Ardhi ya Zanzibar ( Aricle 1 )

Ardhi ya Zanzibar ( Aricle 1 )

aleesha

JF-Expert Member
Joined
Oct 17, 2016
Posts
798
Reaction score
1,178
👉 Ardhi ni nini?

👉 Nani anasitahili kuilinda ardhi ya visiwa vya Zanzibar?

👉 Mmiliki ni nani?

👉 Nani anaweza kumiliki?

Kila nchi Duniani ina ardhi yake huenda matumizi ya ardhi katika kila nchi yanaweza kutofautiana kulingana na maamuzi yao.

Nchi zote Duniani zinaamini katika ardhi zao na sio rahisi kugusa ardhi yao kwa namna unavyotaka wewe! Uwe mzawa au mgeni.

Kwa wageni ndio hatari zaidi kuamua tu au kuchukua uwamuzi wao katika kujimilikisha hali ya kuwa ardhi ipo sehemu ambayo ina Kiongozi wake mkuu ambaye ni mkuu wa nchi pamoja na watendaji wengine wa serikali.

Lakini zaidi nchi Ina wananchi ambao ni wazawa na bila shaka wengi wao wanamiliki ardhi kwa namna tofauti.

UKubwa wa Visiwa vya Zanzibar ni 2,461 km².

Je Zanzibar ina mfumo wa ardhi yake ambao unaonyesha matumizi ya ardhi yake ni % ngapi?

Kwa lugha nyingine tafakuri inaweza kusimama katika asilimia ya ngapi ya ardhi ambayo imetumika katika maendeleo ya nchi?

Inawezekana Zanzibar kuna miradi mingi ambayo inatekelezwa na wageni,lakini je hoja ni majengo ambayo wageni wamejenga?

Labda ni sawa kuhoji maeneo ambayo wageni wanayamiliki huku hakuna mradi wowote unaoendelea? yawezekana wageni hao wamekwama kutokana na ile sheria ya serikali ambayo inasema mgeni akinunua ardhi iwe ni kwa ajili ya kuwekeza na sio kuishi tu?

Samahani! 🤚 naomba niwe wazi kidogo katika hiyo sheria, mimi ninaunga Mkono serikali ya nchi ya Zanzibar kwa 100%✊.

Ardhi ya Zanzibar ni ndogo kwa ukubwa wake kama inavyoonekana Ki Jiografia, kwa namna gani ardhi itolewe bila utaratibu maalum? tena kwa vigezo? .

Huenda bado kuna mwanya sehemu ambao unaruhusu wawekezaji FEKI kuamini kwamba wanaweza kumiliki ardhi Zanzibar.

Nani anayewabeba wageni FEKI ambao wanavaa Koti la uwekezaji hapa visiwani Zanzibar?

Yawezekana kuna wageni ambao wanamiliki maeneo na huwakuti ZIPA wala Kamisheni ya Utalii 😳 wageni wa namna hii wanachukuliwa hatua za namna gani?

Kuna shida mahali? au wazawa baadhi wanahusika ?

Nani atainusuru ardhi ya Zanzibar jamani? 😭😭

Shukran 🤝

NOTE: Natarajia kufanya mwendelezo zaidi kuhusu ardhi ya Zanzibar naamini nitapata ushirikiano zaidi kutoka kwenu!
 
ARDHI YA ZANZIBAR (2)

Ikiwa umuhimu wa kulinda ardhi ya Zanzibar utazingatiwa,basi cha kwanza ni kwamba ieleweke kwamba ardhi yake ipo LIMITED.

Maana yake hatuwezi kuongeza ukubwa Wa eneo kwa upande mmoja na huenda hata tukihitaji Hilo bado tutahitaji kujipanga katika 👉technology na knowledge ya kufanya reclamation ya bahari wenyewe.

Ni kweli kabisa kwamba Zanzibar iliwahi kufanya jambo hilo katika eneo la Darajani miaka ya nyuma sana kutoka company ya Netherlands/Holland.

Lakini je ni jambo rahisi sana? Kwamba halina gharama zake na fedha zitatoka wapi?

Suala jingine la kuzingatia kwenye utoaji wa ardhi Zanzibar ni suala la . Population growth ya Zanzibar.

kwamba idadi inaongezeka kila uchao na kuifanya Zanzibar kua high density population to compare with land.

Yaani ☝️ ile idadi ya watu inazidi ukubwa wa eneo! ndio maana ikiwa tutajikita kwenye kuangalia ardhi yake ni lazima kugusa pia kwenye uwekezaji. Kwamba ardhi wapewe wawekezaji ambao wako SIRIASI😣

3. Zanzibar kuna Mipango miji mizuri lkn tatizo kubwa ni enforcement/implementation.

kuna zaid ya Mipango miji 4 je tumewahi kujiuliza utekelezwaji wake?kwamba umefanyika kikamilifu? Kuna ripoti?

Haya yote kwa ujumla wake ndio yanapaswa kuzingatiwa ndani ya visiwa na ikiwa kuna kasoro zozote zile zikiachwa madhara yake ni makubwa sana kama ifuatavyo:-

1. Wazawa kutokana na ugumu Wa maisha na hali ya umasikini walionao watabakia kua hawana ardhi kwa ajili ya 👇

1. makaazi.
2. ⁠shughuli za kiuchumi na uzalishaji km vile kilimo, viwanda n.k

3. Maeneo ya kuzikia na kufanyia ibada.

4. Ukosefu Wa maeno ya wazi na michezo pamoja na mikusanyiko ya mikutano ya kisiasa, maafa na maombi ya jumla.

5. Kupoteza sifa za umiliki na matumizi ya ardhi hizo na kubakia kua ombaomba na kushindwa kuifanya kazi.

Unaweza kuona mifano halisi katika Vijiji ambavyo vipo nje ya manispaa ya mji wa Unguja. Kwamba wazawa hawana maeneo na hata maisha yao hayalingani na shughuli za uwekezaji uliopo pale.

Sikatai wamewauzia wenyewe wageni baadhi yao maeneo yao,lakini kwanini hakuna usimamizi kama ule wa Kamisheni ya utalii?

Kamisheni ya utalii mgeni ambaye anataka kupata hati ya umiliki wa eneo ni lazima awe na mzawa! Mzawa atamiliki 70% na mgeni 30%.

Ikiwa mgeni anaona hilo sio sawa kwake,kuna ZIPA ambayo ipo kwa ajili yao.kwamba hapo hahitaji kuwa patina na mzawa.

Sasa hata kwenye uuzaji wa maeneo wenyeji wajengewe Mazingira mazuri pia.

Shukran

Nitaendelea.
 
Hapo ndio umuhimu wa Tanganyika unaapo onekana, miaka 100, 200, 500 ijayo maisha yakiwepo hivyo visiwa
 
Back
Top Bottom