popo1986
JF-Expert Member
- Jul 30, 2014
- 1,120
- 372
HEBU MFAHAMU MZEE AKILIMALI.HISTORIA YAKE NA IMEKUAJE AWE NA SAUTI KATIKA KLABU YA YANGA?
1. Jina lake kamili ni Ibrahim Omary Akilimali, mzaliwa wa Kigoma.
2. Ameanza kuishabikia Yanga mwaka 1956, aliipenda Yanga kwa kuwa ina neno Afrika yaani "Young African". Pia baba yake alikuwa shabiki mkubwa wa Yanga hivyo pia alishawishiwa.
3. Alikuja Dar mwaka 1966, mwaka 1967 akapata kazi Bandarini ya ukuli "kubeba mizigo".
4. Mwaka 1972 alifanikiwa kupata kadi yake ya uanachama wa Yanga SC.
5. Wakati Anaingia Yanga alilikuta baraza la tochi ambalo sasa wanajiita baraza la wazee. Kazi kubwa ya baraza la tochi ilikuwa kuchunguza maadui wa Yanga.
6. Akishirikiana na Salum Mwaipande waliunda Yanga asili kuupinga uongozi wa Jabiri Katundu na katibu wake George Mpondela waliokuwa wakitaka kuifanya Yanga iwe kampuni. Uongozi wa Katundu ndio uliojenga lile jengo yalipo makazi ya Yanga na uwanja wa Kaunda.
7. Mwaka 2006 mgogoro wa Yanga kampuni na Yanga asili ulimalizwa baada ya viongozi wa pande zote kupatanishwa na Yusuff Manji.
8. Akilimali ni kiongozi wa kamati ya mziziology. Hii ni kamati inayohusika na matambiko, utukuzaji na utoaji wa baraka za kimila kwa timu.
9. Maamuzi yoyote ya kamati ya utendaji lazima yapitia baraza la wazee ili kupewa baraka.
Pichani:
23. 05. 2015 Mzee Akilimali akiomba kibali cha maandamano polisi ili waruhusiwe kuandamana hadi zilipo ofisi za Mengi kwa dhumuni la kumpinga Mengi ambaye alikuwa anazua chokochoko dhidi ya Manji. Leo hii baada ya Manji kuandaa mkakati wa kuziba mirija ya wachache kujipatia pesa kupitia Yanga, Mzee Akilimali yupo upande wa Mengi na anamchafua Manji.
Wananchi huyu mzee ni nani mpaka atake kuiharibu Yanga yetu.
Copy and paste. From facebook.
My take:
Simba itasimama sana imara jaa kuwa haina wazee kama hawa na pia mambo ya matambiko ni laana kubwa ni sawa na kumkabidhi shetani timu, msizani sisi tunaofanya ibada za kweli tutawaombea, NO kwakuwa mmeamua kuwa na hao wazee akina Akilimali basi kaeni nao, sisi wengine tutabakia kushabikia tu.
1. Jina lake kamili ni Ibrahim Omary Akilimali, mzaliwa wa Kigoma.
2. Ameanza kuishabikia Yanga mwaka 1956, aliipenda Yanga kwa kuwa ina neno Afrika yaani "Young African". Pia baba yake alikuwa shabiki mkubwa wa Yanga hivyo pia alishawishiwa.
3. Alikuja Dar mwaka 1966, mwaka 1967 akapata kazi Bandarini ya ukuli "kubeba mizigo".
4. Mwaka 1972 alifanikiwa kupata kadi yake ya uanachama wa Yanga SC.
5. Wakati Anaingia Yanga alilikuta baraza la tochi ambalo sasa wanajiita baraza la wazee. Kazi kubwa ya baraza la tochi ilikuwa kuchunguza maadui wa Yanga.
6. Akishirikiana na Salum Mwaipande waliunda Yanga asili kuupinga uongozi wa Jabiri Katundu na katibu wake George Mpondela waliokuwa wakitaka kuifanya Yanga iwe kampuni. Uongozi wa Katundu ndio uliojenga lile jengo yalipo makazi ya Yanga na uwanja wa Kaunda.
7. Mwaka 2006 mgogoro wa Yanga kampuni na Yanga asili ulimalizwa baada ya viongozi wa pande zote kupatanishwa na Yusuff Manji.
8. Akilimali ni kiongozi wa kamati ya mziziology. Hii ni kamati inayohusika na matambiko, utukuzaji na utoaji wa baraka za kimila kwa timu.
9. Maamuzi yoyote ya kamati ya utendaji lazima yapitia baraza la wazee ili kupewa baraka.
Pichani:
23. 05. 2015 Mzee Akilimali akiomba kibali cha maandamano polisi ili waruhusiwe kuandamana hadi zilipo ofisi za Mengi kwa dhumuni la kumpinga Mengi ambaye alikuwa anazua chokochoko dhidi ya Manji. Leo hii baada ya Manji kuandaa mkakati wa kuziba mirija ya wachache kujipatia pesa kupitia Yanga, Mzee Akilimali yupo upande wa Mengi na anamchafua Manji.
Wananchi huyu mzee ni nani mpaka atake kuiharibu Yanga yetu.
Copy and paste. From facebook.
My take:
Simba itasimama sana imara jaa kuwa haina wazee kama hawa na pia mambo ya matambiko ni laana kubwa ni sawa na kumkabidhi shetani timu, msizani sisi tunaofanya ibada za kweli tutawaombea, NO kwakuwa mmeamua kuwa na hao wazee akina Akilimali basi kaeni nao, sisi wengine tutabakia kushabikia tu.