BARA BARA YA 5
JF-Expert Member
- Sep 11, 2009
- 1,174
- 835
Nimepita gereji mara moja mida ya saa tisa hivi, fundi wangu kaletewa wali maharage na maparachichi kama matatu hivi, akashushia fanta ile nyeusi.
Baada ya kama dakika kumi akapita muuza madafu akanunua moja kanywa maji na ile ya ndani kakwanguliwa, akapita muuza karanga kanunua fungu moja baada muda hivi kaja muuza machenza kanunua mawili, kamaliza kapita dada anauza mihogo mibichi na matango kununua kala.
Wakati naanza kupata wasiwasi ghafla mkaka anauza miwa kaja fundi kachukua vipakti vitatu. Nikijua sasa huu ni mwisho ghafla kaja dada anatembeza mahindi ya kuchemsha bila hata kujistukia fundi kaagiza moja.
Nikiwa nimetoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango ghafla kaja dada anauza uji wa mchele, fundi bila kupepesa macho kaagiza kikombe kimoja.
Wakati najiandaa sasa kuondoka kaja muuza pweza wale vipande na supu kwenye chupa ya chai kanunua kama vipande saba.
Muda huu naondoka nimepishana na muuza kahawa. Watu wanamiliki matumbo wallah.
Baada ya kama dakika kumi akapita muuza madafu akanunua moja kanywa maji na ile ya ndani kakwanguliwa, akapita muuza karanga kanunua fungu moja baada muda hivi kaja muuza machenza kanunua mawili, kamaliza kapita dada anauza mihogo mibichi na matango kununua kala.
Wakati naanza kupata wasiwasi ghafla mkaka anauza miwa kaja fundi kachukua vipakti vitatu. Nikijua sasa huu ni mwisho ghafla kaja dada anatembeza mahindi ya kuchemsha bila hata kujistukia fundi kaagiza moja.
Nikiwa nimetoa macho kama mjusi aliyebanwa na mlango ghafla kaja dada anauza uji wa mchele, fundi bila kupepesa macho kaagiza kikombe kimoja.
Wakati najiandaa sasa kuondoka kaja muuza pweza wale vipande na supu kwenye chupa ya chai kanunua kama vipande saba.
Muda huu naondoka nimepishana na muuza kahawa. Watu wanamiliki matumbo wallah.