Awali ya yote napenda kutanguliza shukrani zangu za dhati kwa watanzania wote mlioanza kulifuatilia pambano hili siku 3 zilizopita ama masaa machache kabla ya mpambano kuanza, hivyo kikubwa mlicho kiona kwenu ni kushabikia rangi ya mwili tu.
Niwashukuru pia kwa mayowe makali mliyopiga kutoka kila pande ya jiji la Dar na kuashiria kuwa bado mnamchukia Mzungu ati kisa tu aliwatawala.
Wengi wenu sio wapenzi wa mchezo wa Ndondi kwa sasa na miaka ya hivi karibuni. Wengi wenu hamumjui Wladimir Klitschko na wala hamumjui Antony Joshua...ila tu kwa kuwa mmekuta ndio jambo lililo na kick Duniani basi na nyie mkatumbukia na kushabikia kuliko hata wale mlio wakuta.
Nirudi kwenye pongezi kuu na za pekee ambazo zinakwenda kwa mwana Masumbwi Wladimir Klitschko ambae ndie bondia wa uzito wa juu kipenzi cha wengi Duniani kwa sasa. Bondia huyu mwenye rekodi ya kumiliki mkanda wa Uzito wa juu wa Dunia kwa miaka 9 mfululizo ni bondia bora kabisa ambae ameweza kuusimamisha uzito wa juu wa mchezo huu uwe na heshima. Pongezi hizi kwake ni kitendo chake cha kuomba haraka pambano la marudiano kati yake na bondia mchanga asie na jina wala mashabiki katika kila kona ya Dunia Antony Joshua.
Wladimir Klitschko Usiku wa kuamkia hii leo amepoteza pambano lake dhidi ya bondia huyo aliekuwa anapambana kwenye ardhi ya kwao, huku akishangiliwa na maelfu ya raia wenzie, lakini cha kuchosha zaidi ushindi huo amekwenda kuupata kwenye liuwanja la Mpira, mbaya zaidi ushindi huo wa bahati ameupata huku Wladimir Klitschko akiwa anaongoza kwa pointi nyingi tu.
Kwa kuonesha wazi kuwa yeye ni bora zaidi, bondia Wladimir Klitschko alimtwanga gumi moja takatifu na kufanikisha kumlambisha dogo ardhi ya nchi yake...kwa wanaojuwa masumbwi na kumjuwa Wladimir Klitschko basi ni wazi kabisa tunafahamu kuwa pambano liliishia pale. Ujasiri wa dogo kukomaa na pambano ni kutokana tu na makelele ya raia wenzake ambao waliuvaa uzalendo kabla hata mabondia hawa hawajapimwa uzito.
Katika mapambano machache aliopambana, Bondia huyu Antony Joshua alikuwa akiringa kuwa hajawahi kupigwa jeb mpaka kuanguka chini, lakini rekodi hio kwa sasa hana tena, na amebaki nayo kaka yake Wladimir Klitschko ambae katika kupigana kwake masumbwi kote mpaka alipo stahafu hakuwahi kuangushwa, huyu anajulikana kwa majina Vitali Klitschko ambae alikuwa bingwa wa Dunia wa Uzito wa Juu kwa mikanda yote, kabla ya kuja muachia mdogo wake Wladimir Klitschko.
Kwa watu wanaoujuwa mchezo huu wa masumbwi, sambamba na kumjuwa Wladimir Klitschko tunajuwa nini kitaenda mpata dogo Antony Joshua katika mechi ya marudiano. Mbaya zaidi kwa dogo huyu ni kwamba kama akijidanganya na kukubali kwenda kurudiana na Nguli huyu katika Ardhi ya Marekani ama iwe Madison Square Garden, ama iwe Trump Tower basi ni lazima apokee kipigo ambacho waingereza wenzie hawatakuja kukisahau. Kwenye ardhi ya marekani kuna watu wanaojuwa Ndondi na sio wapiga makelele ambao wengi wao walikuwa walevi na cha msingi kwao ni utaifa.
Namuonea huruma Joshua kama atakubali kusaini kupambana na Wladimir Klitschko katika ukumbi wa MGM Grand uliopo Las Vegas Nevada nchini Marekani, kwani umauti waweza mkuta humohumo.
Katika ukumbi huu wa kihistoria, dogo huyu Joshua atashangiliwa TU atakapo fanya shambulizi la maana mwilini mwa Wladimir Klitschko, kitu ambacho sioni kama kina nafasi siku hio. Dogo anatakiwa ajiulize kwanini bondia Muingereza mwenzie Tyson Furry alikuwa yupo tayari hata kufungwa jela ili tu asirudiane na Klitschko. Furry alijitetea na kukataa katakata kurudiana na bondia huyu na kusema kuwa yeye binafsi anatumia Madawa ya kulevya hivyo hawezi kupigana tena na Wladimir Klitschko .
Katika Ukumbi wa MGM ukumbi ambao Wladimir Klitschko hupendelea zaidi na zaidi kuvaa bukta yake nyekundu na Gloves nyekundu hakuna alietoka akiwa salama, kuna ambao walishindwa kuongea baada ya pambano, kuna walio ng'oka meno, kuna walio vunjwa taya, lakini hakuna ambae alitoka bila kuchanwa usoni na kutolewa damu...
Gang Chomba