Anguko la Diamond ni sawa na "Mr nice"

Anguko la Diamond ni sawa na "Mr nice"

Habari zenu wakuu.
Kwa jinsi upepo unavyovuma sina budi kusema kwamba huyu kijanaa mwenzetu kutoka tandale anaelekea kuanguakia pua kama ilivyotokea kwa msanii mwenzake Mr nice( Lucas mkenda),sababu kubwa itakayofanya huyu kijana wetu aanguke mshindo mkubwa ni kulewa sifa kiasi kwamba anatumia umaarufu wake kutoa nyimbo ambazo hazina viwango.
Kitu kingine ni kwamba inaonekana huyu bwana mdogo anatumia nguvu na ukubwa wa timu yake kusambaza nyimbo ambazo ziko chini ya kiwango kitu ambacho ni makosa makubwa kwasababu sisi ambao hatuna timu au hatuko kwenye timu yake ni rahisi sana kuona ubovu wa nyimbo zake kwasababu tunatumia akili zetu kuchambua tofauti na members wa timu yake ambao hutumia mihemko.
Kitu kingine anachofanya huyu kijana ambacho sio kizuri ni kutumia nguvu kubwa kwenye video ili kuficha ubovu wa audio kitu ambacho kwa upande mwingine kinapelekea kuwanyima haki ya kusikiliza mziki mzuri wale wasiotizama video zake.
Mwisho.
Diamond alikuja vizuri sana lakini huko anakoenda kuna giza nene lisiloelezeka, kwani kwa hizi nyimbo zake mbili mpya za yeye na Neyo na rich mavoko zinaashiria kwamba graph yake inashuka kwa kasi.
Namshauri aangalie sana management aliyonayo kwa sasa maana naona huyu "Salam" anafanya umbeya zaidi kuliko kazi anazotakiwa kufanya,pia ikiwezekana siku moja moja afanye nyimbo zake kwenye studio nyingine siyo kila siku "WASAFI RECORD"maana naamini hawawezi kujua kila kitu,pia aache kufanya vitu kwa mazoeya.
Bora umeongea wewe hii KOKORO hata sijaielewa yaani naona staili ya Wasafi ni ile ile tu, ukiangalia Mugachere, Kokoro........

Ngoja tuwaachie wenye Team zao bhana
 
Mkuu kweli nitasubiri sana maana KWENYE UDHIA PENYEZA RUPIA na kuhusu hilo wcb wako vizuri kwa hiyo sitoshangaa kuona hii nyimbo inaachwa tu iendelee kuonekana kwenye jamii lkn ukweli utabaki palepale kwamba haipaswi kuonyeshwa kwa tv za bongo
 
Kitu kimoja ambacho watu hawajaelewa kuhusu diamond ni kwamba jamaa anajua kuucheza mchezo...kucheza na akili za watu..naomba mtoa mada usubir miezi kadhaa utaleta feedback hapa...
 
hakuna ajuae kesho mkuu wala hakuna anaemuombea diamond anguko nampenda diamond sana mimi binafsi ila trend yake haipo sawa kama zamani au wewe unasemaje?
Nikiangalia mtazamo wako kwa diamond nadhani una lean kuto mpenda( may be ulimpenda zamani its ok)

Mimi namkubali, na nakubali akosolewe kwa nia njema, nyimbo ya Ne-yo ndio ilinistua ilikiwa chini ya matarajio yangu, ila kwengine naona ako sawa, akipotoka ntasema.
 
Ila hii video mmmh mmmh mmmh, nahisi itapigwa chini, sasa sijui nani aliitoa idea ya wale madada kuweka viplasta vya x kwenye chuchu, ila hii nyimbo nilitarajia makubwa kutoka kwao ila naipa 7/10 ila video hiiiiiiiii.................... Tusubiri tuone itakuwaje, ila nimemuona fundi mitambo kufanya yake, ktk hii video kama kule mombasa 😛😛😛. Nakuhusu diamond platnumz kushuka sitegemei, sitarajii kama hatashuka kwa Muda huu, kwani huu ni muda wake, ww endelea kupiga ramli, choma ubani lkn ni wakati wake, maneno haya toka 2014 mpaka hivi leo yashazunguzwa sana lkn bado namba moja, najua muda wake wakushuka utafika ila sio sasa na usitegemee atatetereka kiuchumi, muundo na mfumo wakikampuni aliojijengea diamond platnumz ndio utakaomuingizia ela mpaka anakufa kama alivyo AY.
 
Habari zenu wakuu.
Kwa jinsi upepo unavyovuma sina budi kusema kwamba huyu kijanaa mwenzetu kutoka tandale anaelekea kuanguakia pua kama ilivyotokea kwa msanii mwenzake Mr nice( Lucas mkenda),sababu kubwa itakayofanya huyu kijana wetu aanguke mshindo mkubwa ni kulewa sifa kiasi kwamba anatumia umaarufu wake kutoa nyimbo ambazo hazina viwango.
Kitu kingine ni kwamba inaonekana huyu bwana mdogo anatumia nguvu na ukubwa wa timu yake kusambaza nyimbo ambazo ziko chini ya kiwango kitu ambacho ni makosa makubwa kwasababu sisi ambao hatuna timu au hatuko kwenye timu yake ni rahisi sana kuona ubovu wa nyimbo zake kwasababu tunatumia akili zetu kuchambua tofauti na members wa timu yake ambao hutumia mihemko.
Kitu kingine anachofanya huyu kijana ambacho sio kizuri ni kutumia nguvu kubwa kwenye video ili kuficha ubovu wa audio kitu ambacho kwa upande mwingine kinapelekea kuwanyima haki ya kusikiliza mziki mzuri wale wasiotizama video zake.
Mwisho.
Diamond alikuja vizuri sana lakini huko anakoenda kuna giza nene lisiloelezeka, kwani kwa hizi nyimbo zake mbili mpya za yeye na Neyo na rich mavoko zinaashiria kwamba graph yake inashuka kwa kasi.
Namshauri aangalie sana management aliyonayo kwa sasa maana naona huyu "Salam" anafanya umbeya zaidi kuliko kazi anazotakiwa kufanya,pia ikiwezekana siku moja moja afanye nyimbo zake kwenye studio nyingine siyo kila siku "WASAFI RECORD"maana naamini hawawezi kujua kila kitu,pia aache kufanya vitu kwa mazoeya.
Mkuu umeandika assumption tu.. Au ndoto ya mchana..
Am not team Diamond.. Wala c shabiki wa Diamond but I respect akili yake ya biashara kimuziki..
Ukikosoa Siku nyingine njoo na fact.. Na statistics pamoja na mifano ya kutosha..
Nyimbo mbaya.. Hujataja hata moja...
Wasikilizaji wa audio vs watazamaji wa video.. Tupe numbers.. Ama takwimu.. Ukishindwa hata makadirio..
And last.. Uckarir mambo.
 
Lazma tukubali diamond ni mwanamziki mzuri lkn kuna haya ya kufanyia kazi kwenye hizi nyimbo mbili ya neyo na mavoko.
1. Uandishi apunguze kurudiarudia maneno na idea mfano wimbo wa neyo na ule kwenye video yuko na Avril. Zote idea nataka nikuoe nikupeleke nyumbani.
2. Beat na melody ziko kinaigeria sana anakosa identity sababu style za wanaigeria wako wengi sana.
3. Producer anagonga beat zinafanana sana at least awe nao zaidi ya wawili kutofautisha ladha.
4. Staha za video. Sidhani km hawakufikilia basata watawamind. Kuwaweka wadada kwenye mabeseni maziwa nje nikuwazalilisha wanawake na ninje ya utaratibu wetu.

Sio lazma ashindwe hatumuombei lkn akubali critcizm zenye kujenga.
Kuhusu kushuka kimuzik hakuna mtu aliyeishi milele au kuhit milele unawasahau kina defao, kina pepekale kina kofii kina Michael Jackson kila mtu anazama zake hizi nizama za Diamond lkn azingetie ushauri.
All in all Nyimbo hizi hazina kipya hata hazifikii kina INDe,
Lkn Najua Clouds wapo na hizi nyimbo zitakuwa kubwa regadless na uzuri au ubaya wake.
 
Tatizo ni lugha tu wadau.....
Ngoma zote, za mond sehemu anazotumia lugha nje ya kiswahili inaonekana mashairi kapuyanga.
Vionjo kubadilika cjui kama tekno,ngoma haina ladha ya ki-tz, hiyo ni ''marketing target'' wanawaza mangoma yatakayohit abroad ili wakapige show za bei mbaya.
TRUST ME MYFRIEND AND TIME WILL TELL US THIS SONG WILL GIVE RICH MAVOKO MORE INTERNATIONAL STANDARDS
 
Wimbo wa rich mavoko ni mzuri ila diamond ndo amefanya uwe wa kawaida!. Ameimba kwa mazoea na hakuna kupya alichofanya kwenye huo Wimbo! . Kwa lugha nyepesi Rich Mavoko amemfunika boss wake.bora rich angefanya mwenyewe.
Diamond na alikiba style zao hazibadiliki ivyo wanakuwa wabazoeleka masikioni hata wakitoa Wimbo huusikii km mpya.mfn Wimbo wa alikiba na ommy dimpos ni Wimbo Mzur ila style ya alikiba Ile ile.jike shupa Wimbo Mzur ila style Ile ile. ..soon utakuta hawa alikiba na diamond ndo wanabebwa na collabo.
Wimbo wa mwisho mzuri alikiba kutoa ni ule naghalamia na Christian Bella,Wimbo wa mwisho diamond kutoa mzuri ni let me sing na AKA wa S.a
 
Kateleza kidogo blaza ila sehem ya mfano wako haukufanyi Akili nyingi
 
Hizi wahenga wanaita dua za kuku kamwe haziwezi mpata mwewe...na watu wanasahau kadri mnavyo muombea mabaya ndivyo Sir God anavyozidi kum'bariki...Muda wake wa kushuka utafika ila sio sasa,na maneno mnayo muombea yanamfanya akomae zaidi kwenye game...km kweli mnataka ashuke ni bora mkae kimya ajisahau ashuke mwenyewe,mnachokifanya ss ni sawa na kumshtua shtua mtu anaetaka kulala...atakaza jicho balaaa na mwisho wa siku utalala ww unae mwamsha..ila all in all hii Ngoma ya rich mavoko itampeleka rich kimataifa wakapige dolari..na nnadhani target yao ni huko sio vituo vya runinga vya kibongo...
 
Copy
1479849384155.png

Paste
1479849473065.png
 
Hizi wahenga wanaita dua za kuku kamwe haziwezi mpata mwewe...na watu wanasahau kadri mnavyo muombea mabaya ndivyo Sir God anavyozidi kum'bariki...Muda wake wa kushuka utafika ila sio sasa,na maneno mnayo muombea yanamfanya akomae zaidi kwenye game...km kweli mnataka ashuke ni bora mkae kimya ajisahau ashuke mwenyewe,mnachokifanya ss ni sawa na kumshtua shtua mtu anaetaka kulala...atakaza jicho balaaa na mwisho wa siku utalala ww unae mwamsha..ila all in all hii Ngoma ya rich mavoko itampeleka rich kimataifa wakapige dolari..na nnadhani target yao ni huko sio vituo vya runinga vya kibongo...
Huko kimataifa amefika ukingoni kwakuwa ameanza kuwacopy hao wa kimataifa.
Ukimcopy mtu utaweza kushindana naye kwenye soko moja?
 
Kila nyimbo ya diamond ikitokaga..utabiri huu unakuepogo..subiri tu utaona..time will tell
 
Back
Top Bottom