Angekuwepo Hayati Magufuli bwawa la JNHP lingekamilika Juni 2022 na tungeanza kupata umeme kwa bei nafuu


Huyo mpika data aliyedanganya kipande cha Sgr Dar-Moro kitakuwa tayari mpaka Nov 2019?
 
Nimecheka kwa dharau, rubbish 🚮🚮
 
Huyo mpika data aliyedanganya kipande cha Sgr Dar-Moro kitakuwa tayari mpaka Nov 2019?
Tindo mimi nakujua kabisa wewe una chuki na hayati. Kipande cha Sgr Moro Dar kilikuwa na changamoto nyingi huwezi kukubali hata ukiambiwa ukweli.
 
Muda wa kwisha mradi haukuwa realistic. Uliwekwa kumfurahisha mtu kwa jinsi yeye alivyotaka
 
Mwandishi hana tofauti na yatima anayedeka shuleni na kusema angekuwepo Mama nisingechapwa kwa kufeli darasani ilihali ni uzembe wake
 
Tusipotoshane, Tatizo la mradiule ni makosa ya kiufundi katika ujenzi wake. Ni tatizo la mkandarasi wala sio la kisiasa. Hata angekuwa Magu mradi usingekamilika Juni mwaka huu.

Kiufupi ilibidi tuwachukue Warusi kuwa wakandarasi, kwani hata Misri mabwawa yao yalijengwa na mrusi. Sijui ni nini kilichomfanya Magu awape waMISRI kujenga mradi mkubwa kama Ule. Sasa tupo njia panda!
 
Muda wa kwisha mradi haukuwa realistic. Uliwekwa kumfurahisha mtu kwa jinsi yeye alivyotaka
Yani wewe upo busy ku criticize muda, but you can't use the brain of yours kuona alikuwa mtu wa namna gani even to dare kuanzisha huo mradi, kwa akili za viongozi wetu unafikili wangapi wangefikisha huo mradi ulipo Sasa? JPM dared to transform this country, hata kuanzisha tu mradi wa bwawa la umeme its daring ya hali ya juu sana that you won't see in most leaders hapa kwetu. Wengi wapo kutuumiza tu na kuibia taifa..

Shida wengi "akili" zimefungwa governor hauwezi fikiri mambo beyond petty things kama vile mradi utakamilika lini...watu weusi sisi kuna kitu huwa hakiko sawa kwenye vichwa vyetu si bure!!
 
Sio kweli, mkandarasi ndio alikuwa analalamika juu ya milima na hali ya hewa kumchelewesha.

Mkuu unajipa tabu bila sababu ya msingi. Hiyo miradi inaenda kwa spidi ya kawaida kulingana na mazingira halisi ya kitanzania. Hata Magufuli angekuwepo leo hali isingekuwa tofauti sana. Labda “narrative” tu ndiyo ingeboreshwa. Tena naona awamu ya 6 inajitahidi sana. Ni mara ya kwanza Tanzania inabeba mzigo mkubwa wa miradi ya kiwango hicho kwa pamoja. Uwezo wa nchi hii kiuchumi na kimenejimenti sio mkubwa kuweza kuhimili yote hayo kwa kasi.

Magufuli alikuwa mhamasishaji. Alikuwa populist. Aliaminisha wengi kuhusu “uwezo mkubwa sana” wa Tanzania ambao kiuhalisia HAUPO. Alijua wengi wana hulka kama wale ndugu zetu wa ile modeli yenye kupenda maneno mazuri mazuri na “kupetiwa petiwa”. Wengi mmeweka matumaini YA KUPITILIZA kuhusu uwezo wa nchi. Mmeiweka serikali ya CCM kwenye hali ngumu sana. Sisi watazamaji tunaona sawa tu kwani tunasubiri sana kuiona siku CCM itakapoanza kuiishi KWELI na kuachana na ulaghai inaofanya kwa taifa miaka mingi sasa.

Serikali ya awamu ya 6 inajitahidi kufikia matarajio yenu kwa kuhangaika sana. Na uzuri inajaribu kuwa honest kuhusu vyanzo vya pesa. Lakini ukweli utabaki pale pale. Hiyo miradi itachukua miaka kukamilika tena kwa maumivu. Na kwa mtakaoshuhudia ikikamilika itabidi mumshukuru Mungu sana kwa kuwaweka hai hadi wakati huo.

Pia muelewe kuwa kwa pesa kubwa na mikopo ghali iliyowekezwa pale JNHPP msiweke sana matumaini ya umeme wa ile bei rahisi mliyoambiwa. Labda kuwe na ruzuku kubwa sana - ambayo itakuwa maumivu kwenye maeneo mengine ya sekta za kiuchumi na kijamii. Jitahidini sana muanze kuwa REALISTS. Msiumize nafsi zenu bure!
 
We bwege umeenda shule? Pesa hazipo kwa ajili ya mradi?
Badala ya kujibu unakimbilia kutoa lugha za ovyo...

Binafsi nishasema sana hapa kwamba JPM Administration ilijaa UONGO lakini tukaonekana tuna chuki!!

Ripoti ya CAG (Development Projects) ambayo ilitolewa wakati JPM akiwa hai ilieleza mengi kuhusu Bwawa la Nyerere! Na wakati huku mitaani mkidanganywa mambo ni bam bam, ukweli ni pamoja na ufuatao:-



Wakati wewe ukiamini mipesa ipo tu kwa sababu ndivyo mlivyokuwa mnaambiwa, CAG alishindwa kuona bajeti for 2 consecutive financial years.

Bajeti ambayo CAG alithibitisha kuwepo ni kwa 2019/20 and 2020/2021 ambayo unaona hapo TOTAL ni takribani TZS 3 Trillion, wakati Project Cost ni takribani TZS 7 Trillion!

Now endelea kuamini JPM alishatenga matrilions za kumalizia huo mradi!!

Je, baada ya kazi kuanza... mambo yalienda mserereko kama mlivyokuwa mnaambiwa huku mitaani?!

Setback ya kwanza ilikuja baada ya TANESCO kumruhusu Contractor kujenga 1 Diversion Tunnel badala ya 2 kama ambavyo mkataba ulikuwa unase,a. Matokeo yake, iliponyesha mvua, na kutokea mafuriko maji yakapanda juu!



Outcome: Project ika-delay kwa miezi 5




Again, endelea kuamini kwamba angewepo JPM basi mradi ungekamilika by June 2022 wakati tayari setbacks zilishatokea tangu wakati akiwa hai huku mkiambiwa "mambo kama kawa"!!

Je, baada ya ku-delay for 5 months, ina maana mambo ndo yakaanza kwenda kwa mserereko?! CAG mnoko ambae solution yake ilikuwa kuto-renew mkataba wake anaendelea hapa chini"-


E bhana eh!

Kumbe wakati watu wanasubiria kusherehekea Mwaka 2021, mradi ndo kwanza ulikuwa umefikia 28.61%... ikiwa ni delay ya takribani 7 months.

Hapa nakukumbusha tu kwamba, hadi JPM anakutwa umauti, kuna kila dalili mradi ulikuwa hujafikia hata 35% completion rate!!

Je, shughuli zingine zilikuwa zinaenda kwa kasi?!

Summary ya project implantation ni kama inavyoonekana hapa chini:-



Kumbe hadi CAG anaingia mitamboni, kulikuwa na major project components kibao ambazo zilikuwa hata hazijaanza huku zikiwa zime-delay kwa miezi kadhaa! Kuanza kwa ujenzi wa Permanent Bridge kwa mfano, ilikuwa ime-delay kwa zaidi ya Siku 500... sasa yale ma-crane yanayotakiwa kuwekwa kwenye tunnels sijui yatapitia wapi!!

All in all, yote hayo huenda yasingekuwa big issue kama kungekuwa na pesa ya kutosha!! Na hata mwanzoni mambo yalianza kwenda fasta baada ya kuchukua syndicated loans from Trade Development Bank ($ 1 Billion) na Credit Suisse ($0.5 Billion)!

Na hii mikopo inakuja wakati tuna 2 major projects, kwahiyo kuna uwezekano mkubwa ikawa pesa inayopatikana inakuwa distributed kwenye hizo projects 2.

Mikopo mingine ambayo JPM alifanikiwa kuipata kabla hajafariki ni pamoja na mkopo wa $400 Million kutoka UBA.

Hapo ndipo tunarejea swali uliloulizwa na JokaKuu ambalo umejibu kirahisi mno... "mbona kipande cha SGR kutoka Dar to Moro tu, alishindwa kumaliza"?

Sasa endelea kusingizia Wakandarasi na akina Makamba wakati uhalisi ni kwamba, hata wakati JPM anaaga dunia, bado sehemu kubwa ilikuwa haijafanyika!!
 
Jadili hoja yangu. Nimesema muda wa mradi na si whether mradi ni mzuri au mbaya. Jaribu kufuatilia miradi mikubwa kama hiyo duniani ilikamilika kwa muda gani na pia fuatilia mkandarasi huyo kama amewahi kujenga miradi mingapi ya ukubwa huo ili kufahamu capacity yake. Serious companies hasa za ulaya ziliogopa ban kutokana na mradi kwenda kinyume cha mazingira as sehemu ulipo ni hifadhi ya kidunia na hata report yake (ya feasibility) ilikuwa too old.

Kwa maoni yangu, muda wa mradi haukuwa realistic. Ni yale mambo yakuwaambia wataalam kisiasa tu kuwa "mimi nataka miezi 36" utafanyaje, utajua wewe then wataalam wanaenda kuweka kwenye zabuni muda huo , kwa uoga tu kwa kiongozi. Sasa subiri tutauona muda halisi considering pia kama kuna ucheleweshaji wa malipo kama upo.
 
Kwani wahusika wanasemaje kuhusu lini bwawa linategemewa kumalizika kujengwa?
 

Hizo jerojero zinamtosha Joyce mpelekeeni.
Siku za nyuma tuliambiwa tutapata umeme utokanao na gesi kwa bei rahisi nadhani wewe ulikuwa bado mdogo
 
Umeme unaotarajiwa kuzalishwa na JNHP ni MW 2,115 tu kwa nini kila mtu anafikiri umeme huo ndio utakuwa mwingi na kuwa na kiwango (bei nafuu) kwa matumizi ya jamii na viwanda, wakati Tanzania inahitaji kuwa na umeme wa zaidi ya MW 5000. Hivyo ina maana hata bwawa la Nyerere likimalizika bado mahitaji ya umeme ni makubwa na itabidi umeme wa gesi au vyanzo vyengine vitumike.
 
Halina baraka ya mabeberu wanaotaka kulinda ikolojia ya Selous.
 
Tuliza mshono, kma vipi kamfuate kaburini umueleze huu upuuzi wako
 
Lakini kweli. Alikuwa mtu wa vitendo. Vitendo vya kupoteza watu, hawajaonekana mpaka leo. Kutesa. Kuzuia watu wasiseme. Kutoa takwimu za uongo. Kukanusha milipuko ya mgonjwa.
Vilikuwa vitendo kweli kweli.
 
TUNASHUKURU KWA MAJEDWALI. Tunahitaji umeme wa bei nafuu na MRADI HUU UKAMILIKE KABLA YA UCHAGUZI UJAO. HIYO GESI MUIUZE KAMA NI YETU. Hatuwezi kununua umeme wa gesi wa gharama kubwa wakati huu wa bwawa ni nusu ya bei. GESI ITANUNULIWA KWA WINGI MAANA HUKO WANAWEKEANA VIKWAZO VYA KUUZIANA.
 
Mbona SGR kipande cha Dar to Moro kilimshinda kumaliza?
Mjomba Magu kwa SGR alichemsha sana,
Alikuwa hana plan ya mradi,mwanzo ilikuwa Dar hadi Moro,tena diesel locomotive.Mara akanogewa na mwendokasi ya umeme.Mara akataka ifike Dodoma.Novfinancial plan je hiyo pesa ataipata wapi?Akabaki anasema tutaijenga kwa pesa zetu kwa miaka mingapi?
Hata hilo bwawa la Mwl.Nyerere alichemka kwa kuteuwa mkandarasi fake.
Huyo Arab Contractor wa Misri hana sifa za kujenga mradi mkubwa,kwani hata Asswan dam anayojivunia yeye kama yeye hakujenga bali mafundi wa SOVIET "Urusi kishoka"
Mapungufu ya mkandarasi yamekuwepo toka day one lakini kwa kuwa mradi una elements za kisiasa wakubwa kama Waziri Mkuu walionekana kulalamika kimafumbo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…