Angalizo kuhusu kitabu cha “Rich dad - Poor dad”

Ukweli ndio huo, hata uende marekani km huwezi jiongeza utasanda tu.
 
Kuna vitu ambavyo binafsi huwa navifundisha lakini sivifanyii kazi.

Ila kila ninachokufundisha nilishakijaribu kwa vitendo, nikaacha kuendelea nacho kwa sababu maalumu.

Hicho kitabu; kinafungua macho ili kila utakachotenda ujue mbele kuna nini.
 
Big up,
 
Kitabu kizuri sana, kimenisaidia sana yaani sasa najiamini kutohangaika na kununua liabilities. Kwa sasa naamini hata nikiwa na pesa ndogo nitaweza kuanzisha biashara ndogo ila inayokua.
ASANTE SANA ROBERT KIYOSAKI maana haukupoteza muda wako kuandika kitabu hiki.
 
Mwanzo wa business yoyote ni kujua Wateja wako wanataka nini na kujua namna Bora yakuwahudumia.

Biashara nyingi zina-fail kwasababu waanzilishi wanadhani wanajua zaidi ya wataja wanaotaka kuwapatia huduma.

Makosa kama haya yanaweza kuepukwa kama utapata mentor mzuri.

Na moja ya mentorship unaweza kutumia vitabu, maandishi au kupata mawasiliano kabisa na role model wako.

Rich Dad, Poor Dad inakufundisha financial literacy.

Lakini hiyo ni kiasi kidogo utakachojifunza kuhusu kuunda business.

Kama upo na wazo la biashara ngoja nikupe tips ambazo zitasaidia sana wewe kuepuka makosa.

1. Eleleza akili yako kwenye kugundua tatizo.

- usiwazie jinsi utakavyotatua tatizo. Juwa kwanza je kuna tatizo sehemu fulani. Write them down on your notebook ili usisahau.

2. Ongea na watu wachache wanaokutana na hilo tatizo na uwaulize je unaweza kuwasaidia vipi?

3. Tengeneza suluhisho la hilo tatizo kama wanavyopenda clients wako.

Ukifuata hizo hatua utaokoa muda na fedha.

Well, kwa ambaye anapenda kupata namna ya kutengeneza hela kwakutumia ujuzi wowote alionao contact me through my email address wiserastarising@gmail.com

I'm building freelance platform ya kwanza ya Kiswahili. And everyone can join. It's FREE.

You won't pay a dime.

Wakuu nahitaji kuwasiliana na walio-interested ili nijie namna nzuri yakufanikisha hili.

Lengo langu ni kutatua hii changamoto ya watu kushindwa kutengeneza kipato wanapoteza muda au kudanganywa na online marketers wasio waaminifu.

Nitajibu ujumbe punde nikipokea.
 
Hiyo imekaa poa sana.
 
Mtazamo wa rich dad niliamua kuufuata nikiwa mwaka wa pili chuo. Nivigumu sana but nivilahisi ukizamilia. Sijafanikiwa sana hadi sasa but hadi Leo sijachukua cheti cha kuhitimu chuo na pia mfanyakazi wa mshahara wa 1million siyo kitu kwangu ambaye naendesha maisha ya utafutaji wa kijasiliamali. Jambo linalonifariji kwa kufata mtazamo wa rich Dad I see the Bright future.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Je unaposoma kitabu nini ni lengo hasa?
Labda tuanzie hapa.
 
Kuna mambo mengi unaweza kujifunza kwenye kitabu cha Rich Dad, Poor Dad. Nadhani wewe umeangalia jambo moja ambalo linahusiana na msisitizo wa Kujiajiri ni bora kuliko Kuajiriwa.

1. Je dhana ya kufanikiwa inahitaji zaidi ni kiasi gani cha fedha unahifadhi na unawekeza badala kiasi gani unatengeneza nayo ni ya watu wa Marekani?

2. Msisitizo wa kununua Real Assets (kama viwanja, mashamba, nyumba n.k) badala ya Liabilities (gari ya kutembelea kama huna fedha ya kuitunza, nyumba ya kifahari unayoilipia kodi pasipo kukuingizia/hauishi) je hiyo ni kwa Wamarekani tu

3. Dhana ya kujilipa wewe kwanza (Save the amount you want to save, before starting spending your income) je hiyo haiwezi kumsaidia Mtanzania wa Nachingwea ambaye ni muuza korosho?

4. Dhana ya kuwa na jambo ambalo litakupa usongo wa kutaka kutoka kimaisha ni la Wazungu tu? Mfano anashauri wengine wanaweza kutumia mapenzi, wengine waliwahi kufedheheshwa na kudharaulika, wengine wanataka watembelee ulimwengu n.k Kiyosaki anashauri utafute sababu ili upambane kwenye maisha mpaka utoke.

6. Kuwa Mtoaji wa Kihindi (Indian Giver). Ukikopesha hakikisha unarudishiwa, ukisaidia ni pale inapolazimu, usiwe unatapanya mali. Nitatoa mifano ya kibongo, usipende sifa bar kwa washikaji, usipende sifa kwa wanawake, usitoe hela kwa watu hovyo hovyo.





Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…