni alikuwa amesimama Kamanda mkuu. Alikuwa yu ndani ya sare yake ya jeshi iliyokuwa imechafuka kwa urembo na vyeo. Macho yake yalikuwa yanamtazama Jona aliyekuwa amelala chini.

Kidogo akaungana na vijana wawili waliokuwa wamevalia kiraia. Walikuwa ni maaskari pia. Miongoni mwa vijana hao alikuwa ni yule 'jamaa' aliyemfuatiliw Marwa kuyafahamu makazi yake.

Wote wakamtazama Jona kwa muda mchache kabla Kamanda mkuu hajaagiza wamlete ofisini kwake ana maongezi naye.

**

"Jona!" Kamanda akaita akimtazama Jona kitini. Jona alikuwa amekaa hapo akiendelea kuchuruza damu puani. Alikuwa ameketi kana kwamba mgonjwa wa utindio wa ubongo. Alikuwa ameng'ata meno, amekunja ndita, mabega ameyapandisha juu. Macho amefumba kusikilizia maumivu pomoni anayosikia.

Kwa mbali sauti ya Kamanda ikamfikia:

"Jona, utaendelea na mateso haya mpaka lini? Kubali yaishe. Si kila mara utaibuka kuwa mshindi! ... naweza nikakusaidia. Nipatie nafasi."

Jona hakuwa na uwezo wa kujibu. Aliendelea kukaa vilevile kana kwamba hajasikia kitu.

"Ukifanya mchezo utafia rumande kwa ubishi wako!" Kamanda akatishia. "Sasa chagua moja nikakutupie huko uendelee na maumivu yako ama nikusaidie upate unafuu??"

Japo Jona hakuwa na uwezo wa kupambana, na alikuwa anasikia maumivu yasiyo na mithili, akafungua macho na kumtazama Kamanda. Macho yake yalikuwa mekundu mno!

Alimtazama Kamanda kwa macho ya umauti. Macho ya kisasi!!

Akiwa anahisi maumivu ya kufa, akanyoosha mkono wake akitaka kumkamata Kamanda. Ila haukufika, akashindwa kustahimili maumivu.

"Unajifanya mgumu eenh?" Kamanda akamuuliza akibinua mdomo wake. Akagonga meza mara mbili.

Puh! Puh!

**

Mlango wa ofisi ukafunguliwa, wakatoka vijana wawili wa Kamanda wakiwa wamembelelea Jona. Kwa upesi wakayoyoma naye wakielekea rumande kwenda kumtupia huko.

Mlango wa ofisi ulipofunga, Kamanda akanyaka simu yake na kupiga.

"Bado ni mgumu. Nadhani tuangalie namna ya pili sasa," Kamanda alisema kwa hakika.

"Hapana," sauti ikavuma simuni. "Ngoja tutazame na kesho kama bado ataendelea kuvumilia. Virus hao wanatafuna kila siku inavyokwenda. Hataweza kuvumilia zaidi ya kesho. Na itapendeza zaidi kama yule rafiki yake atamletea antidote!"

"Kivipi?" Kamanda akauliza.

"Hao virus ambao wapo mwilini mwake hawaondolewi na antidote waliyonayo. Endapo atakampopatia, basi ataharibu mambo zaidi. Atapata maumivu maradufu!!"

Kamanda akaridhika na hayo maelezo. Akakata simu.

**

"Nipo tayari kwa kila kitu," alisema Marwa akimtazama Miranda. Walikuwa wapo ndani ya nyumba ya Jona majira haya ya mchana. Miranda alifika hapo muda si mrefu hapo nyuma akiwa katika harakati zake za kuwezesha zoezi la kumtoa Jona kituoni.

"Sawasawa!" Miranda akatikisa kichwa. "Hili zoezi inabidi lifanyike kesho kwa namna yoyote. Wewe kazi yako ni ndogo sana. Kule kituoni wameshakuzoea sasa kuwa unaleta chakula mara kwa mara.

Sasa kesho yake nitakupatia hotpot la chakula ulipeleke huko. Utakapofika, utafanya njia zozote ulifungue pale kaunta, kwa muda wa sekunde kumi tu. Kisha ukifanikiwa kulipeleka kwa Jona, umtahadharishe asile.

Ataliweka wazi kwa dakika moja, inatosha. Mengine mimi na Kinoo tutamalizana nayo."

"Sawa, hamna shida," Marwa akapokea maelekezo. Kisha pasipo kupoteza muda akamwambia Miranda kuwa anataka kwenda kituoni kumpelekea chakula Jona.

Na pia vilevile antidote!!

"Hamna shida, naweza kukuwahisha," Miranda akamkarimu. Wakanyanyuka toka sebuleni na kwenda nje walipodumbukia ndani ya Range Rover sport nyeupe na kutimka.

**

- JE MPANGO WA PILI WA KAMANDA KAMA JONA ATAENDELEA KUWA MKAIDI NI UPI?

- MIRANDA ATAFANIKIWA ADHMA YAKE KUMTOROSHA JONA KITUONI?


- UHAI WA MARWA UPO KWENYE KITUFE CHA BUNDUKI, KITABONYEZWA?

- SASHA ATAMWAMBIA SARAH JUU YA MPANGO WAKE? VIPI UTAWABAKIZA WAKINA MIRANDA SALAMA?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…