Arafat Haji: Yanga haitocheza mechi nyingine ya Derby zaidi ya hii ya March 8 katika msimu wa 2024/2025

Arafat Haji: Yanga haitocheza mechi nyingine ya Derby zaidi ya hii ya March 8 katika msimu wa 2024/2025

Smart codetz

JF-Expert Member
Joined
Jan 25, 2023
Posts
218
Reaction score
875
Ndugu Wananchi kwa dhati ya moyo wangu niwapongeze kwa kufika uwanjani kutoka kona zote nchini, mliosafiri kwa anga, mliosafiri kwa magari, mliopanda Pikipiki, mliopanda boti hadi Watembea kwa miguu, yote ni kwa ajili ya Yanga Afrika, huu sio tu upendo bali mahaba ya kulevya kwa klabu hii bora zaidi nchini.

Ndugu Wananchi poleni mno kwa kadhia ya leo, sisi kama Viongozi mliotupa dhamana kusimamia hii chapa kwa niaba yenu tumepigana, tumehakikisha mawazo yenu, matakwa yenu na sauti yenu inasikika kwa sauti ya juu sana, kwa kuheshimu mpira wa miguu na kuheshimu uthubutu wenu tuliandaa na kuleta timu uwanjani tayari kwa kushindana ila yaliyotokea yametokea.

Ndugu Wananchi, poleni kwa kupoteza muda wenu, kwa kupoteza fedha zenu kwa ajili ya mechi hii kubwa na ya kihistoria, ninyi ni sisi na maumivu haya ni yetu sote kama ambavyo tumeimba pamoja, tumelia pamoja basi hata sasa mpaka milele tupo pamoja, hilo likae vyema kwenye kumbukumbu kuwa sisi ni Yanga.

WACHEZAJI na Benchi la Ufundi, asanteni kwa heshima mliowapa Wapenzi wa soka nchini bila kujali timu zao, mmehakikisha mpira wa miguu umeshinda, kuna wakati sio suala la Mshahara wala posho bali heshima kwa nembo ya Kijani na Njano, Asanteni Vijana kwa kufika na angalau Mashabiki wameweza kuwaona na kuwalaki.

WANANCHI, mechi yetu dhidi ya Mtani wetu SIMBA imeisha leo hii kwa msimu wa 2024/25 raundi ya pili na ieleweke vyema hakutakuwa na mechi nyingine sehemu nyingine, siku nyingine na tarehe nyingine yoyote ya kuihusu Yanga dhidi ya Simba kwa Ligi kuu, iwekwe sawa kwenye kumbukumbu na ikolezwe vyema kwa wino kuwa its done and dusted, sisi tunasonga mbele na ratiba zingine.

Hii ndio sauti yenu moja, kamba moja ya DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO na tutashikilia hapo hapo Wananchi, niwatakie safari njema Wananchi wote kurejea makwenu, Mungu awalinde, awatunze mkaungane tena na familia zenu, tutakutana tena wakati mwingine panapo majaaliwa In shaa Allah.
IMG_2839.jpeg
 
WANANCHI, mechi yetu dhidi ya Mtani wetu SIMBA imeisha leo hii kwa msimu wa 2024/25 raundi ya pili na ieleweke vyema hakutakuwa na mechi nyingine sehemu nyingine, siku nyingine na tarehe nyingine yoyote ya kuihusu Yanga dhidi ya Simba kwa Ligi kuu, iwekwe sawa kwenye kumbukumbu na ikolezwe vyema kwa wino kuwa its done and dusted, sisi tunasonga mbele na ratiba zingine.” Arafat
View attachment 3264063
Anajifariji tu, kauli moja tu ya MAZA ikamtoa fei yanga sembuse mechi!!
Nehi
 
WANANCHI, mechi yetu dhidi ya Mtani wetu SIMBA imeisha leo hii kwa msimu wa 2024/25 raundi ya pili na ieleweke vyema hakutakuwa na mechi nyingine sehemu nyingine, siku nyingine na tarehe nyingine yoyote ya kuihusu Yanga dhidi ya Simba kwa Ligi kuu, iwekwe sawa kwenye kumbukumbu na ikolezwe vyema kwa wino kuwa its done and dusted, sisi tunasonga mbele na ratiba zingine.” Arafat
View attachment 3264063
Kwani hiyo tarehe wamecheza? Timu limejaa wendawazimu wengi Sana...Kawaida yenu kususa alafu mkibembelezwa kidogo Tu mnacheza. Kama Ile ya 2021 hata hii mtacheza tu....BY THE WAY MNA FAIDA GANI KIMATAIFA?
 
Waraka mreeefu kama mguu wangu wa tatu. Kwanza huu waraka ni kama wa timu iliyomaliza ligi kwa kukosa ubingwa. Embu soma tena. Waraka wa mwishoni mwa ligi umevuja!
 
Ndugu Wananchi kwa dhati ya moyo wangu niwapongeze kwa kufika uwanjani kutoka kona zote nchini, mliosafiri kwa anga, mliosafiri kwa magari, mliopanda Pikipiki, mliopanda boti hadi Watembea kwa miguu, yote ni kwa ajili ya Yanga Afrika, huu sio tu upendo bali mahaba ya kulevya kwa klabu hii bora zaidi nchini.

Ndugu Wananchi poleni mno kwa kadhia ya leo, sisi kama Viongozi mliotupa dhamana kusimamia hii chapa kwa niaba yenu tumepigana, tumehakikisha mawazo yenu, matakwa yenu na sauti yenu inasikika kwa sauti ya juu sana, kwa kuheshimu mpira wa miguu na kuheshimu uthubutu wenu tuliandaa na kuleta timu uwanjani tayari kwa kushindana ila yaliyotokea yametokea.

Ndugu Wananchi, poleni kwa kupoteza muda wenu, kwa kupoteza fedha zenu kwa ajili ya mechi hii kubwa na ya kihistoria, ninyi ni sisi na maumivu haya ni yetu sote kama ambavyo tumeimba pamoja, tumelia pamoja basi hata sasa mpaka milele tupo pamoja, hilo likae vyema kwenye kumbukumbu kuwa sisi ni Yanga.

WACHEZAJI na Benchi la Ufundi, asanteni kwa heshima mliowapa Wapenzi wa soka nchini bila kujali timu zao, mmehakikisha mpira wa miguu umeshinda, kuna wakati sio suala la Mshahara wala posho bali heshima kwa nembo ya Kijani na Njano, Asanteni Vijana kwa kufika na angalau Mashabiki wameweza kuwaona na kuwalaki.

WANANCHI, mechi yetu dhidi ya Mtani wetu SIMBA imeisha leo hii kwa msimu wa 2024/25 raundi ya pili na ieleweke vyema hakutakuwa na mechi nyingine sehemu nyingine, siku nyingine na tarehe nyingine yoyote ya kuihusu Yanga dhidi ya Simba kwa Ligi kuu, iwekwe sawa kwenye kumbukumbu na ikolezwe vyema kwa wino kuwa its done and dusted, sisi tunasonga mbele na ratiba zingine.

Hii ndio sauti yenu moja, kamba moja ya DAIMA MBELE, NYUMA MWIKO na tutashikilia hapo hapo Wananchi, niwatakie safari njema Wananchi wote kurejea makwenu, Mungu awalinde, awatunze mkaungane tena na familia zenu, tutakutana tena wakati mwingine panapo majaaliwa In shaa Allah.
View attachment 3264063
Utopolo ishushwe daraja,inaleta uhuni katika soka letu na kuaibisha taifa! mambo ya makomandoo sijui kuzuia timu kufanya mazoezi,huu ni ushenz kabisa
 
Back
Top Bottom