Application za kukopesha za simu, kuhack majina ya simu za mteja bila ruhusa tofauti zile ambazo umewapa kama wadhamini

Application za kukopesha za simu, kuhack majina ya simu za mteja bila ruhusa tofauti zile ambazo umewapa kama wadhamini

Ndio Ninachosema.
Ni kweli wana vibali lakini kuna ufake ndani yake ili kuizunguka serikali na kujificha.
Kampuni zingine zina app zaidi ya 10. Niliona sms zile za matangazo. SMS moja imemaliza kwa kutaja app zake.
Siku moja nilishangaa kupigiwa simu na namba moja ambayo niliwasiliana nayo back days kuhusu deni la app fulani. Siku hiyo napigiwa kuhusu kukumbushwa kulipa mkopo kwenye app nyingine. The same number.
Wahudumu kila siku wanabadilishiwa simu za kupigia wateja.
Wakiharibu sana wanabadili jina la app. Mfano M loan sasa wameibadili na kujiita Swift money, hawa ndio baba wa kudhalilisha wateja pamoja na app zingine zinazomilikiwa na kampuni moja.
Ndio kampuni yenye mtaji mkubwa, wanakopesha mpaka milioni 3 kwa app moja ukiwa mteja wao uliyelipa kwa mda wanaoutaka wao.
Ila riba zao ni haramu , 50% ulipe kwa siku 5 ni kweli?
Laki 5 unajikuta unalipa laki 7 na nusu.
Hii mikopo naijua vizuri, walishawahi kuniharibia kisa 56, niliumia sana. Ile app nikawalipa nikawasiliana na boss wao Mkenya wakanikopesha kama milioni 2 na ushehe sijawalipa mpaka kesho.
Dawa ni wa kuwanyoosha
 
Ndio uhuni na utapeli huu na wanajificha makusudi,wanapaswa wa-declare kampuni yao na jina la app ili wabanamishwe vizuri na kushtakiwa pale wanapokosea.
Kinachoendelea kwenye hii mikopo ni uhuni kabisa tena ni ufedheheshaji wa hali ya juu sana.
 
Siyo feki.

Ilivyo ni kwamba utakuta kampuni moja ina apps nne so waweza ona umekopa kampuni nne ila ni umekopa moja.

Na pia hua wana tabia ya kutojiassociate majina na apps zao. So mfano kampuni inaitwa JF ila app wataita Kopaujidai, nyingine mkopokujigaragaza kwahiyo ukiamua kufuatilia unafuatilia mkopokujigaragaza au kopaujidai wakati mhusika wa kweli ni JF
Hawa hata ofisi zao sidhani kama ziko mahali panapojulikana
 
Back
Top Bottom