Antony Joshua Vs Andy Ruiz 2, tukutane hapa kwa updates

Pambano limekosa msisimko.Nilitegemea kungekua na ngumi za hatari ila imekua kinyume chake.
Kiongozi! Siyo pambano la kuuana jombaa!

Andy ana ngumi nzito, ana head movement nzuri na mikono yake miyepesi na anarusha ngumi kwa kasi.

Andy ni killer machine. Ukimsogelea anakuua kwa sekunde chache tu!

Kinachotafutwa ni point! Joshua kapigana very good technically.. Ijapokuwa alikuwa anajisahau kwa sekunde kadhaa..

Na boxing ndivyo inavyosema! Mpinzani wa namna hiyo muhame! Ukisimama naye sura kwa sura utafia ulingoni.
 
Kabisa hakuna mshikemshike kama zamani mpaka inashangaza kwakweli yani.
 
MCHEZO WA NGUMI HAUFANYIKI NDANI YA SHUKA tunauona live , hizi mambo mnatuambia kila siku hatujui eti kisa ngumi za kichwa

Tuliwezaje kuwashabikia akina MIKE IRON TYSON?

Nia ni kushinda au??
Kama nua ni kushinda lazima atumie advantage alionayo
Na luiz ilibidi ajaribu kumuweka kwenye advantage alionayo
Shida nn hasa??
 
Hakuna utamu wa ngumi inapendeza kupigana kwa ushindani siyo kurukaruka na kushika kila mara mpaka inachukiza mmexico kacheza vyema tena kwa kujiamini bila kurudi nyuma.
Kiongozi! Umeshawahi kujifunza mchezo wowote wa ngumi?

Iwe Karate, Kung fu, Muay Thai au Boxing?

Siyo kila mpinzani unamuingia tu wengine ni hatari watakumaliza!

Inakubidi utumie mbinu na ufundi wa hali ya juu. Ndicho alichokifanya Joshua!

Andy ni killer machine, ukisimama naye ngumi kwa ngumi anakumaliza!
 
Nilipenda JOSHUA ashinde ila sijaridhika, KO ndio ulikuwa ushindi wa maana hapa, hawa wote kwa Wilder hawavuki round ya 6
 
Kinachoharibu ladha ya boxing ni uoga... AJ usiku wa leo alikuwa amejaa uoga..
Amekimbia sana. Hakujiamini kabisaaa
Zile zinaitwa mbinu na ufundi!

Unakumbuka pambano la ufunguzi la Mwakinyo yule jamaa aliyepigana na Mfaume? Mfaume ni bondia hatari sana! Cha kwanza anajua ngumi vizuri, pili haogopi anakufuata tu! Tatu ambayo ni hatari zaidi ngumi yake ya mkono wa kushoto ni nzito sana!

Alimpiga kama siyo mtoto basi ni mdogo wa Matumla mpaka fuvu la kichwa likaweka nyufa kwa ngumi yake ya mkono wa kushoto. Matumla mwenyewe alivyoingia gym alisikia jinsi punching bag inavyopigwa alishtuka! Kuangalia ni Mfaume.

Bondia kama Mfaume ukipigana naye utumie mbinu na ufundi. Kichwa kichwa anakumaliza na ataleta madhara makubwa kwenye mwili wako. Ukiangalia pambano la ufunguzi mpinzani aliyepigana na Mfaume alikuwa anamuhama Mfaume upande wa kushoto.

Wapinzani wengine si wa kawaida ukifanya masihara utafia ulingoni.
 
Kinachoharibu ladha ya boxing ni uoga... AJ usiku wa leo alikuwa amejaa uoga..
Amekimbia sana. Hakujiamini kabisaaa
Yule jamaa huwezi kumpiga kwa kumfata. Hata awe Wilder atatia aibu! Yule ni kumshinda kwa mbinu.
 
Yule jamaa huwezi kumpiga kwa kumfata. Hata awe Wilder atatia aibu! Yule ni kumshinda kwa mbinu.
Hii mbinu akitumia kwa Wilder haitafanya kazi.

Wote warefu kwa hiyo ni rahisi ngumi ya Wilder kufika , halafu kingine Wilder kukuvaa haoni hasara.
 
Joshua muoga sana tena sana ndio kashida ila nadhani alikuwa anaogopa kupoteza tena .Chibonge mpambanaji ...
 
Angalau wewe unazijua ndondi, naona watu walitaka "ladha" bila kuangalia technics za mchezo. Kuna watu ukiwaendea kichwa kichwa wanakumaliza.

Hata Tyson aligongwa kwa style hii hii na Lewis.
 
Joshua aliinngia kwa tahadhari sana...amepigana kwa technic amekuja hawezi kumpiga kwa KO.
Hata yeye mwenyewe Andy Luiz amekubali kasema mistake zake mwenyeji.
Hata Wilder kama atapigana na Luiz then akawa nae karibu basi Wilder anaweza kupigwa!
Wilder hawezi kupigwa na Ruiz , tena atashinda kwa K.O kabisa.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…