SteveMollel
JF-Expert Member
- Jul 12, 2015
- 8,797
- 25,177
- Thread starter
-
- #1,941
*ANGA LA WASHENZI (MSIMU WA PILI) -- 18*
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Sheng, kwa hasira, akavuta droo na kutoa bunduki yake ndogo. Pasipo kujiuliza mara mbili, akamtwanga risasi tatu mwanadada huyo, akafa papo hapo!!
Mwanadada ambaye hakuwa na hatia bali akitimiza tu kazi yake.
ENDELEA
Punde wakaingia wanaume wawili na pasipo kuuliza wakanyanyua maiti na kuipeleka inapotakiwa kuwapo.
Sheng akabaki akizunguka kitini kwake akiwa na mawazo makali sana. Hakujua namna ya kufanya. Alihisi kichwa chake kimeganda. Amechanganyikiwa. Hakupata cha kufanya japo aliwaza sana.
Mwishowe akaamua kunyanyua simu na kupiga. Simu ikaita mara mbili kabla ya kupokelewa. Akasemakwa ufupi, nakuhitaji ofisini na punde muda usiende sana hapo ofisini akaingia mwanaume mmoja mwenye asili ya China.
Alisalimu na kuketi. Mwanaume huyu alikuwa ndiye yule waliyejadiliana na Sheng kipindi kile mpaka kufikia kumpelekea pesa Kamanda mkuu hotelini.
Alikuwa amevalia suti yake nyeusi. Imemkaa vema japo hakupendeza. Alikaa kitini kwa muda kidogo kabla Sheng hajamwongelesha.
Kwa muda wote huo Sheng bado alikuwa anawaza tu lakini kitu kisichoeleweka. Unajua namna mtoto mchanga aandikavyo karatasini?? Ndivyo Sheng alivyokuwa anahisi kichwani.
Yaani vuruguvurugu tupu!
Baada ya muda kidogo, akanyanyuka na kuendea jokofu. Akatoa maji madogo na kuyanyonya kama ndama afanyavyo ziwa la mamaye. Si kwamba alikuwa anahisi kiu kali, hapana. Alitaka angalau kifua chake kipoe.
Kwani la sivyo angeweza hata kuchojoa bunduki kwenye droo na kumtwanga mtu aliyemuita mwenyewe hapo.
Alipokunywa na kumaliza maji hayo, angalau kwa mbali akapata ahueni. Akamweleza yule jamaa, jinale Shao, juu ya kikichotokea. Na hakika hata Shao akapigwa na bumbuwazi zito!
Ila akatafuta namna ya kukabiiana nalo apate kumshauri mkuu wake ambaye alikuwa amekwama. Kwanza akamtoa hofu juu ya Jona.
"Wǒmen huì dédào tā!" (Tutampata!) Akasema kwa kujiamini.
"Rúguǒ wǒmen bù yuànyì dehuà, tā huì sǐ de!" (Na kama tusipofanikiwa basi atajifia)
Kwa minajili kwamba virusi waliomuingizia mwili hawatadumu naye kwa muda mrefu. Kadiri anavyokaa navyo ndivyo watakavyomdhoofisha na mwishowe kufa!!
"Tāmen yǒngyuǎn bù zhīdào cóng nǎlǐ dédào jiě yào!" (Kamwe hawatajua wapi pa kupata antidote!) Akasema Shao kwa msisitizo. Maneno hayo yakaingia ndani ya kichwa cha Sheng lakini bado hayakumkosha. Akauliza kama antidote ipo ndani ya kambi yao.
Shao akamjibu ni kiasi kidogo sana kilichopo. Hakiwezi kudumu hata zaidi ya juma moja.
"Méiyǒu! Wǒ yào lìjí mái xià suǒyǒu de jiědú jì!" (Hapana! Nataka antidote zote zifukiwe mara moja!) Sheng akabweka akigongesha kidole chake mezani. Alihofia pengine antidote hizo zinaweza kupatikana na kumsaidia Jona.
Shao akalipokea hilo agizo na kuapa kulitekeleza. Kisha akamsihi mkuu wake kutumia fedha yake sasa kama chambo cha kumpatia Jona. Aweke matangazo kote mitandaoni akitangaza kutafutwa kwa mwanaume huyo na mtu atakayetoa taarifa zitakazofanikisha upatikanaji wake basi apatiwe donge nono la pesa.
Sheng akaridhia hilo wazo kwa moyo mkunjufu. Lakini pia akaagiza vijana wake wote wa vitengo vya usalama wakutane naye usiku wa saa nne. Ana mambo kadhaa anataka kujadili nao.
**
"Hatujafanikiwa mpaka sasa, mkuu!" Sauti ilivuma kwenye simu ya Kamanda. Alikuwa amesimama koridoni akiwa amevalia taulo. Ameshikilia kiuno chake kipana.
Si sebuleni wala chumbani kulipokuwa kunakalika. Tumbo lilikuwa joto. Kama kuna kipindi kigumu alichowahi kupitia akiwa kazini, basi ni hiki.
Mwili ulikuwa unamtetemeka na kila simu iliyokuwa inapigwa alikuwa akiidaka upesi na kuiweka sikioni. Zaidi ya hapo alikuwa mbogo haswa. Hata mkewe na watoto walienda kujifungia ndani baada ya kuona hapakuwa panakalika.
"Hamjafanikiwa mnafanya nini sasa huko??" Akafoka. "Ni kazi gani mwafanya huko ina maana mmeshindwa kui-trace hiyo ambulance mkajua imeelekea wapi??"
"Tumefanya hivyo mkuu," sauti ikajitetea simuni. "Tumefuatilia na hata kwenda mpaka hospitali ambayo jina lake lilikuwa ubavuni mwa ambulance hiyo ..."
"Wakasemaje??" Kamanda akakatiza.
"Hawaitambui hiyo ambulance! Haipo kwenye orodha ya usafiri wao. It means ilifojiwa tu!"
"Na namba?? ... hizo plate nu-number je??" Kamanda akauliza upesi.
"Namba tumezifuatilia, ni za biashara. Gari lilisajiliwa kama daladala ila kuhusu mwenye mali nayo alikwisha fariki muda sana. Hata hili gari halikuwa likifanya kazi hiyo ya daladala kwa muda mrefu hapa jijini kutokana na marufuku ya vyombo vya aina hiyo kufanya kazi hiyo jijini."
Kamanda akashusha pumzi ndefu kisha akauliza:
"Sasa mmefanyaje?"
"Bado tunaendelea na upelelezi mkuu, tutakapopata chochote kitu basi tutakutaarifu."
Kamanda akakata simu na kurejea sebuleni. Akakaa hapo akiwaza na kuwazua nini afanye. Akiwa hapo, mara simu yake ikaita. Akatazama alikuwa ni Sheng. Akapokea simu na kuiweka sikioni.
Sheng akampa taarifa ya kumhitaji ofisini kwake majira ya saa nne usiku.
**
"This is disgrace to Wu family!" (Hii ni fedheha kwa familia ya Wu!) Sheng aliwaka. Macho yake yalikuwa mekundu. Hakuketi kitini, alihisi hataeleweka. Aliongea kwa hasira na jazba.
"Siwezi kukubali kudhalilishwa kiasi hiki na kikundi kidogo cha watu. Kamwe!"
Akatazama kushoto na kulia akipekua rundo la wafanyakazi wake wanaomtazama kwa umakini. Ukumbi ulikuwa kimya. Hata mbu angelikatiza hapo angelisikika.
Vijana watabe, vijana wa kazi, wachina kwa weusi, walikuwa wametega sikio kumsikiliza mkuu wao. Na wakiwa tayari kubeba agizo lolote lile watakalokabidhiwa.
"Sasa ni hivi," Sheng akaelekeza kwa mkono. "Kwa sasa kazi zote zitasitishwa. Hakuna kufanya kazi nyingine yoyote isipokuwa moja tu! Kumtafuta Jona popote alipo. Yeyote atakayeleta kichwa chake ofisini kwangu, nitampatia cash shilingi milioni mia nane!
Zoezi hili lisizidi mwezi mmoja tangu sasa."
Baada ya hayo akawataka waende. Akabaki na Shao aliyejadiliana naye kwa sekunde kadhaa kabla hajamuuliza kumhusu Lee.
"Tā zài nǎlǐ?" (Yuko wapi?)
Shao akapandisha mabega akisema hana taarifa naye.
Kabla hawjajadiliana zaidi, kijakazi akaja na kumpasha habari Sheng kuwa ana mgeni. Kamanda mkuu ameshafika ofisini kwake.
**
"Nimekuita hapa kwa jambo moja," Sheng alifungua kijikao chake cha dharura. Mbele yake alikuwa ameketi Kamanda mkuu akiwa ndani ya shati la kitenge na suruali nyeusi ya kitambaa.
"Nahitaji silaha zaidi kwa ajili ya kazi zangu. Nataka unisaidie kwenye hilo."
"Silaha?" Kamanda akadakia. "Nitakusaidiaje bwana Sheng. Ni ngumu kutoa silaha stock na kukupatia. Itaweza leta suspicions!"
"No! No! No!" Sheng akatikisa kichwa. "Sihitaji silaha zako. Kuna mzigo mkubwa utafika bandarini ukiwa kwenye meli ya wauguzi wanaokuja kutoa huduma ya matibabu bure hapa nchini. Ndani ya meli hiyo kubwa kuna kontena zangu mbili za silaha. Ninachojitaji wewe ufanye ni kuzipitisha kwa kutumia jina la jeshi. Basi!"
Kamanda akameza mate.
"I need them kwa ajili ya kumsaka Jona!" Sheng akamalizia habari.
**
Sasa shauri lilikuwa limekatwa na kesi imefikishwa mahakamani. Boka na Miranda wakataarifiwa kuhitajika kituo cha polisi mara moja.
Ikiwa ni majira ya jioni, Miranda na Boka wakawasili hapo kila mtu akija na usafiri wake lakini ikionyesha bayana kuwa walikuwa na mawasiliano.
Boka alikuwa ameongozana na mwanasheria wake, Bwana Manyanja Mayanja, ambaye yeye ndiye alikuwa akihusika na kila kitu hapo huku mteja wake akiwa msikilizaji tu.
Kwa msaada wa mwanasheria bwana Mayanja Mayanja, wakapewa dhamana na zaidi tarehe za kuhudhuria mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi yao.
"Tutakaposhinda kesi hii, jamhuri italazimika kulipa fidia ya muda na usumbufu na pia kusafisha taswira ya mteja wangu kwa kupitia vyombo vyao vyote vya habari!" Bwana Mayanja Mayanja alinguruma.
Baada ya hapo wakatoka kituoni, ila kabla hawajakwea kwenye vyombo vyao vya usafiri, mara Miranda akaitwa.
Alipogeuka akakutana uso kwa uso na Koplo Massawe.
**
Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app
*Simulizi za series*
ILIPOISHIA
Sheng, kwa hasira, akavuta droo na kutoa bunduki yake ndogo. Pasipo kujiuliza mara mbili, akamtwanga risasi tatu mwanadada huyo, akafa papo hapo!!
Mwanadada ambaye hakuwa na hatia bali akitimiza tu kazi yake.
ENDELEA
Punde wakaingia wanaume wawili na pasipo kuuliza wakanyanyua maiti na kuipeleka inapotakiwa kuwapo.
Sheng akabaki akizunguka kitini kwake akiwa na mawazo makali sana. Hakujua namna ya kufanya. Alihisi kichwa chake kimeganda. Amechanganyikiwa. Hakupata cha kufanya japo aliwaza sana.
Mwishowe akaamua kunyanyua simu na kupiga. Simu ikaita mara mbili kabla ya kupokelewa. Akasemakwa ufupi, nakuhitaji ofisini na punde muda usiende sana hapo ofisini akaingia mwanaume mmoja mwenye asili ya China.
Alisalimu na kuketi. Mwanaume huyu alikuwa ndiye yule waliyejadiliana na Sheng kipindi kile mpaka kufikia kumpelekea pesa Kamanda mkuu hotelini.
Alikuwa amevalia suti yake nyeusi. Imemkaa vema japo hakupendeza. Alikaa kitini kwa muda kidogo kabla Sheng hajamwongelesha.
Kwa muda wote huo Sheng bado alikuwa anawaza tu lakini kitu kisichoeleweka. Unajua namna mtoto mchanga aandikavyo karatasini?? Ndivyo Sheng alivyokuwa anahisi kichwani.
Yaani vuruguvurugu tupu!
Baada ya muda kidogo, akanyanyuka na kuendea jokofu. Akatoa maji madogo na kuyanyonya kama ndama afanyavyo ziwa la mamaye. Si kwamba alikuwa anahisi kiu kali, hapana. Alitaka angalau kifua chake kipoe.
Kwani la sivyo angeweza hata kuchojoa bunduki kwenye droo na kumtwanga mtu aliyemuita mwenyewe hapo.
Alipokunywa na kumaliza maji hayo, angalau kwa mbali akapata ahueni. Akamweleza yule jamaa, jinale Shao, juu ya kikichotokea. Na hakika hata Shao akapigwa na bumbuwazi zito!
Ila akatafuta namna ya kukabiiana nalo apate kumshauri mkuu wake ambaye alikuwa amekwama. Kwanza akamtoa hofu juu ya Jona.
"Wǒmen huì dédào tā!" (Tutampata!) Akasema kwa kujiamini.
"Rúguǒ wǒmen bù yuànyì dehuà, tā huì sǐ de!" (Na kama tusipofanikiwa basi atajifia)
Kwa minajili kwamba virusi waliomuingizia mwili hawatadumu naye kwa muda mrefu. Kadiri anavyokaa navyo ndivyo watakavyomdhoofisha na mwishowe kufa!!
"Tāmen yǒngyuǎn bù zhīdào cóng nǎlǐ dédào jiě yào!" (Kamwe hawatajua wapi pa kupata antidote!) Akasema Shao kwa msisitizo. Maneno hayo yakaingia ndani ya kichwa cha Sheng lakini bado hayakumkosha. Akauliza kama antidote ipo ndani ya kambi yao.
Shao akamjibu ni kiasi kidogo sana kilichopo. Hakiwezi kudumu hata zaidi ya juma moja.
"Méiyǒu! Wǒ yào lìjí mái xià suǒyǒu de jiědú jì!" (Hapana! Nataka antidote zote zifukiwe mara moja!) Sheng akabweka akigongesha kidole chake mezani. Alihofia pengine antidote hizo zinaweza kupatikana na kumsaidia Jona.
Shao akalipokea hilo agizo na kuapa kulitekeleza. Kisha akamsihi mkuu wake kutumia fedha yake sasa kama chambo cha kumpatia Jona. Aweke matangazo kote mitandaoni akitangaza kutafutwa kwa mwanaume huyo na mtu atakayetoa taarifa zitakazofanikisha upatikanaji wake basi apatiwe donge nono la pesa.
Sheng akaridhia hilo wazo kwa moyo mkunjufu. Lakini pia akaagiza vijana wake wote wa vitengo vya usalama wakutane naye usiku wa saa nne. Ana mambo kadhaa anataka kujadili nao.
**
"Hatujafanikiwa mpaka sasa, mkuu!" Sauti ilivuma kwenye simu ya Kamanda. Alikuwa amesimama koridoni akiwa amevalia taulo. Ameshikilia kiuno chake kipana.
Si sebuleni wala chumbani kulipokuwa kunakalika. Tumbo lilikuwa joto. Kama kuna kipindi kigumu alichowahi kupitia akiwa kazini, basi ni hiki.
Mwili ulikuwa unamtetemeka na kila simu iliyokuwa inapigwa alikuwa akiidaka upesi na kuiweka sikioni. Zaidi ya hapo alikuwa mbogo haswa. Hata mkewe na watoto walienda kujifungia ndani baada ya kuona hapakuwa panakalika.
"Hamjafanikiwa mnafanya nini sasa huko??" Akafoka. "Ni kazi gani mwafanya huko ina maana mmeshindwa kui-trace hiyo ambulance mkajua imeelekea wapi??"
"Tumefanya hivyo mkuu," sauti ikajitetea simuni. "Tumefuatilia na hata kwenda mpaka hospitali ambayo jina lake lilikuwa ubavuni mwa ambulance hiyo ..."
"Wakasemaje??" Kamanda akakatiza.
"Hawaitambui hiyo ambulance! Haipo kwenye orodha ya usafiri wao. It means ilifojiwa tu!"
"Na namba?? ... hizo plate nu-number je??" Kamanda akauliza upesi.
"Namba tumezifuatilia, ni za biashara. Gari lilisajiliwa kama daladala ila kuhusu mwenye mali nayo alikwisha fariki muda sana. Hata hili gari halikuwa likifanya kazi hiyo ya daladala kwa muda mrefu hapa jijini kutokana na marufuku ya vyombo vya aina hiyo kufanya kazi hiyo jijini."
Kamanda akashusha pumzi ndefu kisha akauliza:
"Sasa mmefanyaje?"
"Bado tunaendelea na upelelezi mkuu, tutakapopata chochote kitu basi tutakutaarifu."
Kamanda akakata simu na kurejea sebuleni. Akakaa hapo akiwaza na kuwazua nini afanye. Akiwa hapo, mara simu yake ikaita. Akatazama alikuwa ni Sheng. Akapokea simu na kuiweka sikioni.
Sheng akampa taarifa ya kumhitaji ofisini kwake majira ya saa nne usiku.
**
"This is disgrace to Wu family!" (Hii ni fedheha kwa familia ya Wu!) Sheng aliwaka. Macho yake yalikuwa mekundu. Hakuketi kitini, alihisi hataeleweka. Aliongea kwa hasira na jazba.
"Siwezi kukubali kudhalilishwa kiasi hiki na kikundi kidogo cha watu. Kamwe!"
Akatazama kushoto na kulia akipekua rundo la wafanyakazi wake wanaomtazama kwa umakini. Ukumbi ulikuwa kimya. Hata mbu angelikatiza hapo angelisikika.
Vijana watabe, vijana wa kazi, wachina kwa weusi, walikuwa wametega sikio kumsikiliza mkuu wao. Na wakiwa tayari kubeba agizo lolote lile watakalokabidhiwa.
"Sasa ni hivi," Sheng akaelekeza kwa mkono. "Kwa sasa kazi zote zitasitishwa. Hakuna kufanya kazi nyingine yoyote isipokuwa moja tu! Kumtafuta Jona popote alipo. Yeyote atakayeleta kichwa chake ofisini kwangu, nitampatia cash shilingi milioni mia nane!
Zoezi hili lisizidi mwezi mmoja tangu sasa."
Baada ya hayo akawataka waende. Akabaki na Shao aliyejadiliana naye kwa sekunde kadhaa kabla hajamuuliza kumhusu Lee.
"Tā zài nǎlǐ?" (Yuko wapi?)
Shao akapandisha mabega akisema hana taarifa naye.
Kabla hawjajadiliana zaidi, kijakazi akaja na kumpasha habari Sheng kuwa ana mgeni. Kamanda mkuu ameshafika ofisini kwake.
**
"Nimekuita hapa kwa jambo moja," Sheng alifungua kijikao chake cha dharura. Mbele yake alikuwa ameketi Kamanda mkuu akiwa ndani ya shati la kitenge na suruali nyeusi ya kitambaa.
"Nahitaji silaha zaidi kwa ajili ya kazi zangu. Nataka unisaidie kwenye hilo."
"Silaha?" Kamanda akadakia. "Nitakusaidiaje bwana Sheng. Ni ngumu kutoa silaha stock na kukupatia. Itaweza leta suspicions!"
"No! No! No!" Sheng akatikisa kichwa. "Sihitaji silaha zako. Kuna mzigo mkubwa utafika bandarini ukiwa kwenye meli ya wauguzi wanaokuja kutoa huduma ya matibabu bure hapa nchini. Ndani ya meli hiyo kubwa kuna kontena zangu mbili za silaha. Ninachojitaji wewe ufanye ni kuzipitisha kwa kutumia jina la jeshi. Basi!"
Kamanda akameza mate.
"I need them kwa ajili ya kumsaka Jona!" Sheng akamalizia habari.
**
Sasa shauri lilikuwa limekatwa na kesi imefikishwa mahakamani. Boka na Miranda wakataarifiwa kuhitajika kituo cha polisi mara moja.
Ikiwa ni majira ya jioni, Miranda na Boka wakawasili hapo kila mtu akija na usafiri wake lakini ikionyesha bayana kuwa walikuwa na mawasiliano.
Boka alikuwa ameongozana na mwanasheria wake, Bwana Manyanja Mayanja, ambaye yeye ndiye alikuwa akihusika na kila kitu hapo huku mteja wake akiwa msikilizaji tu.
Kwa msaada wa mwanasheria bwana Mayanja Mayanja, wakapewa dhamana na zaidi tarehe za kuhudhuria mahakama kwa ajili ya kusikiliza kesi yao.
"Tutakaposhinda kesi hii, jamhuri italazimika kulipa fidia ya muda na usumbufu na pia kusafisha taswira ya mteja wangu kwa kupitia vyombo vyao vyote vya habari!" Bwana Mayanja Mayanja alinguruma.
Baada ya hapo wakatoka kituoni, ila kabla hawajakwea kwenye vyombo vyao vya usafiri, mara Miranda akaitwa.
Alipogeuka akakutana uso kwa uso na Koplo Massawe.
**
Sent from my SM-J110F using JamiiForums mobile app