Orketeemi
JF-Expert Member
- Feb 12, 2013
- 5,063
- 12,866
Wadau wa soka Tanzania salami kwenu.
Kwa waliofuatilia press mbili , moja ya Mo Dewji siku anaonesha Hundi ya Bilion 20 na press ya Leo ya Semaji Lao Haji Manara watakuwa wameona kitu kinaenda kutokea Msimbazi na anguko Lao lipo jirani Kwa sababu zifuatazo.
1. Uwekezaji wa Mo Dewji pale Simba umekaa Kimagumashi zaidi. Moa Dewji yupo Simba kiujanja ujanja sana na moja ya ishara NI kauli anayoirudiarudia kwamba pale Simba yeye hapati faida. Huu ni ujanja na umagumashi.
2. Kuondoka Kwa Haji Manara. Huyu ni kipenzi cha wana Simba kuliko hata Mo mwenyewe. Ushahid NI maneno ya Haji kuwa Mo amewahi mpigia sim na kumwambia watu Wanasema Haji ni maarufu kuliko Mo. Lakini pia ni mara nyingi wanaSimba wamekuwa wakitaka Mo aondoke Simba lakini hawajawahi kutaka Haji aondoke.
3. Uwepo wa Barbra . Huyu bosi inaonekana yupo pale Kwa kazi maalum ya kuhakikisha analinda maslahi ya Mo klabuni na ndio maana anafanya kila analoweza kuhakikisha hili. Barbara anamtumikia Mo na si Simba.
4. Presha ya matokeo. Kuondoka Kwa Haji Manara kumezidisha presha ya matokeo pale Simba hasa katika michuano ya kimataifa. Haji Manara alikuwa na mchango mkubwa wa kuwajenga wanaSimba Kisaikolojia kitu ambacho Kamwaga hana kipaji hicho. SIMBA itapofanya vibaya itaonekana hamasa ndani ya timu imeshuka na Simba imepoa.
5. Utamaduni wa soka la Tanzania. Ilivyo miaka nenda rudi mapacha wa kariakoo hupeana zam za kutamba na hapajapata kutokea mapacha hawa wakawa na mafanikio Kwa wakati mmoja. Hili japo ni dogo Ila linaleta dalili za anguko la Simba.
Kwa waliofuatilia press mbili , moja ya Mo Dewji siku anaonesha Hundi ya Bilion 20 na press ya Leo ya Semaji Lao Haji Manara watakuwa wameona kitu kinaenda kutokea Msimbazi na anguko Lao lipo jirani Kwa sababu zifuatazo.
1. Uwekezaji wa Mo Dewji pale Simba umekaa Kimagumashi zaidi. Moa Dewji yupo Simba kiujanja ujanja sana na moja ya ishara NI kauli anayoirudiarudia kwamba pale Simba yeye hapati faida. Huu ni ujanja na umagumashi.
2. Kuondoka Kwa Haji Manara. Huyu ni kipenzi cha wana Simba kuliko hata Mo mwenyewe. Ushahid NI maneno ya Haji kuwa Mo amewahi mpigia sim na kumwambia watu Wanasema Haji ni maarufu kuliko Mo. Lakini pia ni mara nyingi wanaSimba wamekuwa wakitaka Mo aondoke Simba lakini hawajawahi kutaka Haji aondoke.
3. Uwepo wa Barbra . Huyu bosi inaonekana yupo pale Kwa kazi maalum ya kuhakikisha analinda maslahi ya Mo klabuni na ndio maana anafanya kila analoweza kuhakikisha hili. Barbara anamtumikia Mo na si Simba.
4. Presha ya matokeo. Kuondoka Kwa Haji Manara kumezidisha presha ya matokeo pale Simba hasa katika michuano ya kimataifa. Haji Manara alikuwa na mchango mkubwa wa kuwajenga wanaSimba Kisaikolojia kitu ambacho Kamwaga hana kipaji hicho. SIMBA itapofanya vibaya itaonekana hamasa ndani ya timu imeshuka na Simba imepoa.
5. Utamaduni wa soka la Tanzania. Ilivyo miaka nenda rudi mapacha wa kariakoo hupeana zam za kutamba na hapajapata kutokea mapacha hawa wakawa na mafanikio Kwa wakati mmoja. Hili japo ni dogo Ila linaleta dalili za anguko la Simba.