Njia rahisi na ya haraka ni M-Pesa,TigoPesa, Airtel Money nk Maoni yangu lakini Kukiwa na uaminifu wa hali ya juu...Tuanze tu, maana tayari wanafunzi kadhaa waliotangazwa kurudishwa nyumbani kwa kukosa ada ama sifa walikuwa zaidi ya elfu kumi (10,000) wengi sana hawa kuwapoteza bilaujuzi wala sifa za kitaaluma. Hiki kijiwe cha JF kikianza tunaweza kukusanya zaidi ya m400 kwa mchango wa elfu moja tu. Tuwaombe moderators wa jukwaa watusaidie...tuweke akaunti ya kutuma. Ili ikiwezekana mhula mpya unapoanza tuwe na kitu cha kuwapa walengwa. Itakuwa thawabu kubwa kwa nchi yetu, kumsaidia mtu kujisaidia. Asante sana kwa maoni haya.
Njia rahisi na ya haraka ni M-Pesa,TigoPesa, Airtel Money nk Maoni yangu lakini Kukiwa na uaminifu wa hali ya juu...
Wazo zuri sana mfuko uitwe Anna Mghwira Education Support Trust Fund( AESTF) nitawaambia rafiki zangu pale kwa Mfalme kule redsea
Asante kwa maoni na mchango wako,
Ahsante mama na tunasubiri pia tunawaombea huo utaratibu uwe na uwepesi kutoka taasisi husika...Tayari tuna mawasiliano na mitandao hii na taratibu zikikamilika tutajulishana. tutatakiwa pia kuwa na akaunti ya benki.
AFYA YA KINYWA NA MENO
NAPOKEA MASWALI NA USHAURI
Asante kwa maoni na mchango wako,
Asante Mboboyu kwa ufafanuzi. Uzi huu ubaki kwa suala la mfuko wa elimu ili kusaidia mjadala uendelee kwa ufanisi.Mkuu, huu uzi ni maalumu na wenye maudhui tofauti na ulichokiwasilisha, hapa tunaangalia ni namna gani kama jamii tunaweza kuunganisha nguvu kuwachangia vijana wetu/wenzetu wanaojiunga na elimu ya juu lakini wananshindwa kumudu gharama za masomo hayo. Tunatambua jitihada za serikali katika hili, lakini mahitaji ni makubwa mno kuliko uwezo wa bodi ya mikopo kwa sasa, kama wadau wa elimu na wana jamii huwa tunakutana kwenye uzi hii kuona nini tunaweza tukafanya ili ama kupunguza au kuondosha kadhia hii kwa wanafunzi wetu.
Jambo lako ni muhimu sana, bila shaka sote tunatambua kwamba MTU NI AFYA, bila afya njema kama jamii hatuwezi kujiletea maendeleo na hata kuyafurahia vizuri matunda ya maendeleo tuliyoyafikia, basi nakuomba ulipeleke hilo suala lako kwenye jukwaa la afya, jukwaa la matangazo madogomadogo au kwenye jukwaa la habari na hoja mchanganyiko. Tunathamini sana mchango wako, na pia kwa niaba ya wadau wengine wa elimu nikukaribishe kwa mchango wako (pale tutakapoanza) ili tuwasaidie vijana wetu/wenzetu walio masomoni.
Asante.
Mama naomba msichelewe sana kukamilisha hiyo mipango ili tujue tunaanzaje kuchangia, tazama bado miezi michache tu mnamo mwezi Oktoba tutapata kundi lingine la wahitaji ambao ndio watakua wanaanza masomo yao. Natambua umuhimu wa maandalizi mazuri, najua yanahitaji muda na umakini, lakini ni lazima muangalie muda wa maandalizi usiutumie muda mwingi wa kukusanya michango.
Kila la heri.
Analyst, hili ndilo lngo lake, ikiwezekana tuondokane kabisa na kuwana kadala raia wasio na elimu kwa sababu ya kukosa ada!Hili ni wazo zuri sana mama.
Huu ni wakati muafaka kwa kila mtanzania kuachana mara moja na utamaduni wa kuchangia harusi na sherehe nyingine zisizokuwa na tija kwa taifa na kuhamia kwenye kuchangia elimu kwa Mtanzania kwa manufaa ya Tanzania ya baadae.
Hakika wazo hili kama likipata msukumo unaostahili, tunaweza tusije kuzungumza tena hapa juu ya watoto wenye ufaulu wanaoshindwa kutimiza ndoto zao za kupata elimu ya juu.
Pesa hii ikishakuwepo, itatolewa kwa walengwa on academic merits. Kulingana na kiasi kitakachokuwepo, itasetiwa cut-off point ya mtoto atakaekuwa eligible kupata hiyo scholarship.
Tujitahidi lisipotee!Mama Anna;
Umetoa wazo zuri sana! Umetoa mwelekeo..!
Humu najua watu wataliunga mkono kwa maneno tuu na pongezi kwa wazo zuri..
Nilifikiri huu wito ungefanya event kabisa ili uliadress vizuri..either uitishe Press au kitu kama fundraising na kuwaalika watu wote walengwa..
Humu kuna members kama 400,000 hivi...bado tunataka ifike kwa watu zaidi hata watu 24milion ambao ni nusu ya Population yetu...
Ikiwezekana zihusishwe Taasisi tuu, watu binafsi na NGOs ! Serikali ikae pembeni manake wataleta siasa..! Hili suala wameshindwa kwa sababu watu wako after political gain..
Leo tukishindwa kusomesha hiki kizazi..miaka 50 ijayo hili taifa litapotea kabisa..
[HASHTAG]#Elimukwanza[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Uzalendokwanza[/HASHTAG]
[HASHTAG]#Mikopo[/HASHTAG] elimu ya juu
Mama Umenifariji. Nikiwa miongoni mwa waliokosa mkopo mwaka jana huku nimekidhi vigezo vyote, hapa umenifariji na nayaona tena matumaini.
Mungu akuzidishie baraka kwa bandiko hili lenye mashiko.